Usajili mpya Yanga SC 2026/27Manqoba
  • Rasmi Kocha mpya Yanga SC 2026/27 ametambulishwa kukinoa kikosi hicho msimu wa 2026/27 ni raia wa Afrika Kusini
  • Manqoba Mngqith ana miaka 55 amepewa jina la kocha wa makombe kutokana na CV yake aliwahi kuifundisha Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini
  • Simba SC vs Yanga SC, Ngao ya Jamii Agosti 12,2026 utakuwa mchezo wake wa kwanza katika ardhi ya Bongo

Rasmi kocha mpya Yanga SC 2026/27 ametambulishwa akiwa na CV kubwa tayari kwa kazi mpya msimu wa 2026/27. Anaitwa Manqoba Mngqith ni raia wa Afrika Kusini. Anachukua mikoba ya Pedro Goncalves ambaye alisitishiwa mkataba wake kabla ya msimu kufika mwisho. Timu hiyo ilikuwa chini ya Kocha Mkuu Abdihamid Moalin aliyekiongoza kikosi kutwaa ubingwa.

Ijue historia ya Yanga SC: Yanga SC: Historia, Usajili wote, kikosi, Ratiba, Matokeo na Takwimu

Je, bado hujashinda mamilioni ya aviator ‘Kindege’ cha SportPesa? Cheza ushinde mamilioni sasa

Changamka! sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

SportPesa Aviator Challenge

Kocha mpya Yanga SC CV yake hii hapa

kocha mpya Yanga SC 2026/27
Manqoba kocha mpya Yanga SC

Ujenzi wa uwanja mpya Yanga SC: Uwanja mpya wa Yanga SC huu hapa | GSM 50/50 Wananchi, Ligi Kuu Bara (NBC Premier League)

Sportpesa Aviator Rain Free Bets- Mil

Safari ya msimu wa 2026/27 kocha mpya Yanga SC inatarajiwa kuanza akitajwa kuwa ni mtu wa makombe. Mchezo wake wa kwanza unatarajiwa kuwa Ngao ya Jamii vs Simba SC. Ni Agosti 12,2026 watani hawa wa jadi wanatarajiwa kukutana kwenye mchezo wa ufunguzi wa ligi.

Kipindi / MiakaTimu / Klabu AlizofundishaMafanikio / Majukumu Makubwa
Hatua za AwaliMaritzburg City, Moja United, Highlanders, Chuo Kikuu cha KwaZulu-NatalKujenga misingi ya ukufunzi na kukuza vipaji vya vijana.
2007 – 2010Golden ArrowsAliiwezesha timu kutwaa ubingwa wa kihistoria wa MTN 8 (2009).
2010 – 2011AmaZulu FCKocha Mkuu wa kikosi hicho kinachoshiriki Ligi Kuu.
2012Chippa UnitedAlihudumu kama Kocha Mkuu kwa kipindi kifupi.
2012 – 2013Golden ArrowsAlirejea kwa awamu ya pili kuinoa klabu hiyo.
2013 – 2020Mamelodi SundownsKocha Msaidizi chini ya Pitso Mosimane (Alishinda CAF Champions League 2016).
2020 – 2024Mamelodi SundownsAlipandishwa na kuwa Kocha Mwenza (Co-head coach) na baadaye Kocha Mkuu (2024).
2025Golden ArrowsAlirejea tena nyumbani kuifundisha timu hiyo kama Kocha Mkuu.
Julai 2026 – SasaYoung Africans SC (Yanga)Ametambulishwa rasmi kuwa Kocha Mkuu mpya wa mabingwa wa Tanzania.

Kocha mpya Yanga SC orodha ya tuzo na mataji

Rekodi zinaonyesha kwamba kocha mpya Yanga SC 2026/27 kabati lake lina tuzo nyingi. Mwendelezo huo unasubiriwa Jangwani. Atakuwa na kibarua cha kutetea ubingwa wa ligi ambao upo mikononi mwa Wananchi waliotwaa msimu wa 2025/26 ikiwa ni mara ya 5 mfululizo na mdhamini mkuu ni SportPesa.

Kipengele / ShindanoIdadi ya Mataji / TuzoMaelezo ya Ziada
Kocha Bora wa Msimu (Coach of the Season)1Alitwaa tuzo hii katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini msimu wa 2021/22.
Bingwa wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini9Alishinda mataji haya akiwa na benchi la ufundi la Mamelodi Sundowns (kama Kocha Mkuu na Kocha Msaidizi).
Bingwa wa MTN8 Cup2Alitwaa kombe hili akiwa na Golden Arrows (2009) na Mamelodi Sundowns.
Bingwa wa Kombe la Ligi (League Cup / Telkom Knockout)3Alishinda mataji haya akiiongoza timu yake kufanya vizuri kwenye michuano ya ndani.
Bingwa wa FA Cup ya Afrika Kusini (Nedbank Cup)3Vikombe vya michuano mikuu ya mtoano nchini Afrika Kusini.
Bingwa wa CAF Champions League1Alitwaa taji hili kubwa la Afrika akiwa na Mamelodi Sundowns mwaka 2016.
Bingwa wa CAF Super Cup1Alishinda taji hili la ubingwa wa mabingwa wa Afrika.
Bingwa wa CAF African Football League (AFL)1Alitwaa taji hili la kihistoria katika msimu wake wa kwanza wa uzinduzi.

Hitimisho

Kocha mpya Yanga SC 2026/27 anakuja kuanza na timu upya kabla msimu haujaanza. Awali jina la Fadlu Davids aliyewahi kuinoa Simba SC lilikuwa linatajwa. Hivyo kutambulishwa kwake kumefuta tetesi hizo na rasmi Manqoba atakuwa kwenye benchi la ufundi.

Share this: