SportPesa inakidhi mahitaji yako yote ya ubashiri wa Soka.
Ligi Kuu ya Uingereza inashirikisha timu maarufu ulimwenguni. SportPesa inakuletea chaguo kubwa na odds nzuri zaidi kwa kila aina ya ubashiri.
Ligi Kuu ya Uingereza ni ligi maarufu zaidi ya mpira wa miguu ulimwenguni. Popote uendapo ulimwenguni, watu wanasikia juu ya timu kubwa kama Manchester United, Tottenham na Liverpool – hata watu ambao hawajawahi kwenda Uingereza au ambao si wapenzi wa mpira wa miguu! Vivyo hivyo, wachezaji wao ni nyota wa kimataifa, na wakati mwingine wake zao pia. Ukiwaangalia “Posh na Becks” ambao walipata umaarufu sana mwishoni mwa miaka ya 1990.
Lakini bila kujali yanayoendelea nje ya uwanja, yanayoendelea katikati ya uwanja namaanisha wakati mpira ukichezwa ndio yanayochochea Ligi Kuu kuwa kivutio cha ulimwengu. Mashabiki hufurahia kutazama na mamilioni kati yao huweka dau kwenye mechi za Ligi Kuu kila wiki.
Ubashiri wa Ligi Kuu ni maarufu nchini Tanzania kama ilivyo kila mahali ulimwenguni. SportPesa inakupa nafasi ya kuweka ubashiri wako katika mechi zinazoendelea kwenye ligi, tuna wachambuzi wazuri ambao huhakikisha wanatoa taarifa za uhakika kuhakikisha odds ni za ukweli na nzuri kulingana na wengine.
Ligi Kuu ya Uingereza.
Uingereza ni nchi yenye historia ndefu na urithi wa michezo ya kujivunia. Ni sehemu ambayo sheria za mpira wa miguu na namna inavyochezwa leo ziliwekwa kwa maandishi kupitia chama cha Soka kilichoundwa mnamo 1863. Wakati huo ndio ulipozaliwa mpira wa miguu. Watu walikuwa wanacheza mpira kwa muda mrefu, lakini kwa sheria mpya zilizowekwa, ziliweza kubadilisha michezo mingi.
Miaka 25 baadaye, mnamo 1888, Ligi ya Soka ya Uingereza iliundwa, na kwa zaidi ya karne moja ilikuwa ni kilele cha mpira wa miguu huko England. Mnamo 1992, hata hivyo, timu za daraja la juu zilikubaliana kujiuzulu kutoka ligi ya Uingereza ili kuunda Ligi Kuu. Hii ilikuwa kuzuia vizuizi vya utangazaji wa Runinga na kuwaruhusu kusaini mikataba mipya, na kupanua wigo la watazamaji ili kuongeza mapato yao.
Ligi ya Uingereza bado ipo hadi leo, na ndio ligi kongwe ya mpira wa miguu ulimwenguni, lakini haiwakilishi kilele cha mchezo huo. Badala yake, washindi huendelea kwenye ligi nyingine kubwa.
Mifumo ya ligi kuu na historia yake.
Wakati Ligi Kuu ya Uingereza ilipoanza, iliundwa na timu 22. Hizi ni pamoja na timu zenye majina makubwa ambayo ni maarufu leo kama ilivyokuwa karibu miaka 30 iliyopita, kama Manchester United, Arsenal na Chelsea. Lakini pia kulikuwa na timu nyingine ambazo zimeshuka daraja la juu, kama vile Oldham Athletic, au timu kama Wimbledon ambazo kwa sasa haziko tena.
Mnamo 1995, idadi ya timu ilipunguzwa hadi 20, ukilinganisha na ligi zingine za juu huko Uingereza, kwa kushusha daraja timu nne na kupandisha mbili. Tangu wakati huo, muundo na mfumo haujabadilika. Kupandisha na kushusha daraja timu tatu kila mwisho wa msimu.
Kila timu inacheza mara mbili kwa msimu, mara moja nyumbani na mara moja ugenini, kwa hivyo kila timu hucheza michezo 38. Alama tatu hutolewa kwa ushindi, na alama moja kwa sare. Mwisho wa msimu, timu iliyo na alama nyingi hutangazwa mshindi.
Timu maarufu na nyakati za kukumbukwa.
Chini ya miaka 30 ya kuwepo kwake, timu 49 zimecheza angalau msimu mmoja wa mpira wa miguu wa Ligi Kuu. Ni timu sita tu ambazo zimecheza kila msimu na hazijawahi kushushwa daraja – lakini sio sita unazofikiria. Manchester United, Tottenham, Liverpool, Arsenal na Chelsea zinajulikana. Lakini timu ya sita ni Everton. Manchester City wakiwa wameshushwa daraja mara mbili.
Leo, ni hadithi tofauti na Manchester City ndio timu ambayo kila mtu anataka kuifunga. Lakini unapoangalia historia yote ya Ubingwa, wapinzani wao Manchester United ndio wamefanikiwa zaidi.
Kwa kweli, kutawala kwa Mashetani Wekundu kwa miaka 20 ya kwanza ya Ligi Kuu kuliwaletea mashabiki wengi, ikiwa ni miaka nane imepita tangu ushindi wao wa mwisho, United wameshinda Ligi Kuu mara nyingi zaidi!
Ligi hiyo ni maarufu kwa timu zake “kubwa sita”. Pamoja na timu hizo mbili kutoka Manchester, pia kuna Liverpool na kisha timu tatu kubwa za London. Arsenal, Tottenham na Chelsea. Timu hizi sita zimeshinda mataji yote isipokuwa mawili ya Ligi Kuu. Mbali ya kwanza ilikuwa wakati Blackburn alishtua ulimwengu wa mpira wa soka mnamo 1995. Lakini mafanikio yao yalikuwa ya kawaida ikilinganishwa na matukio ya msimu wa 2015/16.
Kubashiri kwenye Ligi kuu.
Ikiwa kama unataka kubashiri ligi kuu SportPesa ni mahala sahihi pa kufanya hivyo kwa kuweka dau lako kila siku. Unaweza kubashiri timu moja iliyopo nyumbani , ugenini au sare.