Goli la Mwalimu vs MlandegeGoli la Mwalimu vs Mlandege

Simba SC vs Tanzania Prisons | Ratiba, matokeo, msimamo, NBC Premier League, utabiri, Livescore, h2h, na Habari za timu

  • Simba SC vs Tanzania Prisons moto utawaka kesho Jumapili 10/5/2026, ni katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Bara (NBC Premier League).
  • Kwa mara ya kwanza msimu huu Simba SC watatumia Uwanja wa KMC Complex, kama uwanja wao wa nyumbani.
  • Hii ni mara baada ya muda mrefu, kutumia Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.
  • Ikumbukwe mara ya mwisho timu hizo kukutana matokeo yalikuwa Tanzania Prisons 0-2 Simba SC tarehe 22/2/2026.

Simba SC vs Tanzania Prisons kitawaka kesho Jumapili 10/5/2026, ni katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Bara (NBC Premier League). Mechi hii itapigwa kwenye Uwanja wa KMC, ambapo hii inakuwa mara ya kwanza msimu huu kwa Simba SC kutumia uwanja huo kama uwanja wao wa nyumbani. Hii ni mara baada ya muda mrefu, kutumia Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo. Ikumbukwe mara ya mwisho timu hizo kukutana matokeo yalikuwa Tanzania Prisons 0-2 Simba SC tarehe 22/2/2026.

Fuatilia mwenendo wote wa mashindano ya Ligi Kuu Bara ‘NBC Premier League’ 2025/26; Ratiba, matokeo, mechi, magoli na habari za papo kwa papo kupitia SportPesa Blog.

Je, unataka kushinda mamilioni? Unaweza kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 na SportPesa

Wengi tayari wamevuna mamilioni kupitia mchezo wa Kindege yaani ‘Aviator’ ya SportPesa. Wewe unasubiri nini? Nafasi ni yako cheza Aviator na kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 sasa kwa kubonyeza picha hii chini.

SportPesa Aviator Challenge

Aviator: Paisha kindege ushinde mpaka zaidi ya 800,000,000.

Simba SC vs Tanzania Prisons h2h

Mligo wa Simba SC akipambana na mchezaji wa Mafunzo SC
Mligo wa Simba SC kwenye moja ya mechi za timu hiyo

Timu hizi zimekutana katika mechi 28 za ushindani, ambapo Simba SC wameshinda mechi 18, na Tanzania Prisons wameshinda mechi 6. Mechi 4 katika mikutano yao ziliisha kwa matokeo ya sare. Mchezo huu ni muhimu kwa Simba SC katika kuimarisha dhamira yao ya kupambana na Yanga SC, katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

SOMA HII PIA: Ratiba ya Simba SC NBC Premier League 2025/26 ni moto | Msimamo, Mzizima Dabi, Kariakoo Dabi

Simba kwenye nafasi ya 2 msimamo wa Ligi Kuu Bara (NBC Premier League)

Mpaka sasa Simba SC wanakamatia nafasi ya 2 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara (NBC Premier League), hii ni baada ya kukusanya pointi 46 katika michezo 21. Simba SC imeshinda mechi 13, sare mechi 7 na kupoteza mechi moja tu. Katika michezo hiyo Simba imefunga mabao 35 na kuruhusu mabao 9 tu. Hii inaelezewa na jedwali lifuatalo;

NafasiTimuMechiUshindiSareVipigoMagoli ya Kufunga/KufungwaTofauti ya MagoliPointi
1Young Africans21156047:5+4251
2Simba21137135:9+2646
3Azam221110131:9+2243
4Singida Black Stars22105729:23+635
5TRA United2296727:20+733
6JKT Tanzania2188521:21032
7Pamba2178622:22029
8Dodoma Jiji2177719:21-228
9Mashujaa22511611:17-626
10Namungo2259817:23-624
11Mtibwa Sugar2258916:29-1323
12Coastal Union22571020:27-722
13Fountain Gate21641114:30-1622
14Mbeya City21561018:31-1321
15Tanzania Prisons21351311:28-1714
16Kinondoni MC2123168:32-249

Ratiba ya mechi 5 zijazo za Simba SC

Zimesalia mechi chache kumaliza msimu huu wa 2025/26, na hapa chini ni jedwali la Ratiba ya Simba ya mechi zilizosalia. Kila mechi hapa inabeba pointi 3 muhimu katika vita ya ubingwa wa ligi. Simba SC wanataka kushinda ubingwa huu baada ya kushuhudia watani wao wakiubeba misimu 4 mfululizo.

TareheMudaMechi
10 Mei 202619:00Simba vs Tanzania Prisons
14 Mei 202616:15Mashujaa vs Simba
21 Mei 202618:30Coastal Union vs Simba
24 Mei 202618:15Simba vs Dodoma Jiji
14 Juni 202619:00Simba vs Pamba
18 Juni 202616:00Mbeya City vs Simba
24 Juni 202616:00Mtibwa Sugar vs Simba
27 Juni 202616:00Simba vs Singida Black Stars
30 Juni 202616:00Simba vs Kinondoni MC

SOMA HII ZAIDI: Mzizima Dabi yaiachia maumivu Simba SC 2025/26 | Highlights, msimamo, h2h, ratiba mechi zijazo

Simba SC vs Tanzania Prisons makocha wanasemaje?

Simba SC

Namungo FC vs Simba SC NBC Premier League ni leo
Steve

Akizungumzia mchezo huo kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola amesema: “Hatuiangalii Prisons katika nafasi waliyopo, tunaangalia Prisons tunapokutana nao wanatupa mchezo wa namna gani. Mchezo kati yetu haujawahi kuwa mwepesi, hii ni kutokana na ubora walionao. Lakini malengo yetu ni kuchukua pointi 3 muhimu.”

Tanzania Prisons

Naye Kocha wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa amesema: “Kikosi cha timu yetu kipo kamili na tayari kuwakabili Simba SC kutokana na maandalizi tuliyofanya. Tumeusoma ubora wa mpizani wetu na tupo tayari kuzipigania alama tatu muhimu. Tunazitaka pointi hizi ili kuzidi kujiimarisha kwenye enezo zuri la msimamo.”

SOMA HII PIA: Simba SC vs Coastal Union NBC Premier League Aprili 2, 2026 | H2H, msimamo, live score

Kuhusu Simba SC kuhamia Uwanja wa KMC Complex

Simba SC vs Tanzania Prisons
Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo

Uongozi wa Simba SC alhamisi hii 7/5/2026 walitangaza rasmi kurejea Uwanja wa KMC. Simba SC wamerejea Uwanja wa KMC, baada ya muda mrefu msimu kutumia Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo. Akizungumzia uamuzi huo, Kocha Matola amesema kusema timu yao imehamia KMC Complex kwa kuwa uwanja Meja Jenerali Isamuhyo unaonekana kuzidiwa na uharibifu wa eneo la kuchezea.

Hitimisho

Yanga SC kumfukuza kocha Pedro Goncalves
Chama vs Diarra

Simba SC vs Tanzania Prisons ni mchezo ambao umekuwa ukitoa upinzani mkubwa, mara zote wanapokutana. Simba SC wanaingia katika mchezo huu wakiwa kwenye fomu nzuri, hii ni baada ya kuichapa JKT Tanzania bao 1-0. Kama Simba SC wataibuka na ushindi katika mchezo huu, watakuwa wamefikisha pengo la pointi 9 dhidi ya Azam walio nafasi ya 3.

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.