Feisal Salum ni King of Asisti ndani ya Tanzania Premier League akiwa amefikisha 7
Mechi 10 Azam FC wamepata sare kwenye msimamo nafasi ya 3
Unbeaten 19 Azam F.C NBC Premier League 2025/26 chini ya Kocha Mkuu, Florent Ibenge. Matokeo ya mchezo uliopita hivi punde Azam FC 3-0 JKT Tanzania. Huu ulikuwa ni mchezo wa 19 kwenye ligi uliochezwa Uwanja wa Azam Complex. Wanafikia rekodi ya Yanga SC ambayo nayo imecheza imechi 19 bila kupoteza.
Feisal Salum kiungo mshambuliaji wa Azam FC: Source: Azam FC.
Wamefikisha Unbeaten 19 Azam F.C NBC Premier League 2025/26. Hii inatokana na kiwango kuendelea kuwa bora kwenye mechi za ushindani. Licha ya kutofungwa wanaongoza kwa kupata sare nyingi ambazo ni 10. Kwenye mechi 19 ushindi ni mechi 9 pekee.
Idd Nado nyota wa Azam FC kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania. Source: Azam FC.
Azam FC imepata ushindi mkubwa kwenye mechi 4. Katika mechi hizo walipata ushindi wa magoli 3-0 bila kuruhusu kufungwa. Kipa namba moja ni Aishi Manula aliyesajiliwa hapo akitokea kikosi cha Simba SC 2024/25.
Tarehe
Mechi
Matokeo
17 Apr 2026
Azam FC vs JKT Tanzania
3-0
11 Mar 2026
Dodoma Jiji FC vs Azam FC
0-3
25 Feb 2026
Azam FC vs Mtibwa Sugar
3-0
17 Jan 2026
Azam FC vs Coastal Union
3-0
Feisal Salum King of Asisti
Kiungo mshambuliaji wa Azam FC, Feisal Salum ni King of Asisti NBC Premier League akiwa amefikisha 7. Mbali na kutengeneza pasi kwa wengine amefunga magoli 7. Jumla amehusika katika magoli 14 kati ya 26 yaliyofungwa na timu hiyo iliyo nafasi ya 3 kwenye msimamo.
Unbeaten 19 Azam F.C NBC Premier League ndani ya 2025/26. Msimu wa 2013/14 Azam F.C ilitwaa taji la Ligi Kuu Tanzania Bara bila kupoteza mchezo. Rekodi hiyo itafikiwa kwa mara nyingine? Endelea kufuatilia SportPesa Blog kwa taarifa na matokeo zaidi.