JKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26Nangu vs JKT Tz
  • JKT Tanzania 1-2 Simba SC matokeo ya mchezo wa NBC Premier League Novemba 8,2025 Uwanja wa Meja Isahmuyo.
  • Wilson Nangu ametwaa tuzo ya mchezaji bora mbele ya waajiri wake wa zamani.
  • Dimitar Pantev mchezo wa kwanza wa ligi baada ya kurithi mikoba ya Fadlu Davids.

JKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26 matokeo rasmi kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Meja Jeneral Isamuyo Novemba 8,2025. Wenyeji JKT Tanzania walitangulia kupata goli dakika ya 60 kupitia kwa Edward Songo likasawazishwa na Wilson Nangu dakika ya 64. Mnyama alichukua pointi tatu ugenini.

SOMA HII: Simba SC vs JKT Tanzania Novemba 8,2025

Vuna mamilioni sasa hivi na SportPesa

Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini.

image

JKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26 kazi ilikuwa nzito

JKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26
Beki wa Simba SC, Wilson Nangu kwenye mchezo wa ligi dhidi ya JKT Tanzania. Source: Simba SC.

Wakati matokeo yakiwaJKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26 kazi ilikuwa nzito kwa timu zote mbili. Mchezo huo dakika 45 za mwanzo hakukuwa na timu iliyopata goli. Simba SC walifanya majaribio mawili kupitia kwa Joshua Mutale na Kibu Dennis yaliokolewa na mlinda mlango wa JKT Tanzania Omar Gonzo.

Mlinda mlango wa Simba SC Yakoub Suleman aliokota nyavuni mpira dakika ya 60 uliokwamishwa na Songo. Iliwachukua Simba SC dakika 4 kuweka usawa kupitia  Nangu. Jonathan Sowah alianzia benchi kwenye mchezo huo alipachika bao la ushindi dakika ya 76 likipeleka pointi tatu unyamani.

Ni mchezo wa kwanza kwa Meneja Mkuu wa Simba SC Dimitar Pantev kwenye ligi baada ya kuchukua mikoba ya Fadlu Davids. Kwenye mchezo huo alianza na mshambuliaji mmoja Steven Mukwala. Mabadiliko ya kipindi cha pili alipoingia Abraham Morice, Jean Ahoua, Ellie Mpanzu na Jonathan Sowah yalibadilisha ari ya mchezo.

Tuzo ya mchezaji bora ameibeba beki Nangu

Nangu alichaguliwa kuwa mchezaji bora katika mchezo huo. Beki huyo alifunga goli la usawa kwa Simba SC dakika ya 64. Licha ya kufunga alifanya kazi kubwa katika kuhakisha timu inalinda ushindi.

Kazi nyingine ambayo alipewa ilikuwa ni kupiga faulo na kurusha mipira. Miongoni mwa faulo ambazo alipiga ilikuwa dakika ya 14, 15,16 kipindi cha kwanza. Alisajiliwa na Simba SC akitokea JKT Tanzania hivyo alifunga mbele ya waajiri wake wa zamani.

Nangu amesema: “Tulikuwa tunahitaji pointi tatu muhimu kwenye mchezo wetu. Sikupanga kushangilia nikifunga lakini ilitokea kwa kuwa sikutarajia. Mchezo ulikuwa mgumu tunamshukuru Mungu kupata pointi tatu muhimu,”.

SOMA HII: Mechi za Simba SC 2025/26 CAF Champions League, NBC Premier League

image

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Mukwala vs JKT Tanzania
Steven Mukwala mshambuliaji wa Simba SC dhidi ya JKT Tanzania. Source: Simba SC.

1.Simba SC  pointi 9, mechi 3

2.Pamba Jiji pointi 9, mechi 6

3.Mbeya City pointi 8, mechi 6

4.Mashujaa FC pointi 8, mechi 6

5.Yanga SC pointi 7, mechi 3

6.Singida Black Stars pointi 7 mechi 3

7.JKT Tanzania pointi 7, mechi 6.

Kikosi cha JKT Tanzania kilichoanza dhidi ya Simba SC

Gonzo

Wahabi

Msengi

Pascal

Roony

Sospeter Bajana

Hassan Nassoro

Kilemile

Najimu Mussa

Paul

Hassan Dilunga

Wachezaji wa akiba

Joseph

Kapalata

Gamba

Said Ndemla

Edward Songo

Makame

Elia

Salum

Abel

Kikosi cha Simba SC kilichoanza dhidi ya JKT Tanzania

Simba VS jkt
JKT Tanzania vs Simba SC uwanjani. Source: Simba SC.

Mlinda mlango

Yakoub Suleman

Mabeki

Shomari Kapombe

Athony Mligo

Wilson Nangu

Rushine De Reuck

Viungo

Yusuph Kagoma

Kibu Dennis

Naby Camara

Neo Maema

Joshua Mutale

Mshambuliaji

Steven Mukwala

Wachezaji wa akiba

Hussen Abel

Duchu

Chamou

Kante

Mzamiru Yassin

Ellie Mpanzu

Jonathan Sowah

Seleman Mwalimu

Jean Ahoua

Abraham Morice

SOMA HII: JKT Tanzania FC Vs Simba SC 5/5/2025 : Mabosi Simba wafanya kikao kizito cha Ubaya ubwela

image

Hitimisho

JKT Tanzania 1-2 Simba SC NBC Premier League 2025/26 pointi tatu zinaipeleka Simba SC kuongoza msimamo wa ligi. Songo anakuwa mchezaji wa kwanza kumfunga mnyama msimu wa 2025/26. Kwenye mechi mbili walizochezwa walikuw hawajaruhusu goli.

Share this: