- Ni Clatous Chama ni mchezaji wa kwanza kushinda tuzo 5 mfululizo NBC Premier League 2025/26
- Coastal Union 1-2 Simba SC alitoa pasi mbili za magoli na kuchaguliwa kuwa Man of the Match akifikisha tuzo yake ya 5
- Goli lake alilowafunga Yanga SC lamfikia mchezaji wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand
Kiungo wa Simba SC Clatous Chama ni mchezaji wa kwanza kushinda tuzo 5 mfululizo za Man of the Match.Mwamba wa Lusaka mwenye miaka 34 usajili mpya dirisha dogo amekuwa katika ubora wake. Hii ni rekodi mpya katika historia ya soka la Tanzania ndani ya Ligi Kuu Bara ya NBC. Goli alilofunga dhidi ya Yanga SC limetabiriwa kutwaa tuzo ya goli bora na mchezaji wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand. Mchezo uliopita ubao wa Uwanja wa Mkwakwani ulisoma Coastal Union 1-2 Simba SC, alitwaa tuzo yake ya 5 mfululizo.
Je, unataka kushinda mamilioni? Unaweza kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 na SportPesa
Wengi tayari wamevuna mamilioni kupitia mchezo wa Kindege yaani ‘Aviator’ ya SportPesa. Wewe unasubiri nini? Nafasi ni yako cheza Aviator na kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 sasa kwa kubonyeza picha hii chini.
SOMA HII: Usajili mpya Simba SC balaa: Clatous Chama, Sopu, Mpanzu watikisa tena

Mwamba Clatous Chama ni mchezaji wa kwanza kushinda tuzo 5 NBC Premier League 2025/26

SOMA HII: Clatous Chama usajili wake umelipa | Takwimu na timu alizocheza CAF Champions League

Historia imeandikwa kiungo wa Simba SC, Clatous Chama ni mchezaji wa kwanza kushinda tuzo 5 NBC Premier League mfululizo bila kupumzika. Katika mechi 5 za ligi mara baada ya dakika 90 kiungo huyo alitwaa tuzo hiyo baada ya kuchaguliwa na jopo la kamati. Hii ni tuzo maalumu ambayo hutolewa kwenye kila mechi kwa lengo la kuongeza wachezaji kujituma uwanjani.
Kwenye mechi za Mei 2025/26 Chama amekuwa katika ubora kila mchezo. Alianza Mei 3, 2026 dhidi ya Yanga SC alipofung goli bora na kutoa pasi Uwanja wa Meja Jeneral Isahmuyo. Katika mchezo huo ubao ulisoma Simba SC 2-2 Yanga SC, wawili hawa waligawana pointi mojamoja.
Orodha ya mechi ambazo alichukua tuzo Chama
| Tarehe | Mechi | Uwanja | Magoli | Assist |
|---|---|---|---|---|
| 3 Mei 2026 | Simba SC 2-2 Yanga SC | Meja Jeneral Isahmuyo | 1 | 1 |
| 6 Mei 2026 | Simba SC 1-0 JKT Tanzania | Meja Jeneral Isahmuyo | 1 | 0 |
| 10 Mei 2026 | Simba SC 4-0 Tanzania Prisons | KMC Complex | 1 | 0 |
| 14 Mei 2026 | Mashujaa FC 0-3 Simba SC | Lake Tanganyika | 2 | 0 |
| 21 Mei 2026 | Coastal Union 1-2 Simba SC | Mkwakwani | 0 | 2 |
Ahmed Ally maoni yake kuhusu Clatous Chama

SOMA HII: Clatous Chama aongeza presha Yanga SC | Takwimu, mechi | SportPesa Blog
Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC amesema kuwa Chama ni mchezaji anayeendeleza ubora kila wakati. Kwenye mechi tano mchezaji huyoametwaa tuzo jambo ambalo sio jepesi. Aliongeza kuwa anawachanganya kila siku.
“Clatous Chota Chama ni mchezaji anayeonyesha ukubwa na ubora kwenye mechi zote. Unaona katika mechi tano mfululizo amekuwa bora. Sio jambo jepesi mchezaji kutwaa tuzo mechi 5 mfululizo huu ni ubora na mwendelezo kwa kila mechi,”.
Rio Ferdinand maoni yake kuhusu goli la Chama
Mchezaji wa zamani wa Manchester United, Rio Gavin Ferdinand mwenye miaka 47 amelitaja goli la Chama kuwa na hadhi ya kutwaa tuzo ya goli bora. Beki huyo alikuwa Tanzania kwa wito maalumu na Wizara ya Habari na Michezo. Kwenye mahojiano na mtangazaji wa Clouds Media, Meena Ally alitaja goli hilo kuwa bora.
“Ninaona hili ni goli bora kwenye ligi kutokana na namna mfungaji alivyofunga. Kwa maoni yangu linastahili kuwa goli bora la msimu. Limefungwa kwa ustadi na linafurahisha,” alisema Rio.
Msikie Chama Clatous mwenyewe
Kiungo Chama ambaye amefunga magoli 8 kwenye ligi amesema bado kuna kazi kubwa itaendelea kufanyika kwa mechi zijazo. Chama amesema tuzo hizo ni kwa ajili ya mashabiki. Aliongeza kwa kuwaomba kushirikiana kila wakati.
“Kikubwa ni ushirikiano kutoka kwa wachezaji kwenye kila mchezo. Maelekezo kutoka benchi la ufundi na kupenda kuona timu inapata matokeo.Kupewa tuzo sio kitu chepesi kwani kuna wachezaji wengi nao wanafanya vizuri, mashabiki ninawaomba waendelee kuwa nasi kwenye kila mchezo,”.
Hitimisho
Clatous Chama ni mchezaji wa kwanza kushinda tuzo 5 NBC Premier League 2025/26. Je rekodi hiyo itavunjwa na mchezaji gani msimu huu? Endelea kufuatilia Blog ya SportPesa kwa taarifa za hivi punde.

