Msimamo NBC Premier League ------ kabla ya mechi za mzunguko wa --Msimamo NBC Premier League ------ kabla ya mechi za mzunguko wa --
  • Msimamo Ligi Kuu NBC 2025/26 unazidi kuwa mtamu, hii ni kufuatia vita kali ya ubingwa kati ya timu za Yanga SC na Simba SC.
  • Matokeo ya Yanga SC 3-0 Singida Black Stars yamewarudishia wananchi fomu ya ushindi, baada ya kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa Dodoma Jiji FC.
  • Kabla ya mchezo huo wapinzani wao Simba SC walikuwa kileleni mwa msimamo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union.

Yanga SC rasmi wamerejea kileleni mwa Msimamo Ligi Kuu NBC 2025/26, hii ni baada ya kuichapa Singida Black Stars. Dakika 90 zimekamilika Uwanja wa KMC huku ubao wa matokeo ukionyesha Yanga SC 3-0 Singida Black Stars. Kabla ya mchezo huo wapinzani wao Simba SC walikuwa kileleni mwa msimamo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union.

Fuatilia mwenendo wote wa mashindano ya Ligi Kuu ya NBC 2025/26; Ratiba, matokeo, mechi, magoli na habari za papo kwa papo kupitia SportPesa Blog.

Je, unataka kushinda mamilioni? Unaweza kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 na SportPesa

Wengi tayari wamevuna mamilioni kupitia mchezo wa Kindege yaani ‘Aviator’ ya SportPesa. Wewe unasubiri nini? Nafasi ni yako cheza Aviator na kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 sasa kwa kubonyeza picha hii chini.

Sportpesa Aviator Rain Free Bets- Mil

Aviator: Paisha kindege ushinde mpaka zaidi ya 800,000,000.

Huu hapa msimamo Ligi Kuu NBC

Msimamo NBC Premier League ------ kabla ya mechi za mzunguko wa --
Msimamo NBC Premier League 2025/26 kabla ya mechi za mzunguko wa 24

Yanga wanaendelea kusalia kileleni na pointi zao 57 walizokusanya kwenye mechi 24, kati ya mechi hizo Yanga SC wameshinda mechi 17, sare 6 na kupoteza mara 1. Watani zao Simba wanasalia nafasi ya pili na pointi zao 55 walizokusanya kwenye mechi 24. Azam FC wanakamatia nafasi ya 3 na pointi zao 46.

SOMA HII PIA: NBC Premier League table 2025/26

Yanga SC vs Singida Black Stars h-2-h

Yanga SC vs Singida Black Stars
Yanga SC vs Singida Black Stars

Mchezo huu ni wa 10 kwa timu hizi kukutana katika michuano mbalimbali, kwenye miaka ya karibuni. Yanga SC wameshinda mechi 8, Singida Black Stars wao wameshinda mechi 2 tu. Hakuna matokeo ya sare katika michezo hiyo 10 iliyopita. Hii inafanya mchezo wa Ijumaa kuwa muhimu sana. Jedwali lifuatalo linaelezea takwimu hizi kwa ufupi.

TareheMashindanoMechiMatokeo
22/05/2026Ligi Kuu NBCYoung Africans S.C. vs Singida Black Stars F.C.3-0
05/03/2026Ligi Kuu NBCSingida Black Stars F.C. vs Young Africans S.C.0-3
29/06/2025Fainali ya Kombe la CRDB FederationYoung Africans S.C. vs Singida Black Stars F.C.2-0
17/02/2025Ligi Kuu NBCYoung Africans S.C. vs Singida Black Stars F.C.2-1
30/10/2024Ligi Kuu NBCSingida Black Stars F.C. vs Young Africans S.C.0-1
11/03/2024Ligi Kuu NBCYoung Africans S.C. vs Singida Black Stars F.C.5-0
04/10/2023Ligi Kuu NBCSingida Black Stars F.C. vs Young Africans S.C.2-1
16/01/2023Ligi Kuu NBCYoung Africans S.C. vs Singida Black Stars F.C.1-0
29/11/2022Ligi Kuu NBCSingida Black Stars F.C. vs Young Africans S.C.2-1

SOMA HII ZAIDI: Umeona msimamo wa Ligi Kuu NBC: Takwimu za Yanga SC, Simba SC, JKT zashtua!

Hitimisho

Msimamo Ligi Kuu NBC 2025/26
Matokeo Yanga SC vs Singida Black Stars

Ushindi walioupata Yanga SC vs Singida Black Stars umewarudisha Yanga SC kileleni mwa msimamo Ligi Kuu NBC 2025/26. Ushindi huu unazidi kuchochea moto wa vita ya ubingwa msimu huu. Ikumbukwe Yanga SC wana presha kubwa kufuatia kasi ya watani zao Simba SC walio kwenye nafasi ya pili.

SOMA HII PIA: Ligi Kuu Bara 2025/26 ratiba ya mechi kali| Matokeo, msimamo | SportPesa Blog

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.