Washindi wa Jackpot bonus ya SportPesa wafungukia ushindi wao.
Washindi wa Jackpot bonus ya SportPesa wafungukia ushindi wao.
BAADA ya kufanikiwa kujishindia mamilioni ya Jackpot bonus ya SportPesa, washindi watatu wameibuka na kufungia ushindi wao.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Sixbert Ndimbo mkazi wa Ruvuma ambaye mfanyabiashara alisema kuwa “Nilianza kucheza na SportPesa mwaka 2018 na kufanikiwa kushinda kiasi kidogo cha Shilingi 10, 000 na 20, 000 lakini safari hii nimeshinda kiasi kikubwa.
“Fedha hizi nimepanga kuzipeleka katika biashara zangu kwa kuongeza mtaji baada ya kushinda Jackpot bonus ya Sh 9, 267, 964,”alisema Ndimbo.
Kwa upande wa Joseph Nkini kutoka mkoa wa Kilimanjaro alisema kuwa “Nafurahia kushinda bonus ya Shilingi 7, 764, 036 ambazo kwangu ni nyingi kutokana na kazi yangu ya ufundi ujenzi ninayoifanya.
“Nilishawishika kuanza kucheza na SportPesa kutokana na uchezaji wake kutosumbua, odds zao zipo juu, nawashauri vijana kucheza na SportPesa,”alisema Nkini.
Naye Dickson Kachinda mkazi wa Manyoni, Singida aliyeshinda Jackpot bonus ya shilingi 7, 764, 036 alisema kuwa “Nilianza kucheza na SportPesa mwaka, 2019 nilishawishika kucheza baada ya kumuona mshindi wa bonasi ya Sh 200Mil kutoka Singida.
“Ndiyo na mimi nikaanza kucheza na SportPesa na kilichonishawishi kucheza Jackpot
ni kutoka kwenye mfumo wa bando na kucheza kwa njia ya kawaida,”alisema Kachinda.
Kwa upande wa Sportpesa Meneja Uhusiano na Mawasiliano Sabrina Msuya amesema kila wiki tunazidi kutoa washindi wa Jackpot bonus kuanzia mechi 10-12 na hakuna haja ya kukata tamaa kwani usiposhinda Jackpot basi bonus unaweza pata.
Jackpot yetu kwa sasa ni 595,659,980Tsh hivyo napenda kuwahamasisha wadau wa michezo kujaribu bahati yao ya kushinda kiasi hiki cha pesa ili kubadili maisha yao.
Mwisho