- MC Alger walitunishiana misuli na mabosi wa Yanga SC kuiwinda saini ya winga Okelo.
- Deal done Allan Okelo asaini miaka miwili Yanga SC akitokea Vipers FC
- Injinia Hersi Said Rais wa Yanga SC asimamia shughuli mwanzo mwisho, usiku mnene atambulishwa.
Deal Done Allan Okelo asaini miaka miwili Yanga SC kwenye dirisha dogo la usajili. Hii ni baada ya awali tetesi kueleza kwamba tayari ameshajiunga na Wananchi. Kijana huyo mwenye miaka 25 alizaliwa Julai 4 2000. Ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa kwenye timu ya taifa ya Uganda AFCON 2025 hatua ya makundi nchini Morocco.
SOMA HII: Allan Okello mambo fresh Yanga SC/ Orodha ya wapya waliotambulishwa
Bado hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Deal Done Allan Okelo asaini miaka miwili Yanga SC

Kwa lugha rahisi kwa sasa Deal Done Allan Okelo asaini miaka miwili Yanga SC akitokea Klabu ya Vipers ya Uganda. Rais wa Yanga SC, Injinia Hersi Said aliongoza jahazi kupatikana kwa saini ya kijana huyo. Haikuwa rahisi kutokana na kuwa tegemeo katika kikosi cha Vipers ya Uganda.
Mbali na Vipers ya Uganda kuhitaji huduma yake bado alikuwa na mkataba uliosalia miezi 6 kuitumikia timu hiyo. Kutokana na umuhimu wa mahitaji ya Jangwani walikubali kuvunja mkataba na kuipata saini yake. Kwa sasa anakuwa mchezaji halali wa Yanga SC baada ya kutambulishwa usiku wa kuamkia Januari 13 2026.
Rekodi za Allan Okelo AFCON 2025
| Mechi | Goal | Asists |
| 3 | 0 | 0 |
Utambulisho wa Allan Okelo washtua
Utambulisho wa winga Allan Okelo umeshtua Bongo kutokana na mashabiki kusubiri kwa shauku kubwa. Mapema asubuhi Yanga SC walipandisha ujumbe wakibainisha kuwa tayari ameshafika. Mazungumzo ya Rais wa Yanga SC Injinia Hersi Said na Meneja wa Idara ya Habari Yanga Ally Kamwe yalionesha msisitizo kwamba kesi imeisha.
Injinia alitoa mapendekezo kuwa mchezaji huyo anapaswa kuwa zawadi ya Mapinduzi ambay yalifanyika usiku. Kamwe alimjibu kwamba kama jambo limekamilika kesi imeshaisha. Hali hiyo iliongeza shauku kwa mashabiki kusubiri zawadi ya Mapinduzi 2026.
SOMA HII: Usajili Yanga SC umeanza Emmanuel Samuel asaini miwili/ Okello mkataba mpya

Allan okelo avunja rekodi

Baada ya kusaini Yanga SC Allan Okelo avunja rekodi ya kuwa mchezaji ambaye atakuwa analipwa mshahara mkubwa. Hii inatokana na winga huyo kuwa na ofa zaidi ya mbili mkononi. MC Alger walikuwa wanatajwa kwa ukaribu kuiwinda saini yake.
Hivyo kukubali kusaini miaka miwili ndani ya kikosi cha Yanga SC kunamaanisha kwamba amepewa maslahi mazuri. Yupo tayari Dar baada ya utambulisho wake kazi mpya inaanza. Muda mfupi kabla ya utambulisho wake aliwaaga mashabiki wa Vipers na kuwashukuru viongozi wa timu hiyo.
Orodha ya wanaofuata
Amos Yona
Yanga SC inatajwa kuwa kwenye hesabu za kuinasa saini ya mlinda mlango wa Pamba Jiji, Amosi Yona. Vita imekuwa kubwa kwa mabosi wa timu hiyo kuipata saini yake kwa kuwa kuna timu zaidi ya mbili zinahitaji huduma yake.
Singida Black Stars yinayotumia Uwanja wa Liti ipo kwenye orodha katika timu ambazo zinawania saini yake. Inatajwa kuwa na Simba SC ipo sokoni inamuhitaji kipa huyo.
Depu
Dirson Maria maarufu kama Depu raia wa Angola anatajwa kufikia hatua nzuri kusaini Yanga SC. Huyu ni mshambuliaji ambaye ana tuzo ya ufungaji bora COSAFA. Rekodi zinaonyesha kuwa kwenye mechi 13 alifunga magoli 12. Hivyo Yanga SC wamefikia hatua nzuri kupata saini ya nyota huyo.
Hitimisho
Deal Done Allan Okelo asaini miaka miwili Yanga SC ni mwendelezo wa utambulisho wa wapya ndani ya Jangwani. Tayari kuna wachezaji wengine wamekubaliana na timu hiyo kilichobaki ni utambulisho. Timu hiyo ina kazi kupeperusha bendera kitaifa na kimataifa ambapo mchezo ujao kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ni Aly Ahly vs Yanga SC.

