MotaMota
  • Kocha mpya Yanga SC ni nani? Hili ndio swali kubwa kwa wadau wa soka na hasa mashabiki wa Yanga SC.
  • Hii ni baada ya siku moja tu, tangu uongozi wa timu hiyo ulipotangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha wao mkuu, Pedro Goncalves.
  • Kocha Goncalves aliyempokea kijiti cha kocha, Roman Folz, alifutwa kazi muda mfupi baada ya kuwaongoza Wananchi kupata matokeo ya KMC 0-1 Yanga SC.
  • Majina mbalimbali tayari yamehusishwa kuchukua mikoba ya wa kocha mpya Yanga SC akiwemo kocha, João Paulo Mota Maria na Makala hii inamchambua kocha huyo.

Nani kuwa kocha mpya Yanga SC? Hili ndilo swali kubwa miongoni mwa wadau wa soka na hasa mashabiki wa Yanga SC. Hii inakuja ikiwa ni siku moja tu, imepita tangu uongozi wa timu hiyo ulipotangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha wao mkuu, Pedro Goncalves. Kocha huyo aliyempokea kijiti kocha, Roman Folz, alifutwa kazi muda mfupi baada ya kuiongoza timu hiyo kupata matokeo ya KMC 0-1 Yanga SC. Majina mbalimbali tayari yamehusishwa kuwa kocha mkuu mpya, akiwemo kocha João Paulo Mota Maria.

Fuatilia mwenendo wote wa mashindano ya Ligi Kuu Bara ‘NBC Premier League’ 2025/26; Ratiba, matokeo, mechi, magoli na habari za papo kwa papo kupitia SportPesa Blog.

Je, unataka kushinda mamilioni? Unaweza kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 na SportPesa

Wengi tayari wamevuna mamilioni kupitia mchezo wa Kindege yaani ‘Aviator’ ya SportPesa. Wewe unasubiri nini? Nafasi ni yako cheza Aviator na kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 sasa kwa kubonyeza picha hii chini.

SportPesa Aviator Challenge

Aviator: Paisha kindege ushinde mpaka zaidi ya 800,000,000.

Kocha mpya Yanga SC ni João Mota? Je, Joao Mota ni nani?

Kocha Joao Mota
Kocha Joao Mota

Jina lake kamili ni João Paulo Mota Maria, ni mzaliwa wa Portugal Lisboa, nchini Ureno ambapo alizaliwa tarehe 16/09/1966, hii inamfanya sasa kuwa na umri wa miaka 59. Kocha huyu ana wastani wa 0.64 kufundisha timu. Kocha huyu anapendelea zaidi soka lenye balansi ya kulinda na kushambulia, ambapo hupendelea mfumo wa 4-2-3-1. Kocha huyu anasimamiwa na taasisi ya uwakala ya Arab Africano na kwa sasa anafundisha kikosi cha Al Ittihad inayoshiriki Ligi daraja la pili Falme za kiarabu UAE, ambayo alijiunga nayo tarehe 22/9/2025.

SOMA HII PIA: Romain Folz kocha mpya Yanga SC mwenye CV kubwa | Wachezaji wenye uhakika 2025/26

Historia yake kisoka

Kocha Mota
Kocha Mota

Kocha Joao Mota kama ilivyo kwa makocha wengine, naye amepata nafasi ya kucheza soka katika ngazi mbalimbali. Timu yake ya mwisho ya klabu kuichezea ni Lagoa ya Ureno, japo timu aliyoichezea mechi nyingi zaidi ni União Madeira ya jukuhuko Ureno. Rasmi alistaafu kucheza soka tarehe 01/04/2000. Jedwali hilli linaonyesha historia ya timu alizowahi kucheza kocha huyo, enzi ya ujana wake;

MsimuTareheKlabu AliyoondokaKlabu AliyojiungaAina ya Uhamisho
1999/200001 Aprili 2000LagoaKustaafu SokaKustaafu
1999/200001 Julai 1999BejaLagoaUhamisho wa Bure
1998/199901 Julai 1998Câmara LobosBejaUhamisho wa Bure
1995/199601 Julai 1995TorreenseCâmara LobosUhamisho wa Bure
1993/199401 Julai 1993MontijoTorreenseUhamisho wa Bure
1992/199301 Julai 1992LouletanoMontijoUhamisho wa Bure
1991/199201 Julai 1991LeiriaLouletanoUhamisho wa Bure
1990/199101 Julai 1990União MadeiraLeiriaAda Haikujulikana
1988/198901 Julai 1988Sporting CPUnião MadeiraAda Haikujulikana
1987/198830 Juni 1988União MadeiraSporting CPMwisho wa Mkopo
1987/198801 Julai 1987Sporting CPUnião MadeiraUhamisho wa Mkopo
1986/198730 Juni 1987O ElvasSporting CPMwisho wa Mkopo
1986/198702 Julai 1986Sporting CPO ElvasUhamisho wa Mkopo
1986/198701 Julai 1986Sporting U19Sporting CPKupandishwa Kikosi cha Wakubwa
1985/198630 Juni 1986União MadeiraSporting U19Mwisho wa Mkopo
1985/198601 Julai 1985Sporting U19União MadeiraUhamisho wa Mkopo
1984/198501 Julai 1984Barreirense U19Sporting U19Ada Haikujulikana

SOMA HII ZAIDI: Kocha mpya Yanga SC huyu hapa, kuiwahi mechi ya Yanga SC vs Silver Strikers Jumamosi?

Historia ya baadhi ya timu alizowahi kufundisha

Kocha mpya Yanga SC
Baadhi ya timu alizopita

Kocha, João Paulo Mota Maria ni mzoefu wa soka la kimataifa ambapo, amewahi kuwa kocha wat imu nyingi kama inavyoonyeshwa kwenye jedwali hili;

Msimu / KipindiKlabu / TimuNafasiTarehe ya KuanzaTarehe ya KuondokaMechiPointi kwa Mechi (PPM)
2025/2026Al-Ittihad SCKocha Mkuu22 Septemba 2025Anaendelea0.00
2025/2026Saham ClubKocha Mkuu31 Agosti 202521 Septemba 202520.50
2024/2025Al-Hussein SCKocha Mkuu25 Septemba 202419 Aprili 2025222.09
2024/2025Al-Tadamon SCKocha Mkuu1 Julai 202424 Septemba 20240.00
2023/2024Sudan National Football TeamMratibu wa Timu9 Mei 202430 Juni 20240.00
2023/2024Al-Jabalain FCKocha Mkuu11 Februari 202430 Aprili 202461.00
2022/2023 – 2023/2024Al-Hussein SCKocha Mkuu15 Aprili 20239 Februari 20240.00
2022/2023GE JuventusKocha Mkuu30 Machi 20236 Aprili 20230.00
2022/2023DC Motema PembeKocha Mkuu18 Desemba 202219 Januari 20230.00
2021/2022Al-Hilal ClubKocha Mkuu10 Novemba 202130 Juni 202260.67
2021/2022Al-Hilal ClubKocha Msaidizi1 Julai 20219 Novemba 20210.00
2020/2021Botafogo FC BuéaKocha Mkuu1 Mei 202130 Juni 20210.00
2020/2021EC Tigres do BrasilKocha Mkuu1 Januari 202130 Aprili 20210.00
2020/2021Rio Branco FCKocha Mkuu1 Julai 202030 Novemba 20200.00
2019/2020Saudi Arabia U20Kocha Mkuu1 Novemba 201930 Juni 20200.00
2018/2019Rio Branco FCKocha Mkuu1 Desemba 201830 Juni 201911.00
2017/2018 – 2018/2019Portuguesa U20Kocha Mkuu1 Machi 201830 Septemba 20180.00
2017/2018AD GuarulhosKocha wa Vijana1 Septemba 201728 Februari 20180.00
2016/2017Al-Khaleej FCKocha Mkuu1 Januari 201730 Juni 20170.00
2014/2015 – 2015/2016Dibba Al-Hisn SCKocha Mkuu1 Julai 201430 Juni 20160.00
2012/2013 – 2013/2014AA AparecidenseKocha Msaidizi1 Januari 201330 Septemba 20130.00
2011/2012Hatta ClubKocha Mkuu1 Julai 201130 Juni 20120.00
2010/2011SC FarenseKocha Msaidizi1 Oktoba 201030 Juni 20110.00
2009/2010 – 2010/2011SC Farense U19Kocha Mkuu1 Julai 200930 Septemba 20100.00
2007/2008 – 2008/2009SC Farense Youth 17Kocha Mkuu1 Julai 200730 Juni 20090.00

Hitimisho

TAARIFA YA YANGA SC KWA UMMA
Taarifa ya Yanga SC kwa Umma

Huku kitendawili cha ni nani kuchukua kijiti cha Kocha mpya Yanga SC kikizidi kushika hatamu, uongozi wa timu hiyo umetangaza kuwa kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya makocha Makocha, Abdihamid Moalin na Patrick Mabedi. Makocha hao watafanya kazi kama ‘Co-Headcoaches’ yaani wote wawili watakuwa makocha wakuu wa timu yetu. Kocha msaidizi atasalia, Matthew Silva ambaye alikuwa kocha msaidizi wa Pedro.

SOMA HII PIA: Roman Folz kufukuzwa Yanga SC, kocha mpya huyu hapa

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.