AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika KusiniCAF Misri
  • Goli la Mohamed Salah laipeleka hatua ya 16 bora Misri ikiongoza kundi B na pointi 6
  • AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini hatua ya makundi nchini Morocco
  • Zambia 0-0 Comoros matokeo ya mchezo wa hatua ya makundi Desemba 26,2025

AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini ni matokeo rasmi mchezo wa makundi kwa kundi B. Mohamed Salah alifunga goli pekee la ushindi kwa mkwaju wa penalty dakika ya 45. Goli hilo linaipa tiketi Misri kutinga hatua ya mtoano. Licha ya Misri kuwa pungufu kwenye mchezo huo walipambana kuvuna pointi tatu muhimu.

SOMA HII: AFCON 2025 matokeo na ratiba hii hapa/ Msimamo, live scores

Hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini rekodi yaandikwa

AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini
Mohamed El Shenawy kipa wa Misri mchezaji wa mchezo dhidi ya Afrika Kusini.

Kwenye AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini rekodi imeandikwa kwa timu kutinga hatua ya 16 bora ikiwa pungufu. Mchezaji muhimu kwa kikosi cha Misri alionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 45 kipindi cha kwanza. Afrika Kusini mapambano yote kipindi cha pili hayakuleta matunda.

Ni Mohamed Hany alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano. Licha ya kadi hiyo dakika ya 45+2 bado goli la Salah lilidumu mpaka mwisho wa mchezo. Misri inatinga hatua ya 16 bora ikiwa inaongoza kundi B pointi zake ni 6.

SOMA HII: AFCON 2025 Match round 1: Hawa hapa washindi wa tuzo za mchezaji bora wa kila mechi

image

Mabadiliko katika mchezo

Misri

Salah Misri
Mohamed Salah mshambuliaji wa timu ya taifa ya Misri anayecheza Liverpool ya England.

Eman Ashour in 45 Omar Marmoush out
Mohamed Shehata in out Mahmoud Trezeguet dk 80

Afrika Kusini

Sipho Mbule in Thelenthe Mbatha out dk 45

Relebohile Ratomo in out Oswin Appollia dk 69

Evidence Makgopa in out Sphephelo Sithple dk 75

Elias Mokwana in out Tshepang Moremi dk 79

Kadi za njano

Dakika ya 20 Teboho Mokoena alionyeshwa kadi ya njano kwa Afrika Kusini.
Dakika ya 30 Mohamed Hany alionyeshwa kadi ya njano kwa Miari.
Dakika ya 43 Lyle Foster alionyeshwa kadi ya njano kwa Afrika Kusini
Dakika ya 43 Khuluso Mudau alionyeshwa kadi ya njano mwa Afrika Kusini.

Msimamo kundi B

 MPWDLPTS
1.Misri22006
2. A.Kusini21013
3.Zimbabwe20111
4.Angola20111

Safari ya Misri mpaka hatua ya 16 bora

Misri Afcon
Misri raundi ya 16 AFCON 2025.

Misri katika kundi B mchezo wa ufunguzi ilipata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Zimbabwe. Licha ya mchezo wa kwanza kutengeneza nafasi nyingi na kumiliki mpira kwa asilimia kubwa walifungwa goli mapema. Dakika ya 20 ni Prince Dube alifunga goli kwenye mchezo huo.

Misri waliweka usawa kupitia magoli ya Omar Marmoush dakika ya 64. Mohamed Salah alifunga goli la ushindi. Hivyo Misri walifanya Comeback kwenye mchezo wa ufunguzi wakivuna pointi tatu mazima.

SOMA HII: AFCON 2025 Matchday 1: stats, Mechi 12, Magoli 29

image

Matokeo ya mechi nyingine

Zambia 0-0 Comoros

Angola 1-1 Zimbabwe

Hitimisho

AFCON 2025 Misri 1-0 Afrika Kusini ni mchezo uliozua mjadala mkubwa hasa goli la ushindi. Penalti aliyofunga Mohamed Salah inatajwa kuwa na maajabu yake. Kocha Mkuu wa Afrika Kusini Hugo Broos ameweka wazi kuwa alishangazwa na adhabu hiyo iliyowapa ushindi Misri.

Share this: