SportPesa JACKPOT, Jitafute Utajipata!
‘’Jitafute Utajipata’’, ni usemi wa siku za hivi karibuni, ulioanza kuzoeleka katika jamii kubwa ya Watanzania, ukiwa na maana ya kuhamasisha watanzania kuendeleza mapambano ya kujitafutia riziki mpaka pale atakapofanikiwa.
Kwa maana nyingine hakuna kusudio/nia ambalo/ambayo mtu ataamua kulitekeleza na lisimnufaishe katika utafutaji wake.
Hiyo ndiyo fursa ambayo Kampuni ya kubashiri ya SportPesa imeitoa kwa watanzania, kwa kipindi chote ambacho kampuni inaratibu shughuli zake tangu iingie hapa nchini.
Vijana wana usemi usemao kuwa atafutaye hachoki ukiona amechoka ujue kapata’’. Hapa tunamaanisha hakuna kulala mpaka kieleweke au upate unachostahili.
Kuna njia mbalimbali ambazo zinamuwezesha mtu yeyote kupata kipato cha kumuwezesha kuendesha maisha yake ya kila siku pale atakapoamua kukataa kuwa mnyonge.
Hapa tunazungumzia watu ambao hata iweje hawana nafasi nyingine katika maisha ambayo inaweza kuwakwamua na kuwavusha toka katika hali ya kimaisha waliyonayo na Kwenda kwenye hali ya mafanikio.
Naongelea kijana au mtu yeyote wa makamo au hata yule ambaye umri wake umeanza kumtupa mkono, akiwa anakaribia kustaafu kama ni mwajiriwa.
Au mtu asiye na elimu ya kufanya apate maslahi bora na ya juu, mtu mwenye changamoto za ki ulemavu ambazo zitamfanya kwa namna moja ama nyingine kukosa fursa za moja kwa moja zitakazompa kipato cha kujikimu yeye mwenyewe au na familia yake.
Katika makundi hayo niliyotaja hapo juu kuna walinzi, kuna boda boda, kuna madalali, kuna makuli, mama ntilie, kuna wabeba zege, kuna wapiga debe na wengine wengi.
Kupitia SportPesa hawa wote wana nafasi moja ambayo hawawezi kupewa na mtu yeyote zaidi ya wao wenyewe kuamua na kuchagua kwamba wanataka mabadiliko ya ukweli ya kiuchumi katika Maisha yao.
Hapa nazungumzia Jackpot za SportPesa ambazo zitamhitaji kijana, mtu wa makamo au mzee kucheza kwa kubashiri ili aweze kuapata nafasi ya kujikwamua katika lindi la umaskini.
Moja kati ya vitu ambavyo SportPesa inaweza kujivunia ni namna ilivyotoa fursa kwa watanzania kupitia Jackpot zake, yaani Jackpot ya kati kati ya wiki ambayo ikon zaidi ya Milioni 500 na Supa Jackpot ya zaidi ya Bilioni 1.
Takwimu zinaonyesha maelfu ya watanzania wamenufaika moja kwa moja na Jackpot bonus na Jackpot zenyewe. Mathalani mwezi wa Machi 2023, zaidi ya washindi 3000 wameshinda Jackpot bonus kwa viwango tofauti tofauti.
Hii ni zaidi ya fursa ambayo mtanzania amewekewa na SportPesa. Tunafahamu katika zawadi zetu kuna wanaolipia karo, wanaolipia pango la nyumba, wanaoendeleza biashara zao, wanaotumia pesa ya ushindi kama mtaji, wanaoweka akiba, wanaojengea au kumalizia au kurekebisha nyumba etc.
Aina ya matumizi hayo yanaelezea thamani ya zawadi ambayo wateja wetu wanashinda. Kwa hakika hivyo namna bora ya huu msemo ukijitafuta utajipata na Sportpesa.
Ukiangalia kwa namna ambavyo washindi wetu wanavyotangazwa utagundua uwakilishi wa makundi yote kuanzia rika, jinsia, mikoa na umri kwa mujibu wa sheria.
Sijui wewe msomaji unayesoma muda huu utakuwa kundi gani, lakini kwa ufupi tu wanafunzi wa vyuo, wakulima, waajiriwa katika nafasi mbali mbali kwenye kampuni binafsi, taasisi na mashirika ya kiserikali, madereva bodaboda, wafugaji.
Hapa katika kundi la boda boda na wafugaji kuna mifano halisi ya washindi wa Mwezi 03-2023. Mshindi wetu wa Jackpot bonus ya Tsh 56,383,640 alitokea alikuwa ni dereva boda boda.
Ndiyo, wengine ni mashuhuda katika hilo iwe kwa kushinda kiasi hicho cha fedha wao wenyewe au kwa kuona marafiki, ndugu na jamaa zao au hata watu wengine wakifanikiwa ‘kujizolea fedha baada ya kushinda ubashiri wao katika michezo mbalimbali ya mpira, Kasino na mengineyo ambayo huchezeshwa na kampuni ya SportPesa.
Historia ya Florian Massawe ambaye kwa sasa ni mmoja miongoni mwa matajiri wakubwa nchini imetoka mbali na hiyo ni baada ya kubashiri ‘mkeka’ wake wa Jackpot kwa kiasi cha Sh 2000, kwa wakati ule, na kufanikiwa kushinda michezo yote 13 ya Jackpot na kufanikiwa kushinda kiasi cha zaidi ya Sh Bilioni 1.na milioni 250.
Ilikuwa kama ndoto kwake, kwani kwa maelezo yake siku hiyo aliamka akiwa na mawazo sana kutokana na kuwa na akiba ya Sh 2000 mfukoni mwake ambacho kawa maelezo yake kisingemtosha hata kidogo katika mahitaji yake kwa siku hiyo j hatua iliyomfanya achukue uamuzi wa kubashiri ili kujitafutia fedha ya ziada.
Mimi huwa nabashiri mara kwa mara na pia nilikuwa nafuatilia kwenye mitandao ya kijamii namna washindi wengine wa SportPesa hasa hasa wa Jackpot walivyokuwa wanashinda na kutangazwa.
Kitendo kile kilinipa moyo wa kujiona na mimi kuna siku naweza tusua kamą was hindi wengise wali opita kutuka SportPesa.
Kwa mujibu wake anasema kabla ya kuweka mkeka ulioshinda, alipotazama orodha ya michezo za Jackpot hiyo, moja kwa moja alihamasika kucheza.
‘’Ushindi huu wa bilioni moja na ushehe ni kama ilikuwa ndoto yangu. Nakumbuka siku za nyuma nilikuwa nawaambia washikaji zangu kuna siku hii Jackpot ya mechi 13 nitaitusua.
Unajua nilliweka mkeka ulioshinda Jackpot ya zaidi ya bilioni moja na ushehe siku ya Alhamisi na Ijumaa. Nilitumia muda mrefu kidogo nikiwa nimekaa na kompyuta mpakato na simu zangu mbili nafuatilia takwimu za kila timu zilizopo kwenye Jackpot.
Baada ya kucheza nilisubiri mpaka mechi zilivyoanza kucheza na kuanza kufuatilia matokeo. Mkeka wa kwanza ulikufa siku ya Jumamosi nikiwa nimepatia mechi 6 tu.
Kwa bahati nzuri kile ambacho sikukitarajia katika ubashiri wangu kikatokea.
Mkeka wa pili ukaendela kupumua mpaka siku ya Jumapili usiku ambapo nilishinda mechi zote 13 za Jackpot na kujishindia hiyo zawadi kubwa ya 1,255,316,060″
Hivyo ndiyo ambavyo hata wewe inaweza kukutokea pale tu ambapo utachukua uamuazi ya kutumia Sh 1000 yako au hata zaidi ya kiasi hicho na kutengeneza mkeka/mikeka wako/yako vizuri ukikaa tayari kwa kusubiria ushindi unaoweza kukutoa katika hali ya maisha ulioyo nayo na kuongeza kipato chako.
Hivyo ndivyo mtu mwenye dhamira ya kubadilisha maisha yake anavyokuwa.
Kwa mantiki hiyo usikate tamaa na acha kuishi kinyonge. Jaribu bahati yako kila upatapo nafasi. Maisha ni haya haya hakuna mengine.
Hakuna sababu itakayokufanya ushindwe kupambania ndoto ya kufanikiwa. Sportpesa imetoa fursa katika bidhaa zake. Unaweza kucheza mechi za multibet, unaweza kucheza Jackpot, unaweza kucheza michezo ya kasino, ambapo sasa hivi kuna promosheni kubwa kuliko zote Tanzania ya Drop n Win. Upewe fursa gani tena?
Ni jukumu lako kuipigania ndoto yako na kuyabadilisha maisha yako na familia yako. Cheza leo ushinde na wewe uwe umejipata na SportPesa.