skip to Main Content
Historia Ya Arsenal
C3J9TD Arsenal football club Emirates Stadium

Historia ya Arsenal

Historia ya Arsenal.

Mji wa London unafahamika kama makao makuu ya mpira wa mguu. Vile vile, uwanja wa Wembley pamoja na uwanja wa Emirates ambao ni maarufu sana duniani. Pia mji wa London unajivunia kuwa na klabu za soka kati ya 15 na 18 kulingana na pale utakapoweka mipaka yako. Baadhi ya hizi klabu ni maarufu kuliko zingine na kwa sasa kuna klabu sita ambazo zinashiriki ligi kuu ya Uingereza ambazo ni Arsenal, Tottenham, Chelsea, Westham, Crystal Palace na Fulhmam.

Ingawa hakuna njia ya kupima dhahiri kitu kama cha muda mfupi kama umaarufu, watafiti wengi wa mpira wa miguu na wataalam wa takwimu wanakubali kwamba Arsenal ina wafuasi wengi  zaidi kuliko klabu nyingine yoyote kwenye mji wa London. Lakini huyo sio mshangao kabisa kwani klabu ya Arsenal inayo sababu zote sahihi za kuwa klabu kubwa London. Ni klabu ya zamani na yenye historia ndefu na ya kupendeza. Ni klabu ambayo ishawahi kuwa na wachezaji wenye vipaji vikubwa ambavyo vimewahi kushuhudiwa kwenye mpira wa miguu lakini la muhimu, ni klabu yenye tamanduni ya kushinda vikombe!

Arsenal pia ni klabu ambayo wanasaikolojia wa michezo wanapenda kuizungumzia. Wakati timu inapofikia  mwishoni mwa milenia na mafanikio, ilionyesha jinsi nguvu ya mafanikio inavyoweza kufikiwa wakati timu, wachezaji na meneja wako katika maelewano mazuri – na mnamo 2018, timu ya Arsenal FC ilivyo weza kutetereka kwa karaka na kufika mwisho wa utawala kweneye soka la uingereza. Wacha tuangalie kwa ukaribu namna Arsenal iliwezaye kupoteza ufalme wake tukiangalia wachezaji wake wa zamani na wa sasa.

Miaka ya kukua.

Arsenal FC imekuwa karibu kwa muda mrefu kuliko wapinzani wake wengi wa Ligi Kuu – hata hivyo huenda usingeitambua timu hiyo kama Arsenal katika miaka yake ya mwanzo. Klabu hiyo iliundwa mapema mnamo 1886, kipindi hicho hakuna hata Ligi ya kulipwa nchini Uiengereza.

Kabla ya hapo, Royal Arsenal, ambao ni silaha ambazo zilitengenezwa kwa Vikosi vya Wanajeshi wa Uiengereza, ilikuwa katika mji wa Woolwich. Wakati huo, Woolwich ilikuwa ni kitongoji peke yake kusini mwa mji mkuu, lakini siku hizi, ni moja katika mji wa London. Kikundi cha wafanyikazi takriban 15 wa Arsenal waliamua kuunda klabu ya mpira wa miguu na wakaamua kuita jina la  “Dial Square” baada ya eneo kuu katikati mwa uwanja wa Royal Arsenal.

Katika miezi michache tu baada ya kuanzishwa kwa klabu ya Arsenal, ikawa ni wazi kuwa jina hilo lilikuwa zito na la kutatanisha. Kwa kuongezea, watu walikuwa wakiwataja kama “Arsenal” hata hivyo, mnamo 1887, jina la timu lilibadilishwa rasmi. Miaka minne baadaye, “Woolwich Arsenal,” kama walivyoitwa rasmi wakati huo, alijiunga na Ligi mpya ambayo ilikuwa imeanzishwa hivi punde, na kuwa klabu ya kwanza ya mpira wa miguu kujiunga na ligi ya kulipwa kutoka mji wa London. Mnamo 1904, Arsenal ilijiunga na vilabu vikubwa kwenye ligi daraja la kwanza, lakini katika siku hizo, msimamo kwenye ligi haukuwa mzuri.

MicrosoftTeams-image-Kuhamia London Kaskazini.

Kwenye miaka yake ya kukuza timu, klabu ilikuwa kwenye wakati mgumu wa kifedha, na hii ilitokana na klabu nyingi kuanza kubadilisha uendeshaji wake na kugeukia kwenye soka la kulipwa. Klabu hizo ni pamoja na  Fulham, Chelsea, Millwall, West Ham, Charlton Athletic, na orodha hiyo ilizidi kuendelea. Shida ambayo Arsenal ilikumbana nayo ni kwamba timu hizi hasimu zilikuwa karibu na mashabiki wengi wa mpira wa miguu wa London. Pia, kadiri karne ya 20 ilivyokuwa ikielekea karibu na 1914, wafanya kazi wengi walijikuta wakikosa muda au shauku ya mpira wa miguu.

Kitu cha pili ilikuwa ni kitu cha kawaida kwa timu yoyote ya mpira wa miguu. Hata hivyo, kulikwa na hatua ya kuchukua ili kukuza jina la klabu. Kama mashabiki hawataifuata Arsenal, basi Arsenal atawafuata mashabiki. Mnamo 1913, baada ya kuwa na msimu mbaya uliopelekea kushuka hadi daraja la pili, Arsenal iliamisha makazi yake na kwenda Highbury, Kaskazini mwa London. Kwa hapo yamekuwa makazi yao mpaka sasa.

Uwanja wake halisi ulibakia kama makazi yake kwa miaka mingi, na ilikuwa ikijulikana kwa sifa zake nyingi ambazo zingine zilikuja kurejeshwa baada ya kupigwa mabomu wakati wa vita ya pili ya dunia. Vitu vingi vizuri zilifikia tamati, ingawa mnamo 2006, uwanja wa Highbury ulibomolewa na kujengwa nyumba za makazi ya watu. Ulibadilishwa kwa kujengwa uwanja wa kisasa wa Emirates, ambao hupo mitaa michache kutoka uwanja wa Highbury.

Mtaalamu mpya wa kombe la FA?

Kama umeshawahi kumuuliza mtu miaka 20 iliyopita ni timu ngani ingekuwa ni mtaalamu wa kombe la FA, angekwambia ni mahasimu wa Arsenal ambao ni timu ya Tottenham. Kipi kingine cha Zaidi, angekuwa amepatia. Kwenye michuano la kombe la FA, kwa karne ya 20 timu ya Tottenham ndio ilikuwa inafanya vizuri Zaidi huku ikishinda kombe hilo mara nane kati ya mwaka 1901 na 1991.

Hata hivyo, kwa sasa inamaanisha ni miaka 30 tangu Tottenham kushinda kombe la FA. Hiyo ni Zaidi ya ajabu tu, na jukumu lao kama mabingwa wa michuano ya Kombe la FA imebaki historia tu. Timu ya Chelsea imeshinda kombe la FA mara nne kwa muda wa miaka sita yaani 2007 na 2012 na kufikisha mataji sawa na Tottenham. Hata hivyo, kwa kuangalia michuano ya FA kwa upana zaidi pamoja na historia yake, hakuna timu ishawahi kushiriki, na kushinda mara nyingi kama timu ya Arsenal. Kwa miaka 90 iliyopita, Gunners wamecheza fainali za kombe la FA mara 21 na kati ya hizo wameshinda mara 14. Hiyo ni zaidi ya Tottenham, na ni zaidi ya Chelsea na pia ni nyingi kuliko Manchester United ambayo ni timu inayoonekana kushikilia ushindi wa rekodi nyingi kati ya ligi ya Uingereza.

Arsene Wenger na yasiyowezekana.

Kama ilivyo kwa timu nyingine yoyote ile, Arsenal imekuwa na wakati mzuri na pia wakati mbaya kwenye historia yake. Tulisema hapo awali kwamba kwenye miaka hiyo ya kutengeneza timu kwenye karne ya 20 ilikuwa ni miaka ya changamoto kwa timu ya Arsenal. Kitu ambacho walikuwa hawajui kwa kipindi hicho, lakini miaka 100 baadae, mambo yangekuwa tofauti sana.

Kwenye miaka ya 1990, mawingu ya dhoruba yalikuwa yakijikusanya. Kocha George Graham alikuwa ameongoza timu hiyo kushinda mataji mawili ya ligi – kombe ya FA na mara mbili kombe la ligi pamoja na kombe la Europa kwenye miaka yake saba ya kuiongoza timu ya Arsenal. Lakini tabia binafsi ya Graham iliingia dosari kufuatia kushutumiwa kwake kwa kuchukua hongo kwenye usajili wa wachezaji. Hatimaye alifukuzwa kazi mnamo 1995 na nafasi yake ikachukuliwa na Bruce Rioch kwa kipindi kifupi kisichozidi mwaka mmoja. Kwa hakika, wakati kocha Arsene Wenger akichukua timu, alikuwa na kazi kubwa ya kurundisha imani pamoja na hali ya mpya kwenye timu baada ya changamoto zote hizo.

Wenger aliamua kutupa kila kitu chini na kuanza upya kutoka chini na kuja na staili mpya. Alikuja na kila kitu kipya, mpira wa kushambulia, alidhibiti mazoezi ya mwili na lishe na alichukua jukumu la kuhahakisha fedha zinatumika kwa ufanisi na kwa uwazi. Kwa leo, hakuna kitu kama hicho ungesikia kutoka kwa kocha yoyote mzuri ambacho angefanya, lakini ni vizuri kusema kuwa kwa robo ya karne, Wenger alianzisha enzi mpya ndani ya timu ya Arsenal.

Wenger pia alisajili wachezaji muhimu, wakiwemo Wafaransa wenzake Thierry Henry na Patrick Viera. Matokeo yake? Ule ushindi wa kipindi cha George Graham ulianza kurudi kwa kasi ya aina yake. Arsenal ikashinda tena kombe la ligi na kombe mara mbili mwaka 1998 na 2002. Fainali mara tatu kwenye michuano ya UEFA na kushinda matawi mawili. Na hapo kwenye ligi kuu ya Uingereza mwaka 2003/04 ambayo iliweka historia, Arsenal mbali na kushinda Ligi Kuu ya Uingereza, ilishinda bila kupoteza mchezo wowote. Ilikuwa hajawahi kutokea nah ii ilimaanisha Arsenal ilicheza michezo 49 bila kupoteza.

Hii iliwapa jina la utani la ‘Isiyowezekana’ na kama iliwaingia vichwani mwao wakati wakizungumza na waandishi wa habari, basi haikuingiliana na kiwango chao cha kucheza uwanjani. Arsenal iliweza kumaliza ligi ikiwa nafasi ya kwanza au ya pili kwenye miaka nane kati ya tisa ya Wenger akiwa kocha, isipokuwa jambo ambalo halikuwa nzuri, hawakuweza kutetea taji lao mwaka baada yam waka. Mnamo 2006, mwaka ambao Arsenal ilihamia kwenye uwanja wa Emirates, Arsenal ilishinda kombe la michuano ya UEFA kwenye mafanikio yao, na kuwa timu ya kwanza kwenye historia ya miaka 50 kushinda taji hilo kutoka kwenye mji wa London.

Wenger aliendelea kuwa kocha wa Arsenal kwa miaka mingine 12, na isipokuwa timu iliendelea kushinda mataji – ikiwemo kushinda mara mbili michuano ya FA, siku ngumu za yasiyowezekana zilikuwa nyuma yao na kwenye matokeo ya uwanjani, kwa ujumla yalianza kwenda chini. Aprili 2018, Arsene Wenger alitangaza kujiuzulu nafasi ya ukocha ndani ya Arsenal na kwenye siku yake ya mwisho kama kocha wa Arsenal, mashabiki walimkaribisha huku wakiwa wamesimama kwa shangwe huku timu yake ikimuaga kwa mshindi mnono wa 5-0 dhidi ya Burnley. Hii iliweka alama ya mwisho wa kipindi cha mafanikio kwenye historia ya timu ya Arsenal. 

MicrosoftTeams-image-

Wachezaji wenye historia.

Hatua ya Arsene Wenger kuifanya timu ya Arsenal kuwa moja ya timu zenye historia kubwa kwenye mpira wa miguu haliwezi kuacha hivi hivi. Hata hivyo, hazingeweza kufikia mafanikio hayo bila ya kuwa na vipaji bora kabisa kwenye mpria wa miguu kwa kipindi chote chake. Timu ya Arsenal ilifurahi huduma za wachezaji bora wa kandanda, nah ii imekuwa hivyo kabla na baada ya miaka 22 ya Wenger. Hapa tunaona baadhi ya wachezaji hao.

 

  • Alex James – Tutaanza na moja ya wana historia. James alikuwa ni kiungo mwenye ujuzi wa hali ya juu na mchezaji mwenye akili kubwa ya mpira wa miguu. Aliichezea timu ya Arsenal michezo 230 kati ya 1929 na 1937, na alikuwa ni moja ya wachezaji walikuwepo wakati Arsenal ikishinda taji lake la kwanza la michuano ya FA. James pia alikuwepo wakati Arsenal ikishinda mataji mengine matano ya FA na ligi mnamo 1931. Mafanikio ya James ni ya kipekee alipata ugonjwa hatari wa athma wakati wa muda wake wa kucheza soka.
  • Tony Adams – Beki matata ambaye alitumia muda wake wote wa kucheza kwa kuitumikia timu ya Arsenal, huku akicheza michezo zaidi ya 500 kwa kipindi cha miaka 22. Akiwa kwenye timu kwa kipindi kigumu cha miaka ya 80 na 90, huku akichapikwa jina la Bwana Arsenal, aliipenda timu yake kweli kweli, nah ii inatokea mpaka leo pale mashabiki wa Arsenal wanapoimba jina ikiwa ni zaidi ya miaka 20 tangu astaafu. Nje ya uwanja, Adams alikuwa ameathirika na ulevi, na leo anatumia muda wake kwenye kutoa nasaha pamoja na kusaidia makundi mbali mbali kwa kutumia ujuzi wake kuwasaidia wengine.
  • David Seaman – Ni ukweli mchungu kwamba walinda mlango wengi hawapati kile wanachotakiwa kupata, kusimama katika milingoti miwili kwa dakika nyingi na hatimaye kuhamashisha mchezo wote kwa kutumia mikono ya maajabu. Gunners wamebarikiwa kuwa na baadhi ya walinda milango hodari kabisa kama vile Bob Wilson, Jens Lehmann na Peter Cech. Lakini mikono salama ya Seaman ambaye alifanya kazi ya zaidi na ziada, kwa kuokoa mipira ambayo ilionekana kuwa migumu. Aliichezea Arsenal michezo 563 huku akichezea timu yake ya taifa ya Uingereza michezo 75.
  • Ian Wright – Wright alitangaza kujiunga Highbury mnamo 1991 huku akiwa na deni la goli moja, na akajipata kifunga mara tatu zaidi kwenye mechi yake ya pili tu. Kwenye miaka saba iliyofuata, maajabu yake hayakuisha na Wright alikuwa kinara wa magoli kwa timu yake na hasa pale ilipomuhitaji zaidi. Mataji yalishindwa akiwepo na ilikuwa si ajabu kushinda mataji matatu kwenye msimu wake wa mwisho na timu yake ya Arsenal.
  • Dennis Bergkamp – Sio mwanasoka bora sana kulingana na aina ya vipaji, lakini kiungo huyo ya Kiholanzi alikuwa na uwezo wa kucheza kama mshambuliaji au kushuka chini na kusaidia mabeki. Alikuwa anauza tiketi za uwanjani na vile vile angekutengenezea kahawa kama ungehitaji pia. Thierry Henry alimuelezea kama ndoto huku Pele akisema ni mchezaji bora kwa upande wake – hatuhitaji kuzungumzia zaidi.
  • Thierry Henry – Moja ya kiunganishi cha Wenger cha yasiyowezekana, Henry sio tu moja ya wachezaji bora kwa kikosi cha Arsenal, lakini ni moja ya wachezaji bora katika historia ya ligi kuu ya Uingereza. Akiwa na magoli 228, amekuwa na magoli 53 zaidi ya mfugaji wa pili bora katika historia ya klabu ya Arsenal.

Hawa ni baadhi ya wachezaji wachache ambao wametengeza historia ya klabu ya Arsenal. Hatujui kitatokea nini kwa baadae, lakini historia ni kama imetufunza kitu, tunajua haitaenda kuwa mbaya!

 

 

 

 

Share this:
Back To Top