- Simba SC iliangusha pointi tatu kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza ilipofungwa 2-0 dhidi ya Azam FC
- Azam FC vs Simba SC Aprili 5, Jumapili, Uwanja wa Azam Complex 2026 NBC Premier League
- Msimamo wa hivi karibuni NBC Premier League 2025/26
- Taarifa mpya kuhusu Ellie Mpanzu winga wa Simba SC raia wa Dr Congo
Pata habari za hivi punde Azam FC vs Simba SC, Mzizima Derbi saa 1:00 usiku. Azam FC imecheza mchezo mmoja na Simba SC msimu huu kwenye ligi mzunguko wa kwanza 2025/26. Taarifa za sasa hivi kuelekea mchezo huo utachezwa Uwanja wa Azam Complex. Awali ulitarajiwa kuchezwa Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar.
SOMA HII: NBC Premier League ratiba 2025/26 Aprili | Azam FC vs Simba SC | Yanga SC vs Prisons | Msimamo
Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini, muda ni wako na nafasi ya ushindi inakusubiri.

Azam FC FC vs Simba SC nani kuibuka na ushindi?

Azam FC vs Simba SC ni mechi ngumu kwa timu zote mbili. Hii inatokana na ubora wa wapinzani hawa. Katika mechi 5 zilizopita sare zilikuwa mbili, ushindi kwa Azam FC mechi moja na Simba SC mbili.
Kuelekea mchezo wa mzunguko wa pili Azam FC anapewa nafasi kubwa kushinda. Hii inatokana na rekodi ya mzunguko wa kwanza kumbeba. Licha ya uwezekano kushinda kwa wenyeji bado mnyama anahasira kupoteza mchezo wa mzunguko wa kwanza.
H2H Azam FC vs Simba SC
Tazama jedwali la mechi za hivi karibuni kati ya Azam FC vs Simba SC. Hizi ni mechi walizokutana katika NBC Premier League. Kwenye mechi 5, Azam FC akiwa nyumbani alipoteza mechi 2.
| Tarehe | Mashindano | Timu (H) | Matokeo | Timu, (A) |
| Desemba 7, 2025 | NBC Premier | Simba SC | 0-2 | Azam FC |
| Feb 24, 2025 | NBC Premier | Simba SC | 2-2 | Azam FC |
| Sep 26, 2024 | NBC Premier | Azam FC | 0-2 | Simba SC |
| Mei 9, 2024 | NBC Premier | Azam FC | 0-3 | Simba SC |
| Feb 9, 2024 | NBC Premier | Simba SC | 1-1 | Azam FC |

Msimamo wa NBC Premier League

Tazama jedwali la msimamo wa NBC Premier League ulioboreshwa hivi punde. Azam FC kwenye msimamo ipo nafasi ya 3. Simba SC kwenye msimamo ipo nafasi ya pili.
| POS | MP | W | D | L | PTS |
| 1.Yanga SC | 16 | 11 | 5 | 0 | 38 |
| 2.Simba SC | 15 | 10 | 4 | 1 | 34 |
| 3. Azam FC | 16 | 8 | 8 | 0 | 32 |
| 4. JKT Tanzania | 17 | 7 | 7 | 3 | 28 |
| 5.Pamba Jiji FC | 16 | 6 | 7 | 3 | 25 |
| 6.Singida Black Stars | 16 | 7 | 4 | 5 | 25 |
| 7.Dodoma Jiji FC | 18 | 6 | 6 | 6 | 24 |
| 8.Mtibwa Sugar | 17 | 5 | 7 | 5 | 22 |
| 9.Namungo FC | 17 | 5 | 6 | 6 | 21 |
| 10.TRA United SC | 16 | 5 | 5 | 6 | 20 |
| 11.Mashujaa FC | 17 | 4 | 7 | 6 | 19 |
| 12.Mbeya City | 17 | 4 | 4 | 9 | 16 |
| 13.Fountain Gate | 17 | 4 | 4 | 9 | 16 |
| 14.Coastal Union | 17 | 3 | 6 | 8 | 15 |
| 15.Tanzania Prisons | 17 | 3 | 4 | 10 | 13 |
| 16. KMC FC | 17 | 2 | 2 | 13 | 8 |
SOMA HII: Azam FC yaivuruga Simba SC yaifunga mara mbili mfululizo/ Kariakoo Dabi hakuna tena

Taarifa kuhusu mchezaji wa Simba SC Ellie Mpanzu

Mchezaji wa Simba SC Ellie Mpanzu raia wa DR Congo mwenye miaka 24 kuna uwezokano mkubwa akakosekana kwenye mchezo wa kesho. Mpanzu aliongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kukitumikia kikosi cha mnyama. Alikosekana mchezo ulipita dhidi ya Coastal Union.
Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC amesema mchezaji bado ana mkataba na timu hiyo. Alibainisha kuwa wale wanaosema amegoma hilo sio kweli kwani hakuna madai. Aliongeza kuwa kila kitu kipo sawa.
“Ellie Mpanzu ana mkataba na Simba SC. Huyu ni mchezaji halali kabisa. Hakuna madai kuhusu stahiki zake za mkataba mpya kwa kuwa mkataba wake unaisha mwezi wa 8. Mkataba alioongeza bado hajaanza kuutumia,”.
SOMA HII: Elie Mpanzu Kibisawala ni Simba SC 2025/26/ Rekodi na magoli / Dili lake Yanga SC

Hitimisho
Azam FC FC vs Simba SC wababe wawili wanaowania nafasi ya pili kazini. Mshindi kwenye mchezo huo atajenga ngome kwenye nafasi hiyo. Je Azam FC wataishusha Simba SC hapo?

