- NBC Premier League leo mchezo mmoja mkubwa kuchezwa Singida, saa 10:00 jioni, Uwanja wa Airtel
- Singida Black Stars kuikabili Azam FC leo Aprili Mosi 2026.
- Ni mbinu za Kocha Mkuu Othmen Najjar wa Tunisia vs Florent Ibenge raia wa Dr Congo.
Singida Black Stars kuikabili Azam FC leo NBC Premier League. Wenyeji ngome yao ni Singida wanatumia Uwanja wa Airtel kwa mechi za nyumbani. Ipo chini ya Kocha Mkuu Othmen Najjar raia wa Tunisia mwenye miaka 41. Atapambana na Florent Ibenge wa Azam FC, raia wa DR Congo mwenye miaka 64.
SOMA HII:Singida Black Stars vs Azam FC NBC Premier League | H2H, msimamo, takwimu, utabiri
Je, bado hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa hivi
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Singida Black Stars kuikabili Azam FC leo kazi ipo

Singida Black Stars kuikabili Azam FC leo kazi ipo kutokana na uimara wat imu zote mbili. Wenyeji kwenye mechi 5 Machi, wamepoteza mbili zote wakiwa nyumbani. Je leo watakubali kupoteza mchezo wa 3?
Timu hiyo kwenye mechi kubwa mbili ilipoteza dhidi ya Yanga SC na Simba SC. Mechi 2 za ugenini ilipata ushindi na kuvuna pointi 6. Ikiwa nyumbani imeshinda mchezo mmoja kati ya mechi 3.
Maoni ya Kocha Mkuu Othmen Najjar

Kocha Mkuu Othmen Najjar amesema kuwa wachezaji wanazidi kuimarika. Kuelekea kwenye mchezo dhidi ya Azam FC anaamini watafanya vizuri. Ameongeza kuwa wanawaheshimu wapinzani lakini wanahitaji matokeo.
“Sio Azam FC peke yake hapana ila timu nyingi hapa Tanzania zinaonyesha viwango bora. Muda mwingine huja na matokeo ambayo hujatarajia. Kwa maana hiyo ni wazi mpira wa Tanzania umepiga hatua nzuri.
“Hakuna timu ndogo wala timu kubwa. Muhimu kwetu kufanya kile ambacho tumekifanya mazoezini ili kupata matokeo. Tumeanza kurudi hatua kwa hatua. Kipindi nilichokabidhiwa timu tulikuwa nafasi ya 13. Na sasa tunazidi kuwa bora tuna wachezaji wazuri ambao wanaweza kutupeleka katika hatua nzuri zaidi,”.
SOMA HII: Mtibwa Sugar 1-3 Singida Black Stars, KMC FC yapigwa na Azam FC/ Namungo FC vs Yanga SC lineups

Maoni ya Ibenge wa Azam FC

Kocha wa Azam FC, Florent Ibenge amesema mchezo wa leoni muhimu kupata pointi tatu. Kocha huyo mchezo uliopita ugenini alivuna pointi moja dhidi ya Mashujaa FC. Amebainisha kwamba wachezaji wanahitaji ushindi.
“Akili zetu kwa sasa kuelekea mchezo dhidi ya Singida Black Stars zinawaza ushindi. Tunajua itakuwa ni ngumu, tunataka kucheza soka safi dakika zote 90. Ni bahati kwa wachezaji na soka la Tanzania kuwa na aina hii ya mechi,”.
Msimamo wa NBC Premier League 2025/26
| POS | MP | W | D | L | PTS |
| 1.Yanga SC | 16 | 11 | 5 | 0 | 38 |
| 2.Simba SC | 14 | 9 | 4 | 1 | 31 |
| 3. Azam FC | 15 | 7 | 8 | 0 | 29 |
| 4. JKT Tanzania | 17 | 7 | 7 | 3 | 28 |
| 5.Pamba Jiji FC | 16 | 6 | 7 | 3 | 25 |
| 6.S. Black Stars | 15 | 7 | 4 | 4 | 25 |
| 7.M. Sugar | 17 | 5 | 7 | 5 | 22 |
| 8.Namungo FC | 17 | 5 | 6 | 6 | 21 |
| 9.Dodoma Jiji FC | 17 | 5 | 6 | 6 | 21 |
| 10.TRA United | 16 | 5 | 5 | 6 | 20 |
| 11.Mashujaa FC | 17 | 4 | 7 | 6 | 19 |
| 12.Fountain | 16 | 4 | 4 | 8 | 16 |
| 13.Coastal Union | 16 | 3 | 6 | 7 | 15 |
| 14.Mbeya City | 16 | 3 | 4 | 9 | 13 |
| 15.T. Prisons | 17 | 3 | 4 | 10 | 13 |
| 16. KMC FC | 16 | 2 | 2 | 12 | 8 |
SOMA HII: Singida Black Stars 1-2 Simba SC NBC Premier League/ Highlights, goal, standings

Hitimisho
Singida Black Stars kuikabili Azam FC leo NBC Premier League. Huu ni mchezo mkubwa ndani ya ligi namba 6 kwa ubora Afrika. Azam FC haijapoteza mchezo msimu huu je wenyeji wataivunja rekodi?

