- Prince Dube ameanza kikosi cha kwanza kuwakabili mabosi wake wa zamani
- Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup vikosi vya timu zote mbili hadharani
- Simba SC na Singida Black Stars ziliishia hatua ya nusu fainali zitawatazama kupitia luninga
Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup bingwa mpya anakwenda kusakwa. Mashindano haya yalianza hatua ya makundi huku timu tano zikishiriki kutoka bara. Singida Black Stars iliondowa na Yanga SC hatua ya nusu fainali. Wababe Simba SC waliondolewa na Azam FC hivyo wote watatazama mchezo wa leo kwenye luninga.
SOMA HII: Azam FC yaivuruga Simba SC yaifunga mara mbili mfululizo/ Kariakoo Dabi hakuna tena
Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini, muda ni wako na nafasi ya ushindi inakusubiri.

Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup nani atashinda?

Kwenye mchezo wa leo Azam FC vs Yanga SC fainali ya Mapinduzi Cup duru zinaipa ushindi Yanga SC. Licha ya watoto wa Jangwani kupewa nafasi kubwa kupata ushindi haiondoi ugumu uliopo mchezo wa leo. Ikumbukwe kwamba Azam FC iliwafungashia virago Simba SC hivyo sio yakuibeza.
Matokeo ya mechi za hatua ya nusu fainali
Azam SC 1-0 Simba SC
Singida Black Stars 0-1 Singida Black Stars.
Wachezaji waliofunga hatua ya nusu fainali
Lameck Lawi beki alifunga kwa Azam FC
Maxi Nzengeli alifunga kwa Yanga SC yeye ni kiungo mshambuliaji.
SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi

Kikosi cha Yanga SC kitakachoanza dhidi ya Azam FC
Langoni
Aboutwalib Mshery
Mabeki
Kibwana Shomari
Boka
Dickson Job
Ibrahim Bacca
Viungo
Conte
Maxi Nzengeli
Duke Abuya
Pacome
Celestin Ecua
Mshambuliaji
Prince Dube
Kocha Mkuu, Pedro Goncalves.
Wachezaji wa akiba
Semsey, Yao, Hussein, Assinki, Nondo, Edmund, Mudathir, Sheikhan, Mwanengo.
Kikosi cha Azam FC vs Yanga SC

Langoni
Aishi Manula
Mabeki
Chilambo
Zouzou
Lamek Lawi
Twalib
Viungo
Himid
Zidane
Feisal
Kitambala
Akaminko
Mshambuliaji
Diakite
Kocha Mkuu, Florent Ibenge
Wachezaji wa akiba
Anthony, Yoro, Manyama, Mtasingwa, Caleb, Kanoute, Mnumba, Doudou, Zayd, Kamanya, Bela, Alobogast.
SOMA HII: Ratiba ya Yanga SC 2025/26 NBC Premier League, CAF Champions League/ Live scores

Safari mpaka fainali
Azam FC kundi A
Azam FC 1-1 Singida Black Stars
Mlandege FC 0-2 Azam FC
URA 1-2 Azam FC
Azam FC 1-0 Simba SC.
Matokeo ya Yanga SC
Yanga SC ilikuwa kundi C
KVZ FC 0-3 Yanga SC
TRA United 0-1 Yanga SC
Singida Black Stars 0-1 Yanga SC.
Maoni ya makocha wa Azam FC vs Yanga SC

Timu zote mbili ambazo zinakutana kwenye hatua ya fainali zimefika hapo kwa ushindi wa goli mojamoja hatua ya nusu fainali. Azam FC waliwaondoa vigogo Simba SC huku Yanga SC ikiwaondoa vigogo Singida Black Stars.
Inakuwa fainali ya makocha wapya kwenye timu zao ndani ya msimu wa 2025/26 hivyo mbinu zao zitajibu nani mkali. Kwa Yanga SC Pedro ni mchezo wa kwanza fainali na Azam FC ni mchezo wa kwanza kwenye fainali visiwani Zanzibar.
Pedro ameweka wazi kwamba anaamini mchezo utakuwa mgumu kutokana na timu pinzani kuwa na matokeo mazuri. Aliongeza kuwa licha ya ugumu uliopo watatumia nafasi watakazopata kwa umakini kwenye fainali.
Upande wa Kocha Mkuu wa Azam FC, Ibege alibainisha kuwa ni mchezo ambao unahitaji umakini mkubwa . Hii inatokana na uzoefu walionao wapinzani wao watapambana kupata matokeo mazuri.
Hitimisho
Azam FC vs Yanga SC fainali NMB Mapinduzi Cup ni mchezo unaokwenda kuhitimisha mashindano haya makubwa. TRA United, Singida Black Stars na Simba SC ziliaga mapema mashindano. Nyingine ni Mlandege, Fufuni nazo zitashuhudia bingwa akitwaa taji la kwanza ndani ya 2026.

