- NBC Premier League msimu wa 2025/26 mechi zote za moto kutokana na ushindani uliopo.
- Simba SC vs JKT Tanzania Novemba 8,2025 itachezwa saa 1:00 usiku Uwanja wa Meja Isahmuyo.
- Wajeda niwagumu katika kupoteza mechi zao ndani ya ligi.
Simba SC vs JKT Tanzania ni ratiba ya mchezo ujao kwenye NBC Premier League. Saa 1:00 usiku itachezwa kwenye Uwanja wa Meja Jeneral Isahmuyo. Mara ya mwisho wababe hawa walipokutana hapo, mnyama alipata ushindi wa goli moja lililofungwa na Fabrince Ngoma.
SOMA HII: Mechi za Simba SC 2025/26 CAF Champions League, NBC Premier League ni moto| Matokeo na wafungaji
Unasubiri nini? Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini.

Simba SC vs JKT Tanzania utakuwa mchezo wa aina gani?

Mafahari wawili Simba SC vs JKT Tanzania wanapokutana huwa unakuwa mchezo wenye matumizi makubwa ya nguvu. Mnyama chini ya meneja Dimitar Pantev hupendelea mpira wa pasi nyingi. Wajeda chini ya Kocha Mkuu, Ahmed Ally wao hupendelea mpira wa kasi na kujilinda.
Katika msimamo JKT Tanzania ipo nafasi ya 5 bada ya mechi 5. Ushindi ni kwenye mechi moja na sare mechi 4. Hii inatoa taswira kuwa wapo imara katika eneo la ulinzi.
Upande wa Simba SC ni nafasi ya 7 pointi 6 baada ya mechi mbili. Katika eneo la ulinzi, haijaruhusu goli la kufungwa. Safu ya ushambuliaji imefunga magoli 6.
H2H
05/5/2025, JKT Tanzania 0-1 Simba SC
24/12/2024, Simba SC 1-0 JKT Tanzania
28/05/2024, Simba SC 2-0 JKT Tanzania
15/02/2024, JKT Tanzania 0-1 Simba SC
01/03/2021, Simba SC 3-0 JKT Tanzania
04/10/2020, JKT Tanzania 0-4 Simba SC
7/02/2020, Simba SC 0-1 JKT Tanzania
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC Septemba 16 Uwanja wa Mkapa | Takwimu, matokeo, H2H

Utabiri wa matokeo ya mchezo
Simba SC imekuwa na rekodi ya kupata matokeo inapokutana na JKT Tanzania. Katika mechi 7, wajeda walipata nafasi kufunga goli moja pekee. Nafasi kubwa ya ushindi anapewa mnyama.
Mechi 7 walizokutana, ushindi kwa JKT Tanzania ni mara moja. Mnyama alipata ushindi katika mechi 6. Magoli yalifungwa 13, katika hayo safu ya ushambuliaji ya Simba SC ilifunga magoli 12 na ile ya JKT Tanzania 1.
Licha ya kupewa nafasi kubwa ya kupata matokeo bado JKT Tanzania sio mpinzani mwepesi. Timu hiyo ni imara katika kujilinda kwenye mechi zake inazocheza. Dakika 90 zitaamua nani atavuna pointi tatu.
Kikosi cha JKT Tanzania kinachotarajiwa kuanza vs Simba SC

Ramadhani Chalamanda, Hassan Dilunga, Abdulahim Bausi, Mohamed Bakari, David Bryson, Salehe Karabanka, Laurian Makame, Salum Khamis, Pascal Mussa, Ally Msengi na Paul Peter.
Mlinda mlango
Yakoub Suleman
Mabeki
Chamou
Mligo
David Kameta
De Reuck
Viungo
Yusuph Kagoma
Joshua Mutale
Ellie Mpanzu
Morice Abraham
Jean Ahoua
Mshambuliaji
Jonathan Sowah
Matokeo ya mechi 5 zilizopita JKT Tanzania kwenye ligi
Oktoba 24,2025 Mbeya City 2-2 JKT Tanzania
Oktoba 19,2025, JKT Tanzania 1-1 Namungo FC
Oktoba Mosi, JKT Tanzania 1-1 Azam FC
Septemba 22,2025 Coastal Union 1-2 JKT Tanzania
Septemba 18,2925, Mashuja FC 1-1 JKT Tanzania

Matokeo ya mechi 5 zilizopita Simba SC

Oktoba 26,2025 Simba SC 0-0 Nsingizini Hotspurs. Ligi ya Mabingwa Afrika.
Nsingizini Hotspurs 0- 3 Simba SC, Oktoba 19,2025. Ligi ya Mabingwa Afrika.
Oktoba Mosi 2025, Simba SC 3-0 Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Septemba 28 2025, Simba SC 1-1 Gaborone United, Ligi ya Mabingwa Afrika.
Septemba 25 2025, Simba SC 3-0 Fountain Gate mchezo wa Ligi Kuu Bara.
Hitimisho
Simba SC vs JKT Tanzania ni mchezo unaotarajiwa kutokuwa na magoli mengi kutokana na aina ya mbinu za wapinzani. JKT Tanzania wamekuwa wakijilinda huku Simba SC wakishambulia kwa kushtukiza. Licha ya mnyama kuwa na rekodi yakupata ushindi wa magoli 4-0 bado mchezo unatarajiwa kuwa mgumu kwa timu zote mbili.

