Yanga SC 2-1 Gaborone United CAF Champions League | Highlights | SportPesa Blog

ByLunyamadizo Mlyuka

September 13, 2026
Yanga SC 2-1 Gaborone United CAF Champions LeagueShalulile PShalulile P
  • FT: Yanga SC 2-1 Gaborone United CAF Champions League 2026/27
  • Peter Shalulile na Toure wamewafungashia virago Wabotswana katika hatua ya awali
  • SportPesa Blog tumekuletea takwimu na rekodi za wafungaji

Ni Yanga SC 2-1 Gaborone United CAF Champions League 2026/27 matokeo rasmi mchezo wa hatua ya awali Uwanja wa Azam Complex. Wananchi wametinga hatua inayofuata kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2. Mchezo wa kwanza Botswana ilikuwa 1-1.Septemba 12, 2026 kete muhimu ilikuwa kwa upande wa Yanga SC inayosonga mbele hatua inayofuata.

Gaborone United vs Yanga SC: Gaborone United 1-1 Yanga SC CAF Champions League | Highlights | H2H | Seleman Mwalimu goal | SportPesa Blog

Je, bado hujashinda mamilioni ya aviator ‘Kindege’ cha SportPesa? Cheza ushinde mamilioni sasa

Changamka! sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Yanga SC 2-1 Gaborone United taarifa muhimu

Yanga SC 2-1 Gaborone United CAF Champions League
Nyota wa Yanga SC wakishangilia ushindi dhidi ya Gaborone United

Yajue matokeo ya Yanga SC CAF: Matokeo ya Yanga SC CAF Champions League 2025/26/ Standings, fixture

KipengeleMaelezo
MashindanoLigi ya Mabingwa Afrika
HatuaHatua ya awali
TareheSeptemba 12, 2026
UwanjaAzam Complex, Dar
MatokeoYanga SC 2-1 Gaborone United

H2H Yanga SC vs Gaborone United CAF Champions League

TareheMatokeo
Septemba 5, 2026Gaborone United 1-1 Yanga SC
Septemba 12, 2026Yanga SC 2-1 Gaborone United

Yanga SC ilivyowaondoa Gaborone United CAF Champions League

Wawakilishi wa Tanzania katika anga la kimataifa Yanga SC wamewaondoa jumlajumla Gaborone United hatua ya awali. Katika mchezo wa pili wa marudio uliochezwa Uwanja wa Azam Complex wamepata ushindi wa mabao 2-1. Peter Shalulile alifungua pazia mapema dakika ya 7 kwa pasi ya SelemanMwalimu na Toure alifunga bao la pili dakika ya 83.

Bao pekee la Gaborone United limefungwa na Ditsele dakika ya 87. Ushindi huu kwa Yanga SC unawafanya wasonge hatua inayofuata kwa jumla ya mabao 3-2. Hatua inayofuata itacheza dhidi ya CFFA ya Madagascar.

Hitimisho

Yanga SC 2-1 Gaborone United matokeo muhimu kwa wenyeji kusonga mbele hatua inayofuata. Shukrani kwa Shalulile ambaye alifunga bao la ufunguzi akitumia pasi ya Seleman Mwalimu. Siku hiyo ilikuwa maalumu ilipewa jina la Sele Day kwa kuwa alifunga bao kwenye mchezo uliopita ugenini. Gaborone United safari yao inaishia katika ardhi ya Tanzania msimu wa 2026/27 mpaka wakati mwingine tena.

Share this: