Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi CupHimid Zenji
  • Prince Dube ameanza kikosi cha kwanza kuwakabili mabosi wake wa zamani
  • Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup vikosi vya timu zote mbili hadharani
  • Simba SC na Singida Black Stars ziliishia hatua ya nusu fainali zitawatazama kupitia luninga

Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup bingwa mpya anakwenda kusakwa. Mashindano haya yalianza hatua ya makundi huku timu tano zikishiriki kutoka bara. Singida Black Stars iliondowa na Yanga SC hatua ya nusu fainali. Wababe Simba SC waliondolewa na Azam FC hivyo wote watatazama mchezo wa leo kwenye luninga.

SOMA HII: Azam FC yaivuruga Simba SC yaifunga mara mbili mfululizo/ Kariakoo Dabi hakuna tena

Vuna mamilioni sasa hivi

Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini, muda ni wako na nafasi ya ushindi inakusubiri.

image

Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup nani atashinda?

Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup
Pacome kiungo mshambuliaji wa Yanga SC. Source: Yanga SC.

Kwenye mchezo wa leo Azam FC vs Yanga SC fainali ya Mapinduzi Cup duru zinaipa ushindi Yanga SC. Licha ya watoto wa Jangwani kupewa nafasi kubwa kupata ushindi haiondoi ugumu uliopo mchezo wa leo. Ikumbukwe kwamba Azam FC iliwafungashia virago Simba SC hivyo sio yakuibeza.

Matokeo ya mechi za hatua ya nusu fainali

Azam SC 1-0 Simba SC

Singida Black Stars 0-1 Singida Black Stars.

Wachezaji waliofunga hatua ya nusu fainali

Lameck Lawi beki alifunga kwa Azam FC

Maxi Nzengeli alifunga kwa Yanga SC yeye ni kiungo mshambuliaji.

SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi

image

Kikosi cha Yanga SC kitakachoanza dhidi ya Azam FC

Langoni

Aboutwalib Mshery

Mabeki

Kibwana Shomari

Boka

Dickson Job

Ibrahim Bacca

Viungo

Conte

Maxi Nzengeli

Duke Abuya

Pacome

Celestin Ecua

Mshambuliaji

Prince Dube

Kocha Mkuu, Pedro Goncalves.

Wachezaji wa akiba

Semsey, Yao, Hussein, Assinki, Nondo, Edmund, Mudathir, Sheikhan, Mwanengo.

Kikosi cha Azam FC vs Yanga SC

Azam FC
Nyota wa Azam FC Mtasigwa kwenye mazoezi. Source: Azam FC.

Langoni

Aishi Manula

Mabeki

Chilambo

Zouzou

Lamek Lawi

Twalib

Viungo

Himid

Zidane

Feisal

Kitambala

Akaminko

Mshambuliaji

Diakite

Kocha Mkuu, Florent Ibenge

Wachezaji wa akiba

Anthony, Yoro, Manyama, Mtasingwa, Caleb, Kanoute, Mnumba, Doudou, Zayd, Kamanya, Bela, Alobogast.

SOMA HII: Ratiba ya Yanga SC 2025/26 NBC Premier League, CAF Champions League/ Live scores

image

Safari mpaka fainali

Azam FC kundi A

Azam FC 1-1 Singida Black Stars

Mlandege FC 0-2 Azam FC

URA 1-2 Azam FC

Azam FC 1-0 Simba SC.

Matokeo ya Yanga SC

Yanga SC ilikuwa kundi C

KVZ FC 0-3 Yanga SC

TRA United 0-1 Yanga SC

Singida Black Stars 0-1 Yanga SC.

Maoni ya makocha wa Azam FC vs Yanga SC

Yanga SC hawana utani wamerejea kazini
Pedro Kocha Mkuu wa Yanga SC. Source: Yanga SC.

Timu zote mbili ambazo zinakutana kwenye hatua ya fainali zimefika hapo kwa ushindi wa goli mojamoja hatua ya nusu fainali. Azam FC waliwaondoa vigogo Simba SC huku Yanga SC ikiwaondoa vigogo Singida Black Stars.

Inakuwa fainali ya makocha wapya kwenye timu zao ndani ya msimu wa 2025/26 hivyo mbinu zao zitajibu nani mkali. Kwa Yanga SC Pedro ni mchezo wa kwanza fainali na Azam FC ni mchezo wa kwanza kwenye fainali visiwani Zanzibar.

Pedro ameweka wazi kwamba anaamini mchezo utakuwa mgumu kutokana na timu pinzani kuwa na matokeo mazuri. Aliongeza kuwa licha ya ugumu uliopo watatumia nafasi watakazopata kwa umakini kwenye fainali.

Upande wa Kocha Mkuu wa Azam FC, Ibege alibainisha kuwa ni mchezo ambao unahitaji umakini mkubwa . Hii inatokana na uzoefu walionao wapinzani wao watapambana kupata matokeo mazuri.

Hitimisho

Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup ni mchezo unaokwenda kuhitimisha mashindano haya makubwa. TRA United, Singida Black Stars na Simba SC ziliaga mapema mashindano. Nyingine ni Mlandege, Fufuni nazo zitashuhudia bingwa akitwaa taji la kwanza ndani ya 2026.

Share this: