- Yanga SC vs Simba SC Kariakoo Dabi yanukia Zanzibar Januari 2026
- Simba SC vs Azam FC 2026 NMB Mapinduzi Cup ni Mzizima Dabi visiwani
- Steve Barker kocha mpya Simba SC kwenye mtihani mgumu kufuta Simba SC 0-2 Azam FC mchezo wa NBC League.
Simba SC vs Azam FC ni mchezo unaofuata NMB Mapinduzi Cup. Hii ni hatua ya nusu fainali ya kwanza Uwanja wa New Amaan Complex saa 2:15 usiku. Mshindi wa mchezo atakutana na mshindi wa nusu fainali ya pili Yanga SC vs Singida Black Stars. Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker katika kibarua kufuta Simba SC 0-2 Azam FC mchezo uliopita wa NBC League.
SOMA HII: Simba SC 0-2 Azam FC ni matokeo yaliyovunja rekodi/ Ratiba ya mechi zijazo CAF Champions League
Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini, muda ni wako na nafasi ya ushindi inakusubiri.

Simba SC vs Azam FC matokeo yao NMB Mapinduzi Cup 2026

Simba SC vs Azam FC mpaka zinakutana zilianzia hatua ya makundi. Azam FC ilicheza mechi tatu huku Simba SC ikicheza mechi mbili. Ushindi kwa Simba SC ni mechi zote mbili huku Azam FC ikishinda mbili na kulazimisha sare mchezo mmoja. Kariakoo Dabi inanukia ikiwa Simba SC atapata ushindi na Yanga SC atashinda nusu fainali ya pili.
Utabiri wa matokeo Simba SC vs Azam FC
Kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza ni matajiri Azam FC wanapewa nafasi kubwa yakushinda. Hii inatokana na aina ya wachezaji walionao, spidi na ubora kwenye kutumia nafasi. Simba SC licha yakupewa nafasi ndogo sio timu ya kuibeza.
Matokeo ya Simba SC NMB Mapinduzi Cup
Januari 3,2026
Simba SC 1-0 Muembe Makumbi City
Mfungaji:-Bajaber
Januari 5,2026
Fufuni FC 1-2 Simba SC
Wafungaji:-Hassan Mbegu na Nabby Camara
SOMA HII: Matokeo ya Simba SC 2025/26 | Ratiba, vinara wa ufungaji

Kikosi cha Simba SC kinachotarajiwa kuanza
Mlinda mlango
Hussen Abel
Mabeki
Duchu
Mligo
Chamou
De Reuck
Viungo
Kante
Chasambi
Naby Camara
Ellie Mpanzu
Neo Maema
Bajaber
Matokeo ya Azam FC NMB Mapinduzi Cup

Desemba 31,2025
Azam FC 1-1 Singida Black Stars
Mfungaji:-Kitambala Jephte
Januari 2,2026
Azam FC 2-0 Mlandege
Wafungaji:-Zidane na Himid Mao
Januari 5,2026
Azam FC 2-1 URA Uganda
Wafungaji:-Kitambala Jephte na Alobogast
Kikosi cha Azam FC kinachotarajiwa kuanza
Langoni
Air Manula
Chilambo
Zouzou
Lawi
Twalib
Himid
Zidane
Kibeku
Kitambala
Akaminko
Diakite
Wachezaji wakuchungwa kwa Simba SC
Nabby Camara
Nyota huyu alishikilia ufunguo wa ushindi mchezo dhidi ya Fufuni kwa goli la jioni. Ni imara katika kuzuia na kushambulia. Uwezo wake kwenye mguu wa kulia umekuwa na hatari kwa wapinzani.
Ellie Mpanzu

Licha ya kiwango chake kutokuwa kwenye ubora ni mchezaji tegemeo. Kurejea kwake kikosi cha kwanza kunaongeza nguvu kwa Simba SC na hatari kwa wapinzani. Ni mchezaji mwenye spidi na maamuzi ya haraka kwenye kushambulia.
De Reuck
Beki huyu alikuwa nje kwa muda kutokana na kutokuwa fiti. Amerejea uwanjani hivyo hatari yake akiachwa huwa ni kubwa. Uwezo kwenye matumizi ya mipira ya adhabu katika kufunga upo kwenye miguu yake.
Wachezaji wakuchungwa kwa Azam FC
Zidane
Ni kiungo mwenye hatari akiwa uwanjani. Kwenye mechi kubwa amekuwa na matokeo mazuri kutokana na kujihatarisha mara nyingi. Simba SC wanamkumbuka kwenye mchezo wa ligi 2024/25 aliwafunga goli dakika ya 88.
Kitambala
Kwenye Mapinduzi Cup amefunga magoli mawili katika mechi tatu.Ni mchezaji ambaye anapenda kufunga akiwa uwanjani. Uwezo wake katika maamuzi ya haraka ni kitu cha kutazamwa na wapinzani Simba SC.
Alobogast
Mshambuluaji ambaye amekwenda hewani matumizi ya nguvu na akili. Ni mchezaji anayepaswa kutazamwa kwa ukaribu kutokana na uwezo wake katika kufunga.
SOMA HII: Simba SC ina mgogoro mzito kwa sasa? Ukweli huu hapa/ Mo na Mangungu sakata lipo hivi

Maneno ya makocha wa Simba SC vs Azam FC
Steve Barker, Kocha Mkuu wa Simba SC amesema wanatambua utakuwa mchezo mgumu. Maandalizi yamefanyika ili kupata matokeo mazuri.
“Tutakuwa na mchezo mgumu lakini tumefanya maandalizi mazuri.Kikubwa ambacho tunahitaji ni matokeo mazuri,”.
Florent Ibenge, Kocha Mkuu wa Azam FC amesema kutakuwa na mabadiliko kwenye kikosi na watacheza kama siku zote. Malengo makubwa ni kupata ushindi.
“Tumefanya maandalizi mazuri na tupotayari kwa mchezo. Kutakuwa na mabadiliko kwenye kikosi ila malengo ni kupata matokeo mazuri,”.
Hitimisho
Simba SC vs Azam FC mchezo wa nusu fainali NMB Mapinduzi Cup itaamua nani kwenda hatua ya fainali. Mshindi wa mchezo Januari 9 atakuwa jukwaani kuwatazama Yanga SC vs Singida Black Stars nusu fainali ya pili. Je inawezekana Kariakoo Dabi ya Yanga SC vs Simba SC kuanza visiwani? Matokeo yataamua.

