Yanga SC itafungwa na nani 2025/26Captain Nondo
  • Yanga SC itafungwa na nani 2025/26 NBC Premier League?
  • Kariakoo Dabi ft: Simba SC 2-2 Yanga SC, Mei 3, 2026 Uwanja wa Meja Jeneral Isahmuyo.
  • Goncalves ajivunia wachezaji wa timu hiyo kutokana na kutimiza majukumu yao

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26 NBC Premier League? Hii ni baada ya kufikisha mechi 20 mfululizo bila kufungwa. Matokeo ya mchezo uliopita Mei 2, 2026 Uwanja wa Meja Jeneral Isahmuyo ilikuwa Simba SC 2-2 Yanga SC. Mnyama alianza kufunga ndani ya dakika 10 kisha Wananchi wakarudisha goli mojamoja kila kipindi.

SOMA HII: Yanga SC na maajabu 2025/26 | Matokeo ya hivi punde, wafungaji na msimamo NBC Premier League

Paisha Kindege cha SportPesa uvune mamilioni sasa hivi

Muda ni sasa kushinda mamilioni ukicheza mchezo wa Aviator. Ni rahisi sana kwa kila rubani kuvuna mamilioni. Cheza sasa upate mgao wako bila chenga ni rahisi sana

Sportpesa Aviator- 800Mil

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26 NBC Premier League?

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26
Prince Dube na Pacome kwenye mchezo wa NBC Premier League.

Je Yanga SC itafungwa na nani 2025/26 NBC Premier League? Mnyama alikuwa anapewa nafasi kuvunja rekodi hiyo amekwama. Katika mechi mbili walizokutana walitoshana nguvu mzunguko wa kwanza ni sare ya 0-0.

Mabingwa watetezi wamepata ushindi mechi 14 na sare mechi 6. Ni timu nyingine ambayo haijapoteza ni Azam FC. Ikumbukwe kwamba Yanga SC 2021/22 walitwaa taji wakiwa ni unbeaten. Endelea kubashiri mechi zilizobaki uvune mkwanja na SportPesa.

Wananchi wana rekodi ya kuwa na unbeaten 49 misimu mitatu mfululizo. Kuanzia 2020-21, 21-22 na ilivunjwa 2022/23 kwa kufungwa 2-1 na Ihefu Novemba 29, 2022. Je 2025/26 rekodi itadunda?

SOMA HII: Yanga SC Unbeaten NBC Premier League 2025/26: Haya hapa Matokeo yote na rekodi za Wananchi msimu huu, Azam hawavumi lakini wamo

Aviator game promotional banner featuring a red propeller plane and a jackpot of 800,000,000.

Matokeo ya Yanga SC 2025/26

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26
Dube na De Reuck

Pedro Goncalves, Kocha Mkuu wa Yanga SC anajivunia wachezaji wa timu hiyo kutimiza majukumu kwa kujituma. Mbele ya Simba SC walitoka nyuma wakifungwa magoli 2-0 na mwisho wakasawazisha. Ni Libase Gueye na Clatous Chama walifunga ndani ya dakika 10 za mwanzo kwa wenyeji.

Prince Dube na Bakari Nondo walifunga kwa Yanga SC. Matokeo hayo yanaifanya timu hiyo kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi 5. Kipigo kikubwa walichotoa ni magoli 6-0 ilikuwa dhidi ya Mbeya City na Mashujaa.

Hapa tunakuletea matokeo ya mechi 20 za Yanga SC NBC Premier League. Kinara wa ufungaji magoli ni Prince Dube amefunga 9. Huyu ni raia wa Zimbabwe anaongoza kutwaa tuzo za Man of the Match akiwa nazo 3.

TareheTimu (H)MatokeoTimu (A)
Aprili 16, 2026Yanga SC6-0Mbeya City
Aprili 8, 2026Pamba Jiji FC Yanga SC
April 4, 2026Yanga SC3-0  Tanzania Prisons
March 21, 2026Mtibwa Sugar1-1  Yanga SC
March 18, 2026TRA United0-0  Yanga SC
March 15, 2026Azam FC0-0  Yanga SC
March 12, 2026Tanzania Prisons0-1  Yanga SC
March 5, 2026Singida Black Stars0-3  Yanga SC
March 1, 2026Yanga SC0-0  Simba SC
Feb 25, 2026Yanga SC5-0  JKT Tanzania
Feb 22, 2026Namungo FC0-1  Yanga SC
Jan 27, 2026Yanga SC3-1Dodoma Jiji  
Jan 19, 2026Yanga SC6-0  Mashujaa
Dec 7, 2026Coastal Union0-1  Yanga SC
Dec 4, 2026Yanga SC2-0  Fountain Gate
Nov 9, 2026Yanga SC4-1KMC  
Oktoba 28, 2026Yanga SC2-0Mtibwa Sugar  
Sep 30, 2026Mbeya City0-0  Yanga SC
Sep 24, 2026Yanga SC3-0  Pamba Jiji FC
Mei 3,2026Simba SC2-2Yanga SC

Msimamo wa NBC Premier League 2025/26

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26
Okello kiungo mshambuliaji wa Yanga SC

 Msimamo wa NBC Premier League uliobereshwa hivi punde. Yanga SC wanaongoza ligi na pointi 48. Simba SC nafasi ya pili ina pointi 43.

POSMPWDLPTS
Yanga SC20146048
Simba SC20127143
3. Azam FC201010040
4. JKT Tanzania2088432
5.TRA United2086630
6.Pamba Jiji2078529
7.Singida Black Stars2085729
8. Dodoma Jiji FC2067725
9.Namungo FC2058723
10.Mtibwa Sugar2058723
11.Coastal Union2057822
12. Mashujaa20410622
13.Fountain Gate20541019
14.Mbeya City20461018
15.Tanzania Prisons20351214
16. KMC FC2023159

SOMA HII: Yanga SC haina utani kuwapa mikataba mastaa hawa wa kazi 2025/26

Hitimisho

Yanga SC itafungwa na nani 2025/26 NBC Premier League? Kwa sasa ni mzunguko wa pili mechi 10 zimesalia msimu kufika tamati. Wananchi wamekuwa na safu bora ya ulinzi wakiruhusu magoli matano na safu ya ushambuliaji imefunga magoli 46.

Share this: