KMC FC 0-1 Yanga SC NBC PremierA- Okello
  • KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier League 2025/26, Uwanja wa KMC Complex
  • Allan Okello raia wa Uganda afunga goli la ushindi na kuwa Man of the Match
  • Pedro Goncalves fukuto la kufutwa kazi linaendelea kumuandama

KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier League matokeo rasmi mchezo wa leo Mei 6. 2026, Uwanja wa KMC Complex. Goli la ushindi limefungwa na Allen Okello dakika ya 65. Wananchi wameendeleza ubabe mbele ya wakusanya mapato baada ya mzunguko wa kwanza kupata ushindi wa magoli 4-1.

SOMA HII:Yanga SC: Historia, Usajili wote, kikosi, Ratiba, Matokeo na Takwimu

Je, bado hujashinda mamilioni ya aviator ‘Kindege’ cha SportPesa? Cheza ushinde mamilioni sasa

Changamka! sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Aviator game promotional banner featuring a red propeller plane and a jackpot of 800,000,000.

KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier League

KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier
Okello tuzo NBC Premier League.

Mwisho wa dakika 90 KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier League. Dakika 45 za mwanzo wababe hawa wawili hakuna aliyepata goli ilikuwa 0-0. Ushindi huu unaiongezea ufalme Yanga SC nafasi ya kwanza ikifikisha pointi 51.

Okello amechaguliwa kuwa Man of the Match mara baada ya mchezo. Kiungo huyo raia wa Uganda amekuwa kwenye kiwango bora katika mechi za hivi karibu. Leo alianza kikosi cha kwanza na alitumia dakika 90 nafasi yake ilichukuliwa na Sure Boy.

Matokeo haya yanazidi kuididimiza KMC FC katika msimamo ikiwa mkiani. Pointi zake 9 baada ya mechi 21 imepata ushindi kwenye mechi mbili pekee. Huu unakuwa mchezo wa 16 kupoteza ndani ya NBC Premier League.

SOMA HII: Kariakoo Dabi-Goli la Clatous Chama gumzo kubwa | Ahmed Ally atamba | SportPesa Blog

Aviator game promotional banner featuring a red propeller plane and a jackpot of 800,000,000.

Pedro Goncalves akalia kuti kavu

Mara baada ya mchezo mashabiki walikuwa wakimzomea Kocha Mkuu, Pedro Goncalves. Hii inatokana na kile walichodai kutofurahishwa na matokeo ya timu hiyo. Licha ya ushindi bado walikuwa wakimtaka awaachie timu yao wakimfuata rais wa Yanga SC, Injinia Hersi Said.

TakwimuKMC FCYanga SC
Umiliki wa mpira (%)4357
Magoli01
Kona16
Kadi za njano11
Kadi nyekundu00
Mashuti yaliyolenga lango36
Mashuti yasiyolenga lango16

Yanga SC kwenye mchezo wa leo wamekuwa na umiliki mkubwa ndani ya dakika 90. Walifanya mashambulizi mengi zaidi na kupata goli 1. KMC FC walicheza kwa kujilinda na kushambulia kwa kushtukiza.

SOMA HII: Wachezaji wanne wa Yanga SC warejea kazini | Taarifa mpya kuhusu Depu, ratiba 2025/26

Hitimisho

KMC FC 0-1 Yanga SC NBC Premier League dakika 90 zimekamilika ushindi ukienda kwa wageni. Pedro Goncalves alianza kwa mbinu ya 4-4-2 na KMC FC walikuwa na mpago kazi wa 4-3-3. Wakusanya mapato wamepoteza nje ndani mbele ya mabingwa watetezi msimu wa 2025/26.

Share this: