- Ni Simba SC vs Pamba Jiji FC NBC Premier League Juni 14, 2026, Uwanja wa KMC Complex.
- Mzunguko wa kwanza ubao wa Uwanja wa Kirumba ulisoma Pamba Jiji FC 1-1 Simba SC
- H2H Simba SC imepata ushindi kwenye mechi 2 na sare 1
Ni Simba SC vs Pamba Jiji FC NBC Premier League Juni 14, 2026 ni ratiba inayofuata mzunguko wa pili. Mnyama amekutana mara moja na Pamba Jiji FC ndani ya ligi walipofungana 1-1. Wababe hawa wanatarajiwa kukutana Jumapili 16:00 UTC.
Bado hujashinda mamilioni ya SportPesa?
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Bashiri na SportPesa uvune mkwanja sasa hivi kwa kubonyeza picha hapo chini.

Kivumbi cha Simba SC vs Pamba Jiji FC kupigwa KMC Complex


Wababe wawili Simba SC vs Pamba Jiji FC kivumbi chao ni Uwanja wa KMC Complex katika mchezo ujao wa ligi. Hii ni vita ya kuwania kutwaa ubingwa na kuwa ndani ya 10 bora. Mnyama yupo nafasi ya pili kwenye msimamo akiwa na pointi 58 huku wapinzani nafasi ya 7 na pointi 33.
Ushindi kwa Simba SC utaongeza nguvu kuzidi kuifukuzia Yanga SC iliyo nafasi ya kwanza na pointi 60. Ikiwa wageni watapata pointi 3 wataongeza uwezekano kumaliza ligi ndani ya 10. Hii ni mechi kali inayosubiriwa kwa shauku kubwa.
Rekodi ya Mechi za Pamba Jiji FC dhidi ya Simba SC
| Tarehe | Timu Nyumbani | Matokeo | Timu Wageni |
|---|---|---|---|
| 19/03/2026 | Pamba Jiji FC | 1 – 1 | Simba SC |
| 08/05/2025 | Simba SC | 5 – 1 | Pamba Jiji FC |
| 22/11/2024 | Pamba Jiji FC | 0 – 1 | Simba SC |
Muhtasari wa Takwimu
| Kipengele | Pamba Jiji FC | Simba SC |
|---|---|---|
| Mechi Zilizochezwa | 3 | 3 |
| Ushindi | 0 | 2 |
| Sare | 1 | 1 |
| Kufungwa | 2 | 0 |
| Magoli Yaliyofungwa | 2 | 7 |
| Magoli Yaliyoruhusiwa | 7 | 2 |
Wachezaji wakuchungwa
Kuelekea mchezo ujao kwa wawili hawa kuna wachezaji wakali wakuchungwa kila timu. Hii inatokana na uwezo walionao uwanjani. Wenyeji chini ya Kocha Mkuu, Steve Barker wamekuwa na mwendelezo wa matokeo mazuri, hawa hapa wachezaji muhimu:-
Clatous Chama

SOMA HII: Pamba Jiji FC waigomea Simba SC NBC Premier League/ Highlights, statics, standings, goal
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC amekuwa tegemeo eneo la kiungo. Magoli 8 aliyofunga kwenye ligi yanampa nguvu kuwa kwenye mwendelezo bora. Kwenye mchezo dhidi ya Dodoma Jiji FC alikosa penalti iliyosababishwa na Ellie Mpanzu.
Mpanzu
Ellie Mpanzu aliandika rekodi kutwaa tuzo ya mchezaji bora dhidi ya Dodoma Jiji FC ikiwa ni mara ya kwanza. Alisababisha penati a alifunga goli. Hivyo ni mchezaji mwenye hatari akiwa uwanjani.
Seleman Mwalimu
Huyu ni mshambuliaji wa Simba SC. Magoli 8 amefunga akiwa ni mshambuliaji pekee ndani ya kikosi cha mnyama. Amekuwa imara zaidi akianzia sub kutokana na mbinu za mwalimu.Je mchezo ujao ataanza kikosi cha kwanza?
Yona Amos
Huyu ni mlinda mlango namba moja wa Pamba Jiji FC.Miongoni mwa nguzo imara kwenye kupambania ulinzi ndani ya lango.Wachezaji wa Simba SC watakuwa na kazi kubwa kupenya kwenye nyavu za kipa huyu ikiwa ataanza langoni kutokana na uwezo alionao.
Mathew Tegisi
Kiungo mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa kwenye kucheka na nyavu. Wakati ubao wa Kirumba ukisoma Pamba Jiji FC 2-3 Tanzania Prisons alifunga magoli 2. Alifunga goli la ushindi dhidi ya KMC FC, kwenye mechi 2 mfululizo kafunga magoli 3. Huyu anajua kufunga hivyo ana hatari asipochukwa.
Zabona
Uzoefu kwenye ligi unampa nguvu kuwa mhimili ndani ya kikosi cha Pamba Jiji FC. Ni miongoni mwa wachezaji muhimu kwenye mechi za ushindani. Kocha Mkuu wa Pamba Jiji Francis Baraza amekuwa akimpa majukumu mara kwa mara uwanjani.
Hitimisho
Burudani inarejea huku Simba SC vs Pamba Jiji FC NBC Premier League ikiwa ni mechi inayotazamiwa kuwa na ushindani mkubwa. Mnyama anapambania pointi 3 kuwania ubingwa huku Pamba Jiji FC anapigania kuwa 10 bora. Je nani ataibuka mshindi mchezo ujao? Endelea kufuatilia SportPesa Blog.

