Fei Toto maandalizi AFCONFei Toto maandalizi AFCON
  • Zikisalia siku 10 tu, joto la mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, linazidi kupanda.
  • Mashindano hayo yatafanyika nchini Morocco, ambapo yataanza kutimua vumbi Desemba 21, 2025.
  • Mchezo wa ufunguzi utakuwa kati ya Morocco vs Comoros.
  • Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kimeweka kambi Misri

Joto la mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, nchini Morocco linazidi kupanda. Zimesalia siku 10 kiwake, ambapo mashindano hayo yataanza Desemba 21, 2025. Katika mchezo wa ufunguzi wenyeji Morocco watakabiliana na Comoros.

SOMA HII PIA: TANZANIA KIBARUANI AFCON 2025, RATIBA HII HAPA

Bado hujashinda? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Mfumo wa mashindano ya AFCON 2025 Morocco

Vita ya wakubwa
Vita ya wakubwa

Ikumbukwe katika mashindano ya mwaka huu kunatarajiwa na makundi sita, kila Kundi linatarajiwa kuwa na timu nne. Namba ya timu zinazoshiriki AFCON iliongezwa kutoka timu 16 hadi 24 mnamo 2019, ili kuruhusu timu zaidi kufuzu, na muundo huo umeendelea kutumika. Timu mbili za juu kutoka kila kundi zitatinga hatua ya mtoano ya raundi ya 16, zikifuatiwa na timu nne zilizoshika nafasi ya tatu kwa viwango bora zaidi.

Hatua za mtoano zitachezwa kwa mechi moja moja. Kama mchezo utamalizika kwa sare, muda wa nyongeza utaongezwa ili kumpata mshindi. Ikiwa mshindi atashindwa kupatikana ndani ya muda wa nyongeza basi mikwaju ya penalti itatumika kuamua mshindi.

SOMA HII ZAIDI: TAIFA STARS HIYO AFCON 2025, MAMA AWAPA TANO

Ratiba ya viwanja vitakavyotumika

Uwanja wa Complex Sportif Prince Moulay Abdellah, uliopo katika mji mkuu, utakuwa mwenyeji wa fainali ya mashindano haya mnamo Januari 18. Ingawa uwanja huo utaandaa mechi ya kwanza na ya mwisho ya AFCON, ni mmoja tu kati ya viwanja vinne jijini Rabat vitakavyotumika. Viwanja vingine vitakavyotumika ni Pamoja na Complexe Sportif Prince Héritier Moulay El Hassan, Stade El Barid, na Stade Annexe Olympique Complex Sportif Prince Moulay Abdellah.

Rabat ni moja ya miji sita mwenyeji, huku mingine ikitumia uwanja mmoja tu. Casablanca (Stade Mohamed V) inafahamika sana kwa mashabiki wa soka barani Afrika. Hii ni kwa kuwa ndiyo nyumbani kwa vilabu maarufu vya Wydad na Raja.

Grand Stade de Tanger ndicho kiwanja kikubwa zaidi kinachotumika. Kiwanja hiki kina uwezo wa kubeba watazamaji 75,000. Mechi zingine zitachezewa Grand Stade de Marrakech, Complexe Sportif de FES, na Grand Stade d’Agadir.

Makundi na Timu

AFCON 2025
Timu ya Taifa-taifastars

Kundi A:

Morocco, Mali, Zambia, Comoros

Kundi B:

Misri, Afrika Kusini, Angola, Zimbabwe

Kundi C:

Nigeria, Tunisia, Uganda, Tanzania

Kundi D:

Senegal, DR Congo, Benin, Botswana

Kundi E:

Algeria, Burkina Faso, Guinea ya Ikweta, Sudan

Kundi F:

Ivory Coast, Cameroon, Gabon, Msumbiji

Taifa Stars yawasili Misri Kujiandaa na AFCON 2025

Kikosi cha Taifa Stars
Kikosi cha Taifa Stars

Kuelekea kuanza kwa mashindano hayo, timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imewasili jijini Cairo, Misri, kuanza rasmi maandalizi ya mwisho. Kikosi hicho, kinachoongozwa na kocha mkuu, Miguel Gamondi kilipokelewa vizuri na baadhi ya Watanzania waishio Misri. Sambamba na hao Walikuwepo baadhi ya maofisa wa ubalozi.

Taifa Stars imeweka kambi nchini Misri kwa lengo la kupata mazingira bora ya mazoezi. Mipango ya awali inaeleza kuwa kuna mahitaji ya mechi za kirafiki, zitakazowapa wachezaji nafasi ya kuongeza uimara wa kiufundi na kiakili kabla ya kuelekea Morocco. Kocha Gamondi amesema kambi hiyo ni muhimu kurekebisha makosa yalioonekana katika mechi za kufuzu na kuimarisha umoja wa kikosi.

SOMA HII PIA: Tanzania 2-1 Senegal CECAFA 2025 Arusha | Maandalizi ya CHAN yapamba moto

Hitimisho

Wachezaji wengi wa kimataifa, akiwemo nahodha Mbwana Samatta, walitarajia kujiunga na timu hiyo moja kwa moja kutoka vilabu vyao barani Ulaya na Asia. Wachezaji wa ligi ya ndani pia wameonyesha ushindani mkubwa katika mazoezi ya awali. Ikumbukwe Tanzania imepangwa Kundi C pamoja na Nigeria, Tunisia na Uganda, kundi linalotajwa kuwa gumu, lakini benchi la ufundi limeeleza kuwa wanakwenda kupambana bila woga.

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.