- FT: Mashujaa FC (0) vs Simba SC (3) NBC Premier League Mei 14, 2026 Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma.
- Clatous Chama amefunga magoli mawili na Seleman Mwalimu amfunga goli moja
- Mashujaa FC imecheza mechi mbili na Simba SC
Mwisho wa reli Kigoma Mashujaa FC (0) VS Simba SC NBC Premier League matokeo rasmi mchezo uliochezwa Uwanja wa Lake Tanganyika. Clatous Chama alianza kujiamulia mambo mapema dakika ya 5 kwa goli la kona iliyojaa nyavuni na dakika ya 70 akafunga. Seleman Mwalimu alifunga goli la tatu dakika ya 90+2. Huu unakuwa ushindi mkubwa wa kwanza kwa mnyama ugenini dhidi ya Sokwe.
SOMA HII: Ratiba ya mechi zilizobakia za Simba SC kwenye NBC Premier League 2025/26 | SportPesa Blog
Je, Unataka kushinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa
Ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege kupitia kampuni bora ya kubashiri ya SportPesa. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Mashujaa FC (0) VS Simba SC NBC Premier League vita ya ubingwa inaanza upya

Baada ya ubao kusoma Mashujaa FC (0) VS Simba SC NBC Premier League vita ya ubingwa inaanza upya kutokana na tofauti ya pointi mbili kubaki dhidi ya vinara. Mnyama anafikisha jumla ya pointi 52 nafasi ya pili huku vinara Yanga SC wakiwa na pointi 54. Watani hawa wote wamebakiwa na mechi 7 kukamilisha msimu wa 2025/26.

H2H Mashujaa FC vs Simba SC

| Tarehe | Mechi | Matokeo |
|---|---|---|
| 03/02/2023 | Mashujaa FC vs Simba SC | 0-1 |
| 15/03/2024 | Simba SC vs Mashujaa FC | 2-0 |
| 01/11/2024 | Mashujaa FC vs Simba SC | 0-1 |
| 02/05/2025 | Simba SC vs Mashujaa FC | 2-1 |
| 29/01/2026 | Simba SC vs Mashujaa FC | 2-0 |
| 14/05/2026 | Mashujaa FC vs Simba SC | 0-3 |
Mnyama amepata ushindi kwenye mechi zote 6 walizokutana na Mashujaa FC NBC Premier League. Matokeo ya leo Mei 14, 2026 yanavunja rekodi ya ushindi mkubwa. Sokwe ni goli moja amefunga mbele ya mnyama.
Hitimisho
Ni Mashujaa FC (0) vs Simba SC NBC Premier League yanachangamsha upya kazi ndani ya ligi. Wababe wawili tofauti yao kwa sasa ni pointi mbili kutoka 5 za awali.Je nani atakuwa bingwa ndani ya ligi? Endelea kufuatilia SportPesa Blog.

