KMC FC inaburuza mkiaKMC FC vs Azam FC
  • KMC FC inaburuza mkia 2025/26 ipo kwenye hatari ya kushuka daraja
  • Mechi iliyopita matokeo yalikuwa KMC FC 1-1 Tanzania Prisons, Uwanja wa KMC Complex
  • Ipo nafasi ya 16 ikipata ushindi katika mechi 2 kati ya 19, vipigo mechi 14, sare 3 NBC Premier League
  • Kocha Maximo alifungashiwa virago mrithi wa mikoba yake Bares naye akafuata

KMC FC inaburuza mkia 2025/26 katika msimamo wa NBC Premier League. Haijawa na matokeo mazuri katika mechi za ushindani. Mchezo uliopita ikiwa nyumbani ubao ulisoma KMC FC 1-1 Tanzania Prisons. Ipo katika hatari ya kushuka daraja.

SOMA HII: KMC 0-2 Simba SC, Umeona msimamo wa Ligi Kuu, ratiba ya NBC?

Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Hujashinda na SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

SportPesa Aviator Challenge

KMC FC inaburuza mkia 2025/26, haya hapa matokeo yake

KMC FC inaburuza mkia
Saliboko Daruesh nyota wa KMC FC.

KMC FC inaburuza mkia 2025/26 kwenye msimamo wa NBC Premier League. Baada ya mechi 19 imepata ushindi mechi 2 pekee ikipoteza mechi 14. Ina sare 3 ni timu inayoongoza kwa kupokea vipigo kwenye mechi nyingi.

Inaweza kushuka daraja ikiwa haiatapata matokeo mazuri kwenye mechi zilizobaki mzunguko wa pili. Ikiwa itaendelea kupoteza ama kupata sare itakwenda kushiriki Championship. Inatumia Uwanja wa KMC Complex kwa mechi za nyumbani.

Haya hapa matokeo ya KMC FC 2025/26

TareheMechiMatokeo
Aprili 14, 2026KMC FC vs Tanzania Prisons1-1
Aprili 8, 2026Singida Black Stars vs KMC FC1-0
Aprili 3, 2026Mbeya City vs KMC FC3-2
Feb 22, 2026KMC FC vs Azam FC0-2
Feb 11, 2026KMC FC vs Simba SC0-2
Feb 8, 2026Dodoma Jiji FC vs KMC FC2-1
Feb 3, 2026KMC FC vs Mashujaa FC1-0
Jan 31, 2026Namungo FC vs KMC FC1-0
Jan 27, 2026Coastal Union vs KMC FC1-1
Jan 23, 2026TRA United vs KMC FC3-0
Nov 25, 2025Pamba Jiji FC vs KMC FC3-0
Nov 25, 2025KMC FC vs Mtibwa Sugar0-0
Nov 21, 2025KMC FC vs JKT Tanzania0-1
Nov 9, 2025Yanga SC vs KMC FC4-1
Okt 25, 2025Fountain Gate vs KMC FC1-0
Okt 18, 2025KMC FC vs Mbeya City0-3
Sep 27, 2025Tanzania Prisons vs KMC FC1-0
Sep 23, 2025KMC FC vs Singida Black Stars0-1
Sep 17, 2025KMC FC vs Dodoma Jiji FC1-0

SOMA HII: Yanga SC Unbeaten NBC Premier League 2025/26: Haya hapa Matokeo yote na rekodi za Wananchi msimu huu, Azam hawavumi lakini wamo

SportPesa Aviator Challenge

Mechi alizopata ushindi KMC FC

KMC FC inaburuza mkia
Baraka Majogoro kiungo wa KMC FC.
TareheMechiMatokeo
Feb 3, 2026KMC FC vs Mashujaa FC1-0
Sep 17, 2025KMC FC vs Dodoma Jiji FC1-0

Kocha afungashiwa virago

Aprili 3, 2026 KMC FC ilifikia makubaliano ya kusitisha mkataba wa Abdalah Mohamed maarufu kwa jina la Bares. Mchezo wa mwisho kwa benchi la ufundi kuongoza ilikuwa Mbeya City 3-2 KMC FC. Imani Mwalupetelo anaongoza benchi la ufundi kwa sasa.

Anakuwa ni kocha wa pili kufutwa kazi. Mwanzo wa msimu ni Marcio Maximo alianza kukinoa kikosi hicho raia wa Brazil. Mkataba wake ulisitishwa rasmi Desemba 6, 2025.

SOMA HII:Yanga SC haijafungwa mechi 19 NBC Premier League 2025/26 | Matokeo na msimamo

Hitimisho

KMC FC inaburuza mkia 2025/26 katika ligi namba 6 kwa ubora Afrika. Safu ya ushambuliaji imefunga magoli 8 ambayo ni machache kuliko timu zote. Ukuta umeruhusu kufungwa magoli 30.

Share this: