skip to Main Content
Mwongono Wa Timu – Manchester City
manchester-city

Mwongono wa timu – Manchester City

MANCHESTER City inajulikana duniani kama moja ya timu ya Ligi Kuu England yenye nguvu kubwa. Kwa kipindi cha misimu ya hivi karibuni, imekuwa ni timu isiyofungika – na chache zimeweza kufanya hivyo. Lakini muongo mmoja uliopita, ilikuwa habari tofauti na miaka ya kwanza 120 ya Manchester City kati ya 130 ilikuwa tofauti na ilikuwa ikitajwa kama “timu nyingine ya Manchester.”

Hebu tuangalie kuhusu stori yao, na watu ambao walikuwa nguzo kuiwezesha kuwa timu kama ilivyo sasa kwenye ligi.

Siku za mwanzo

Manchester City kiuhalisia ni kongwe zaidi kati ya timu mbili za Manchester, na kongwe zaidi kwenye ligi yote ya soka. Ilianzishwa na binti wa msimamizi wa Kanisa la St Mark’s Church kule eneo la Gorton mwanzoni mwa miaka ya 1880. Alitaka kuwafanya wanaume wa eneo hilo kuwa na kitu cha kufanya wakati wa mapumziko na kutokuleta vurugu. Jina kamili la Manchester City lilikubaliwa na kuundwa rasmi mwaka 1896.

City ilijiunga kwenye ligi miaka miwili baadaye na ikafanya makubwa, ikifanikiwa kupanda kutoka Ligi Daraja la Kwanza mwaka 1899. Miaka mitano baadaye, timu ilitwaa taji laje la kwanza la FA na ikimaliza nafasi ya pili kwenye ligi. Na mambo yakaendelea kuwa mazuri kwa kipindi cha miaka 30 iliyofuata kwa vijana hao wa jezi ya rangi ya bluu. Wakati majirani zao Manchester United wakiibuka na kutawala soka la Uingereza, City walikuwa wakikabiliwa na matatizo ya kifedha na ikatishia uwepo wake. Walitakiwa kusubiri hadi mwanzoni mwa miaka ya 1930 ambapo City ikawa na taji kwenye kabati lake. Baada ya miaka migumu, wakafuzu fainali ya FA kwa miaka miwili mfululizo, wakipoteza kwa Everton mwaka 1933, lakini wakawafunga Portsmouth mwaka uliofuata.

Sapoti imara 

Mafanikio yao yalikuwa ni madogo baada ya vita vya dunia, huku wakitokea kwenye fainali mara chache sana na kuwa na nyakati za kushuka Daraja la Pili na kupanda. Kwa maneno mengine, stori yao inafanana na timu nyingine ambazo mara kwa mara zimekuwa zikipambana katikati ya msimamo na kileleni.

Kitu cha kufurahisha ni kwamba, licha ya kukabiliwa na wakati mgumu, huku Manchester United wakiendelea kung’ara kule juu, mashabiki wa nyumbani wa City mara zote waliendelea kuiunga mkono kwa nguvu zaidi kushinda hata majirani zao. Hicho kinaelezea kile kilichotokea wakati wa mafanikio ya Kombe la FA mwaka 1934. Katika raundi ya sita waliwakabili Stoke City pale Maine Road na mashabiki 84,569 walihudhuria kuwapa sapoti.

Ilikuwa ni idadi kubwa ya mashabiki ambayo haijawahi kushuhudiwa kabla, sio tu hapo Maine Road, na kule Old Trafford bali sehemu yoyote. Kiukweli iliendelea kuweka rekodi ya kuhudhuriwa mashabiki wengi zaidi nyumbani kwa kipindi cha miaka 82, ilikuja kuvunjwa mwaka 2016 wakati Tottenham ilipocheza na Beyer Leverkusen kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya katika Uwanja wa Wembley ambao walikuwa wakiutumia kama uwanja wa nyumbani kwa muda.

Kutoka Hyde Road hadi Ethiad

Ukizungumzia viwanja vipya, Manchester City imeondoka kwenye viwanja kadhaa vya nyumbani kwa miaka na miaka, wakati mwingine kwa kuchagua na wakati mwingine kutokana na umuhimu. Katika miaka ya ujenzi, klabu ilikuwa na kitu fulani ikitoka kwenye uwanja mmoja wa nyumbani kwenda mwingine. Mwaka 1887, ilihamia kwenye uwanja wao wa sita wa nyumbani ndani ya miaka saba, na wakahamia uwanja jirani na hoteli ya Hyde Road. Uhamisho huo uliwapa hamasa, na haraka klabu na hoteli wakajenga uwanja kwa ushirikiano, huku wachezaji wakitumia vifaa vyao na baadaye kuleta bidhaa kwenye hoteli na baa kuviuza baada ya kila mchezo.

Uwanja ukajengwa kwa wiki chache, na ukaongezwa na kupanuliwa kwa kipindi cha miaka iliyofuata. Hata hivyo, hili likaifanya klabu kuwa na umaarufu mkubwa na kuleta matatizo makubwa. Mwaka 1913, mchezo wa kombe dhidi ya Sunderland ulivutia watazamani ambao waliripotiwa kuwa 41,709, ingawa wengi wanaamini walikuwa wengi kushinda hao. Kujaa kwa mashabiki kukawafanya kuvamia uwanjani, na mwamuzi hakuwa na njia nyingine zaidi ya kusitisha mechi, Iikawa wazi kwamba, City walihitaji kutafuta uwanja mpya wa nyumbani, na ingawa kulikuwa na wazo la kuupanua zaidi Uwanja wa Hyde Road, mpango wo ulilazimika kusitishwa baada ya miale ya sigara iliposababisha moto mkubwa. Vitu vingi viliungua, lakini majukwaa yalibaki.

Mwaka 1923, Manchester City ilihamia kwenye uwanja wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 pale Maine Road, na walikaa hapo kwa kipindi cha miaka 80 iliyofuata. Ukiwa ndio uwanja wao wa nyumbani kwa City, uwanja huo ulitumika mara kadhaa kwenye mechi za nusu fainali ya Kombe la FA na Ngao ya Hisani kwa kipindi cha miaka, pia ukitumika katika mechi mbili za kimataifa miaka ya 1940.

Maine Road ulikuwa uwanja ambao uliwapokea mashabiki zaidi ya 84,000 kwenye fainali hiyo maarufu ya FA mwaka 1934. Lakini karne ya 21, hilo lingekuwa ngumu kulikubali. Sheria mpya zilitungwa msimu wa 1994-95 na kuruhusu viwanja vyote kuwa na viti vya kukaa. Hilo likapunguza uwezo wa Maine Road na kubaki kuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 35,000 tu.

Kwa mara nyingine mpango wa kupanua uwanja ukaja, lakini uwanja huo ulikuwa hauwezi kupanuliwa zaidi ya hapo na sasa kukawa na wazo la kutafuta uwanja mwingine. Hapo timu ikahamia kwenye Uwanja wa City of Manchester, ambao sasa unajulikana kama Ethiad uliobadilishwa mwaka 2003. Uwanja ulijengwa kwa ajili ya michezo ya Jumuiya ya Madola ya mwaka 2002. Kwa kuwa ulikuwa uwanja wa kisasa kwa karne ya 21, umetumika pia katika michezo ya riadha, rugby na hata mapambano ya masumbwi.

Kitu muhimu zaidi kwa sasa ni kwamba, wametimiza malengo na Manchester City hatimaye imefanikiwa kuwa timu yenye nguvu kubwa.

Miaka ya ajabu

Kuchomoza kwa City kutoka katikati ya msimamo hadi kutawala kileleni kuna sababu kubwa iliyochangia hilo. Lakini ilikuwa kama Chelsea kabla kwa kubadili umiliki wa klabu. Septemba mwaka 2008, Kampuni ya Abu Dhabi United Group (ADUG) ilichukuwa utawala na kuifanya kuwa timu tajiri zaidi kwenye Ligi Kuu England.

ADUG ilimwaga fedha kwenye kila sehemu, kuweka mambo ya kisasa ya uendeshaji wa klabu. Pia wakamchukua Roberto Mancini kuwa kocha wao na wakatumia fedha nyingi kwenye usajili wa wachezaji na kuwa na uwezo wa kwenda samabamba na PSG au Real Madrid na hilo likaifanya Manchester City kuwa moja ya timu ngumu kuzifunga na hapo ikawa timu ya ushindi na siyo ya kushindwa.

Mwaka 2011, walishinda taji la FA likiwa la kwanza kwa City kwa kipindi cha miaka 35. Waliiondosha Manchester United katika njia yao kwenda kwenye fainali na wakashinda. Huku sasa ikiwa na tabia ya ushindi, mambo yalibadilika na sasa Manchester City ikaingia kwenye zama mpya za kuweza kusajili mchezaji yeyote.

Na mipango ikawa tofauti huku Mancini akipewa chochote kwa ajili ya kubadilisha staili ya timu, lakini hilo halikuwa suluhisho la kudumu, kwani akabadilisha na nafasi yake kupewa Manuel Pellegrini kutoka Chie. Ulikuwa ujio wa Pep Guardiola ambao ukaifanya City kuwa juu zaidi kwa kushindana na timu nyingine sita kubwa.

Wachezaji alama

Angalau ni ukweli. Wamiliki, makocha na mameneja wamechangia mafanikio au kufeli kwa timu. Lakini kuna kitu kimoja ambacho si Pep Guardiola wala mmiliki wa ADUG, Sheikh Mansour bin Zayed Al Nahyan anayeweza kukifanya, kwamba kwenda dimbani Jumamosi mchana na kufunga mabao.

Manchester City imetengeneza umaarufu, katika nyakati mbaya na zile zuri, ni sehemu ya nyota waliovaa jezi kwa miaka. Hebu tuangalia majina ya wachezaji waliochangia mafanikio ya timu hiyo.

  • Bert Trautmann – Leo hii, wakati wachezaji wakizungumzia kukabiliwa na wakati mgumu, mara zote wanaungana na mitandao ya kijamii kufanya hivyo. Bert Trautmann alikuwa mfungwa wa Ujerumani ambaye alikataa kurudi nyumbani mwaka 1948 na akachagua kujenga maisha yake mwenyewe nchini England. Alijiunga na Manchester City baada ya wakati mzuri kule St Helens, na kuwa golikipa chaguo namba moja mwanzoni mwa miaka ya 1960. Na akawa sehemu ya familia ya City na kuwa mchezaji aliyependwa zaidi.
  • Mike Summerbee – Tayari tumesema kwamba mataji yalikuwa machache kwa City kipindi cha karne ya 20. Bado Mike Summerbee alikuwa pale kwa nyakati zote, na wakafanikiwa kupata taji miaka ya 1960. Lakini bila ujuzi wake, kasi na kufikiri kwa haraka kwenye winga, kwa uhakika ingekuwa habari nyingine kabisa. Sasa akiwa na umri wa miaka 70 na ushee, Summerbee bado ni familia ya pale kwenye dimba la Ethiad na amekuwa balozi wa mfano.
  • Pablo Zabaleta –Kuna waliofanya mazuri kabla ya Guardiola, na muhimu kuwapa shukrani kwa kile walichokifanya. Pablo Zabaleta alikuwa mmoja wa walioleta mafanikio wakati wa zama za Mancini. Alikuwa pale kuongoza mapinduzi na alikuwa na timu. Zabaleta alikuwa wa aina yake, akicheza sehemu yoyote ambayo alitakiwa kufanya hivyo katika hali yoyote, na wakati alipoondoka mwishoni mwa mwaka 2017 kujiunga na West Ham, ilikuwa kama kusema kwa heri kwa moja ya familia yake.
  • Yaya Toure – Wakati mwingine ni suala la muda tu. Toure mmoja wa wachezaji wote ambao wanajua nini anachotakiwa kufanya wakiwa dimbani. Katika msimu wake wa kwanza, alifunga bao la ushindi kwenye nusu fainali na fainali ya FA mwaka 2011 na mwaka uliofuata, mabao yake mawili dhidi ya Exeter katika raundi ya awali ya Ligi Kuu na kuiwezesha City kuwa kileleni.
  • David Silva – Wote tunahitaji maajabu kidogo kwenye maisha yetu, na ndio hicho ambacho El Mago alikileta kwa mashabiki wa City kwa kipindi cha miaka 10 ya kuwepo pale. Staili yake na uwezo wa kucheza na mpira na kufunga mabao pamoja na kutoa pasi za mwisho za kutosha kulichangia mafanikio ya timu. Ni mfano mzuri kuwa mmoja waliochangia mafanikio ya City.
  • Sergio Aguero – Hatimaye, huu ni usajili uliolipa zaidi kwa Manchester City. Kitu pekee kilochokuwa kikihitajika kutoka kwake ni kufunga mabao na hilo alilifanya bila kuchoka. Aguero hakuwa straika maarufu wa kila timu kumpigania wakati aliposajiliwa na City miaka 10 iliyopita, lakini sasa ni tofauti kabisa. Akawa mfungaji bora anayeongoza katika historia ya klabu hiyo. Mchango wake umesaidia sana mafanikio ya Manchester City kitu ambacho hakitasahaulika kamwe.

 

Share this:
Back To Top