Orodha ya wafungaji bora NBC Premier League 2025/26
Prince Dube na Fabrince Ngoy wanaongoza chati ya ufungaji magoli
Rekodi ya mfungaji bora mwenye magoli 26 inazidi kuwa ngumu
Orodha ya wafungaji bora NBC Premier League 2025/26 vita inazidi kushika kasi. Hii inatokana na kupanda kushuka kwa wafungaji ndani ya uwanja. Mechi 11 zimebaki msimu kufika mwisho na vinara wana magoli 8.
Cheza na ushinde sasa na ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni muda huu
Hujashinda na kindege cha SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kubashiri SportPesa bonyeza picha hii chini.
Orodha ya wafungaji bora NBC Premier League 2025/26
Depu mshambuliaji wa Yanga SC 2025/26.
Bado vita inaendelea kwenye orodha ya wafungaji bora NBC Premier League 2025/26 wakitafuta tuzo ya mfungaji bora. Msimu wa 2024/25 ni Jean Ahoua wa Simba SC alifunga magoli 16. Msimu huu ni Prince Dube wa Yanga SC na Fabrince Ngoy wa Namungo wanaongoza chati wakiwa na magoli 8.
Baada ya mechi 19 kuchezwa hakuna aliyefunga hat trick ndani ya ligi. Pia rekodi ya Mohamed Hussen maarufu kwa jina la Mmachinga ya 1999 kufunga magoli 26 bado haijavunjwa. Je msimu huu kuna mshambuliaji atatoboa kweli?
Orodha ya wafungaji bora NBC Premier League 2025/26 kazi ni kubwa. Katika orodha ya waliohusika kwenye magoli mengi hakuna mchezaji wa Simba SC. Je mnyama atazinduka mzunguko wa pili kuongeza ushindani?