- Lameck Lawi nyota wa mchezo Azam FC 1-0 Simba SC, NMB Mapinduzi Cup 2026
- Azam FC yaivuruga Simba SC yaifunga mara mbili mfululizo NBC Premier League matokeo Simba SC 0-2 Azam FC.
- Kariakoo Dabi hakuna tena hatua ya fainali kwa mafahari wawili Yanga SC vs Simba SC
Azam FC yaivuruga Simba SC 2025/26 baada ya kupata matokeo mara mbili mfululizo. Wababe hawa wamekutana mara mbili mashindano tofauti. Simba SC 0-2 Azam FC ilikuwa ligi na Azam FC 1-0 Simba SC, NMB Mapinduzi Cup. Kupoteza kwa Simba SC kunafanya matarajio ya Kariakoo Dabi fainali kukosekana kabisa.
SOMA HII: Simba SC 0-2 Azam FC ni matokeo yaliyovunja rekodi/ Ratiba ya mechi zijazo CAF Champions League
Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini, muda ni wako na nafasi ya ushindi inakusubiri.

Azam FC yaivuruga Simba SC kwa mbinu uwanjani

Azam FC yaivuruga Simba SC kwa mbinu uwanjani katika Mzizima Dabi. Kwenye mechi mbili mfululizo safu ya ushambuliaji ya Simba SC haijafunga goli. Matajiri wa Dar wamemfunga mnyama magoli 3.
Matokeo ya Azam FC vs Simba SC 2025/26
Simba SC 0-2 Azam FC, NBC Premier League
Azam FC 1-0 Simba SC, NMB Mapinduzi Cup
Matokeo ya Simba SC Mapinduzi Cup 2026
Januari 3,2026
Simba SC 1-0 Muembe Makumbi City
Mfungaji: Bajaber
Januari 5,2026
Fufuni FC 1-2 Simba SC
Mfungaji: Hassan Mbegu na Nabby Camara
Januari 8,2026
Azam FC 1-0 Simba SC.
SOMA HII: Simba SC vs Azam FC 2026 NMB Mapinduzi Cup/ Lineups, live score, prediction

Kikosi cha Simba SC nusu fainali dhidi ya Azam FC
Mlinda mlango
Hussen Abel
Mabeki
Duchu
Mligo
Chamou
De Reuck
Viungo
Kante
Jean Ahoua
Naby Camara
Ellie Mpanzu
Neo Maema
Mshambuliaji
Jonathan Sowah

Azam FC matokeo yake Mapinduzi Cup 2026
Desemba 31,2025 Azam FC 1-1 Singida Black Stars
Mfungaji: Kitambala Jephte
Januari 2,2026
Azam FC 2-0 Mlandege
Zidane na Himid Mao
Januari 5,2026
Azam FC 2-1 URA Uganda
Wafungaji: Kitambala Jephte na Alobogast
Januari 8,2026
Azam FC 1-0 Simba SC
Mfungaji: Lameck Lawi.

Kikosi cha Azam FC vs Simba SC
Langoni
Air Manula
Mabeki
Chilambo
Zouzou
Lawi
Twalib
Viungo
Himid
Zidane
Kibeku
Kitambala
Akaminko
Diakite
Mchezaji bora wa mchezo

Beki Lameck Lawi alichaguliwa kuwa mchezaji bora. Nyota huyo alifunga goli pekee la ushindi dakika ya 73 ambalo lilidumu mpaka mwisho. Ni zawadi ya milioni mbili alikabidhiwa baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora.
Kocha Simba SC Steve Barker kapishana na kombe
Steve Barker, Kocha Mkuu wa Simba SC amepishana na kombe la Mapinduzi. Kupoteza mbele ya Azam FC kunawakosesha tiketi kusonga mbele. Unakuwa mchezo wa kwanza kupoteza akiwa kwenye benchi la ufuni.
“Tulikuwa tunahitaji matokeo mazuri kuendelea kwenye mashindano lakini haijawezekana. Wachezaji walipata nafasi lakini hawakuzitumia. Tutakwenda kufanyia kazi makosa ili kuwa bora,”.
Maoni ya Ibenge, kocha wa Azam FC
Florent Ibenge, Kocha Mkuu wa Azam FC amesema wachezaji walijituma na kutengeneza nafasi. Kwa namna ambavyo wamechezaji ni furaha kupata matokeo mazuri.
“Maandalizi ambayo tulifanya yalikuwa kwa umakini. Vijana wamejituma na kucheza vizuri. Kwa matokeo tuliyopata bado tunapaswa kufanya vizuri mchezo ujao,”.
Hitimisho
Azam FC yaivuruga Simba SC kwa kuwaondoa katika NMB Mapinduzi Cup. Kijana Lameck Lawi alizima ndoto za mnyama kutinga hatua ya fainali. Lango la Azam FC lilikuwa linalindwa na mchezaji wa zamani wa Simba SC, Aishi Manula.

