SUPA JACKPOT BONUS YAENDA MOSHI-Ni Tsh 9, 260,274
Mkazi wa Moshi mjini, Geofrey Damas Sindato kutoka Moshi, mkoa wa Kilimanjaro, wiki iliyopita alijishindia kitita cha Tshs 9, 260, 274 kama bonus ya Jackpot ya mwisho wa wiki, baada ya kubashiri na kupatia kwa usahihi mechi 14 kati ya mechi 17 za Supa Jackpot ya SportPesa.
Akizungumza katika ofisi za SportPesa, oysterbay jijini Dar-Es-Salaam, Geofrey anasema alianza kucheza na sportPesa kuanzia Mwaka 2019, baada ya kuona na kusikia kuhusu matangazo ya washindi wa bonus za SportPesa.
“Nilianza kucheza na SportPesa miaka minne iliyopita. Nakumbuka wakati ule kulikuwa na washindi ambao walikuwa wanatangazwa kupitia vyombo vya habari na sisi wananchi kutangaziwa kwa nji mbali mbali.’’.
Mbali na hilo mimi nilivutiwa na kampuni hii kwa sababu kwa kipindi kile SportPesa walikuwa wanadhamini timu za Simba na Yanga, ambazo ni za hapa Tanzania, na kwa wakati huo huo walikuwa wanadhamini Everton ya Uingereza.
Kwa kuwa na mimi napenda mpira kitendo cha kujua kampuni hii ya SportPesa inadhamini timu yangu na pia inadhamini timu za ligi kuu Uingereza, hilo lilinipa imani kwamba lazima hawa SportPesa ni kampuni kubwa na ya kuaminika, hivyo uhakika wa malipo ni mkubwa vilev ile’’.
Anaendelea kuelezea kuwa baada ya muda kupita tangu aone tangazo la mshini wa alikuwa akikutana na washkaji zake ambao walikuwa wanacheza, hivyo aliwaomba wamfundishe mpaka alipojua kucheza ama kubashiri yeye mkeka ulioshinda.
Akiongelea Geofrey anasema kwanza huwa na kawaida ya kufuatilia mikeka ya Jackpot ya SportPesa ya kati kati ya wiki na ya mwisho wa wiki (Supa Jackpot) kuanzia kila Jumatatu mpaka labda jumatano.
Baada ya hapo hutumia kama siku mbili kufanya uchambuzi wa na kufanya maamuzi ni kwa namna gani aweke mkeka au mikeka.
“Mimi huwa na kawaida ya kuweka ama kubashiri mikeka miwili ila inapotoka. Sasa wiki iliyopita nilifuatilia mikeka siku ya Jumatatu kupitia magazeti na kwenye simu yangu. Baaada ya hapo niliweka mikeka 2 tu.
Nilipoweka mikeka hiyo sikuwa na hamu ya kufutilia matokeo ya timu zilipoanza kucheza, ila ninachoweza kukumbuka kwa ufasaha ni kwamba baada ya kuweka mikeka hii sikufuatilia mwenendo wa matokeo.
Nilkuja kupata sms kutoka SportPesa, siku iliyofuata majira ya asubuhi, ikinipa hongera kwa kushinda 9, 260, 274 kama zawadi ya Supa Jackpot bonus. Wakati nimepokea sms ile sikuamini kama ni kweli nimeshinda’’. Aanasema Geofrey.
Anaendelea kusema kwamaba aliikagua ile meseji ya ushindi mara mbili mbili na baada ya kujiridhisha na kiwango cha ushindi alijaribu kutaka kuhamisha pesa kutoka kwenye akaunti ya SportPesa kwenda kwenye Airtel Money yake lakini alishindwa.
‘’Baada ya kama dakika 45, kupita mtoa huduma kwa wateja wa SportPesa nilipigiwa simu na kujulishwa kama nimeshinda 9, 260, 274 na kwa wakati ule nisingeweza kufanya chochote ikiwemo kutoa au kuhamisha pesa kutoka kwenye akaunti yangu ya SportPesa mpaka nitakapokuja makao makuu kwa ajili ya uhakiki na taratibu nyingine za ki utawala.
Nilifurahi kuongea na mtoa huduma kwa kuwa nilipata uhakika wa malipo na baada ya hapo nilianza mchakato wa kuja Dar-Es-Salaam na kufanikiwa kufika leo na namshukuru Mungu nimeshapitia hatua zote za uhakiki, kujaza fomu na pia kupiga picha ya makabidhiano ya mfano wa hundi’’.
Geofrey anasema pesa ya aliyoshinda ataweka sehemu ya pesa ya ushindi wake katika ujenzi wa mji wake na pia pesa nyingine atawekeza kama mtaji kwenye shughuli zake za ujasiriamali.
Akizungumzia ushindi wa Geofrey, Mkuu wa mawasiliano wa kampuni ya SportPesa Sabrina Msuya alimpongeza Geofrey kwa ushindi wa bonus ya Supa Jackpot na kumtaka aendelee kupambania ndoto yake ya kushinda Supa Jackpot ya bilioni moja.
‘’Kwanza karibu SportPesa. Pili nachukua nafasi hii kukupongeza kwa ushindi wa bonus ya Supa Jackpot na tatu anapenda kukuasa uendelee kucheza kadiri uwezavyo, kwani kama walivyokuwa washindi wengine waliopita, unaweza kushinda zaidi ya mara moja.
Wewe mwenyewe umesema hapo awali kwamba ulishawahi kushinda siku za nyuma 250,000 kwenye Jackpot ya mechi 13 na pia umeshawahi kushinda 10,000, 5000- katika multibet.
Nachukua nafasi hii pia kuwakumbusha watanzania kwamba Jackpot yetu ya Supa Jackpot inazidi kupanda, Mzigo kwa wiki hii umesimamia TZS 598, 498, 850.