- Alama za hivi punde za mpira wa miguu kati ya Singida Black Stars vs Azam FC kwenye Ligi Kuu
- Singida Black Stars waonja joto ya jiwe mbele ya Azam FC Aprili Mosi, 2026, Uwanja wa Airtel
- Usajili wa Feisal Salum unalipa afunga goli la ushindi kwa pasi ya Idd Nado
- Ayoub Lyanga amewafunga waajiri wake wa zamani goli moja dakika ya 70, (Singida Black Stars 1-2 Azam FC)
Singida Black Stars waonja joto ya jiwe mbele ya Azam FC. Ni kwenye mchezo wa NBC Premier League Aprili Mosi 2026, Uwanja wa Airtel. Singida Black Stars 1-2 Azam FC matokeo rasmi kwenye mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa.
SOMA HII: Mtibwa Sugar 1-3 Singida Black Stars, KMC FC yapigwa na Azam FC/ Namungo FC vs Yanga SC lineups
Je, bado hujashinda mamilioni? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune pesa sasa
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Singida Black Stars waonja joto ya jiwe mbele ya Azam FC

Licha ya kuwa wapo nyumbani Singida Black Stars waonja joto ya jiwe mbele ya Azam FC. Kichapo cha magoli mawili kimewalaza na viatu wakipishana na pointi 3 muhimu. Magoli kwenye mchezo huyo yote yalifungwa kipindi cha pili.
Usajili wa Feisal Salum unalipa
Usajili wa kiungo Feisal Salum ambaye alijiunga na Azam FC akitokea Yanga SC unalipa kutokana na kazi anayofanya. Goli alilofunga kiungo huyo lilikuwa ni muhimu kwa kuipa timu yake pointi tatu. Hilo linakuwa ni goli la 7 kwa kiungo huyo aliyekuwa akitajwa kupigiwa hesabu na Simba SC kwenye tetesi.
Ikumbukwe kwamba dakika 45 za mwanzo ilikuwa Singida Black Stars 0-0 Azam FC. Kipindi cha pili hali ilibadilika, dakika ya 50 kupitia kwa Lusajo Mwaikenda na dakika ya 63 Feisal Salum alifunga goli la pili. Ni Ayoub Lyanga alifunga goli pekee kwa Singida Black Stars dakika ya 70.
Kiungo wa Azam FC, Idd Nado alichaguliwa kuwa mchezaji bora. Hiyo ilitokana na kazi aliyofanya kuhusika kwenye magoli yote mawili. Alitoa pasi ya goli kwa Lusajo na Feisal katika mchezo huo.
Takwimu za mchezo wa Singida Black Stars vs Azam FC

| Singida Black Stars | Azam FC | |
| 9 | Mashuti | 13 |
| 5 | Lenga lango | 8 |
| 50% | Umiliki | 50% |
| 4 | Mashuti yasiyolenga lango | 5 |
| 0 | Kadi nyekundu | 0 |
| 1 | Kadi ya njano | 4 |
| 3 | Kona | 2 |
| 1 | Magoli | 2 |
H2H Singida Black Stars vs Azam FC
01/04/2026, Singida Black Stars 1-2 Azam FC 03/12/2025, Azam FC 0-0 Singida Black Stars
06/04/2025, Singida Black Stars 1-0 Azam FC
28/11/2024, Azam FC 2-1 Singida Black Stars
21/04/2024, Azam FC 1-0 Singida Black Stars
04/11/2023, Singida Black Stars 1-3 Azam FC
13/03/2023, Singida Black Stars 1-0 Azam FC
31/10/2022, Azam FC 1-0 Singida Black Stars
11/03/2021, Azam FC 3-0 Singida Black Stars
20/10/2020, Singida Black Stars 0-2 Azam FC
Mechi zijazo NBC Premier League 2025/26
| Tarehe | Timu mwenyeji | Timu mgeni | Uwanja na muda | |
| Aprili 3,2026 | Dodoma Jiji FC | vs | Fountain Gate | Airtel, Singida saa 08:00 mchana |
| Aprili 3,2026 | Mbeya City | vs | KMC | Tanzanite Kwaraa, Manyara, saa 10:15 jioni |
| Aprili 4, 2026 | Mashujaa FC | vs | Pamba Jiji | Lake Tanganyika, saa 10:00 jioni |
| Aprili 4, 2026 | Yanga SC | vs | Tanzania Prisons | KMC Complex, saa 12:30 jioni |
| Aprili 4, 2026 | Namungo FC | vs | JKT Tanzania | Majaliwa, saa 9:00 usiku |
| Aprili 5, 2026 | TRA United | vs | Singida B.S | Sheikh Amri Abeid, saa 10:00 jioni |
| Aprili 5, 2026 | Azam FC | vs | Simba SC | Azam Complex, saa 1:00, usiku |
| Aprili 6, 2026 | Coastal Union | vs | Mtibwa Sugar | Mkwakwani,Saa 1:00 usiku |
SOMA HII: Mashujaa FC yaibana Azam FC NBC Premier League/ Highlights, statics, standings

Msimamo wa NBC Premier League 2025/26

| POS | MP | W | D | L | PTS |
| Yanga SC | 16 | 11 | 5 | 0 | 38 |
| Azam FC | 16 | 8 | 8 | 0 | 32 |
| Simba SC | 14 | 9 | 4 | 1 | 31 |
| 4. JKT Tanzania | 17 | 7 | 7 | 3 | 28 |
| 5.Pamba Jiji FC | 16 | 6 | 7 | 3 | 25 |
| 6.Singida Black Stars | 16 | 7 | 4 | 5 | 25 |
| 7.Mtibwa Sugar | 17 | 5 | 7 | 5 | 22 |
| 8.Namungo FC | 17 | 5 | 6 | 6 | 21 |
| 9.Dodoma Jiji FC | 17 | 5 | 6 | 6 | 21 |
| 10.TRA United SC | 16 | 5 | 5 | 6 | 20 |
| 11.Mashujaa FC | 17 | 4 | 7 | 6 | 19 |
| 12.Fountain Gate FC | 16 | 4 | 4 | 8 | 16 |
| 13.Coastal Union | 16 | 3 | 6 | 7 | 15 |
| 14.Mbeya City | 16 | 3 | 4 | 9 | 13 |
| 15.Tanzania Prisons | 17 | 3 | 4 | 10 | 13 |
| 16. KMC FC | 16 | 2 | 2 | 12 | 8 |
UFUNGUO
POS- Nafasi
MP- Mechi zilizochezwa
W- Ushindi
D- Sare
L- Poteza
PTS- Pointi
SOMA HII: Azam FC 0-0 Yanga SC Dar Derby/ Highlights, standings, statics

Hitimisho
Singida Black Stars waonja joto ya jiwe mbele ya Azam FC baada ya kupoteza pointi 3. Ushindi huo unawapandisha matajiri wa Dar mpaka nafasi ya pili wakiishusha Simba SC. Wenyeji wanabaki nafasi ya sita wakipoteza mechi 5.

