- Steve Barker ameshinda taji la kwanza Simba SC kwa kuifunga Yanga SC goli 1-0 hatua ya fainali.
- Goli la ushindi lilifungwa na Seleman Mwalimu kwa mkwaju wa penati iliyosababishwa na Edmund John
- Dabi ya Kariakoo Zanzibar ushindi kwa mnyama, Clatous Chama alichezewa faulo dakika za jioni.
Rekodi imeandikwa Steve Barker ameshinda taji la kwanza Simba SC mbele ya Pedro Goncalves wa Yanga SC. Aprili 29, 2026 ubao wa New Amaan Complex ulisoma Yanga SC 0-1 Simba SC goli likifungwa na Seleman Mwalimu kwa mkwaju wa penati. Muungano Cup 2026 mshindi rasmi ni mnyama ambaye amesharejea nalo Dar akitokea Zanzibar.
Je, wajua? Unaweza kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 na SportPesa
Wengi tayari wamevuna mamilioni kupitia mchezo wa Kindege yaani ‘Aviator’ ya SportPesa. Wewe unasubiri nini? Nafasi ni yako cheza Aviator na kushinda mpaka Shilingi Milioni 800 sasa kwa kubonyeza picha hii chini.

Steve Barker ameshinda taji la kwanza Simba SC mbele ya Pedro Goncalves wa Yanga SC

Steve Barker ameshinda taji la kwanza Simba SC baada ya kupokea mikoba ya Dimitar Pantev. Raia huyu wa Afrika Kusini amekuwa na mwendelezo mzuri kwenye mechi za ushindani. Katika mechi tatu za Muungano Cup 2026 zote timu ilipata ushindi.
Hili linakuwa ni taji la kwanza kwa Simba SC 2025/26. Mara baada ya mashindano kukamilika kocha wa Simba SC alitwaa tuzo ya kocha bora. Hii inatokana na matokeo mazuri ambayo alipata kwenye mechi zote.
Edmund John nyota wa Yanga SC alimchezea faulo Clatous Chama dakika ya 118. Zilikuwa zimesalia dakika 2 mchezo huo kukamilika kwa kuwa dakika 90 ilikuwa 0-0. Mwalimu alimfunga Djigui Diarra kipa namba moja wa Yanga SC.
Mnyama kwenye mechi tatu alifunga jumla ya magoli 4. Kinara wa ufungaji ni Seleman Mwalimu akiwa nayo matatu. Goli moja lilifungwa na Neo Maema hatua ya nusu fainali dakika ya 89.
SOMA HII: Muungano Cup 2026 Man of The Match Simba SC vs Yanga SC | Matokeo, takwimu | SportPesa Blog

Matokeo ya mechi za Steve Barker Muungano Cup 2026

| Tarehe | Hatua ya Mashindano | Mechi | Matokeo |
| Aprili 23, 2026 | Robo fainali | Simba SC vs Mafunzo SC | 1-0 |
| Aprili 26, 2026 | Nusu fainali | Mlandege FC vs Simba SC | 0-3 |
| Aprili 29, 2026 | Fainali | Yanga SC vs Simba SC | 0-1 |
Tuzo kwa Simba SC Muungano Cup 2026
| Tuzo | Mshindi | Timu | Takwimu |
| Mfungaji Bora | Seleman Mwalimu | Simba SC | Magoli 3 |
| Kipa Bora | Hussen Mwalimu | Simba SC | Clean sheet 2 |
| Kocha Bora | Steve Barker | Simba SC | Ushindi mechi 3 |
| Mchezaji Bora Chipukizi | Hussein Mbegu | Simba SC | Ameanza kikosi cha kwanza mechi 2 |
SOMA HII: Muungano Cup 2026 | Gueye, Oura, Mpanzu wa Simba SC kutikisa Zanzibar, ratiba na matokeo
Hitimisho
Steve Barker ameshinda taji la kwanza Simba SC mbele ya Pedro Goncalves wa Yanga SC. Kocha huyu ameongeza ari ya ushindani kwenye kikosi hicho. Je rekodi yake itaendelea kwenye mataji mengine ikiwemo CRDB Federaton Cup na NBC Premier League? Endelea kufuatilia Blog ya SportPesa.

