- Yanga SC 0-1 Silver Strikers CAF Champions League ushindi wa kwanza kwa wenyeji kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Bingu-Malawi.
- Goli la kwanza limefungwa na Andulu Yosefe aliyekuwa ndani ya 18 kwa kumchagulia upande uliomshinda Djigui Diarra.
- Yanga SC wanakibarua cha kupata ushindi wa angalau magoli 2-0 mchezo ujao Uwanja wa Mkapa, Oktoba 25.
Yanga SC 0-1 Silver Strikers CAF Champions League ni matokeo rasmi katika mchezo wa kwanza, Uwanja wa Bingu. Goli la ushindi limefungwa dakika ya 76 na Andulu Yosefe. Unakuwa ni ushindi wanne kwa Silver Strikers wakiwa nyumbani hivyo wamendeleza ubabe wao. Bado mchezo mmoja wa maamuzi utakaochezwa Uwanja wa Mkapa, Oktoba 25 na Yanga SC wakitakiwa kupata ushindi wa angalau magoli 2-0 ili kutinga hatua ya makundi.
SOMA HII: Yanga SC vs Silver Strikers CAF Champions League 2025| Lineup, H2H
Unasubiri nini? Vuna mamilioni sasa hivi
Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini.

Yanga SC 0-1 Silver Strikers CAF Champions League goli limefungwaje?

Yanga SC 0-1 Silver Strikers CAF Champions League goli lilifungwa kipindi cha pili. Katika dakika 45 za mwanzo hakukuwa na timu iliyoona lango la mpinzani. Wenyeji walilazimika kusubiri mpaka dakika ya 76 kupata goli la kuongoza.
Mpira ulianza kwa mlinda Chikoka George aliyepiga pasi ndefu. Uchizi vunga aliweka pasi ya kupenyeza ndani ya 18 ikapenya kwa walinzi wa Yanga SC. Ernest alitoa pasi ya goli kwa Andulu Yosefe ambaye aliwaadhibu Yanga SC kwa kumfunga mlinda mlango namba moja Djigui Diarra.
Kikosi cha Yanga SC dhidi ya Silver Strikers
Kipa
Djigui Diarra
Mabeki
Israel Mwenda
Boka
Dickson Job
Ibrahim Bacca
Viungo
Maxi Nzengeli
Mudathir Yahya
Mo Doumbia
Pacome
Aziz
Mshambuliaji
Boyeli
Wachezaji wa akiba
Mshery
Nondo
Zimbwe
Duke
Ecua
Balla
Edmund
Dube
SOMA HII: Yanga SC vs Silver Strikers CAF Champions League | H2H, takwimu muhimu, utabiri

Mechi 6 za Yanga SC zilizopita

Septemba 16, 2025 – Yanga SC 1-0 Simba SC, (Ngao ya Jamii).
Septemba 19, 2025 – Wiliete 0-3 Yanga SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika
Septemba 24,2025 – Yanga SC 3-0 Pamba Jiji, (Ligi ya NBC).
Oktoba 27,2025 -Yanga 2-0 Wiliete SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika).
Septemba 30,2025, Mbeya City 0-0 Yanga SC, (Ligi ya NBC).
Oktoba 18, 2025, Silver Strikers 1-0 Yanga SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika)
Mechi 6 za Silver Strikers zilizopita

Shire FC 1-4 Silver Strikers, Septemba 11 2025 Malawi Cup
Elgeco Plus 1-1 Silver Strikers, Septemba 21 2025, Ligi ya Mabingwa Afrika.
Silver Strikers 0-0 Elgeco Plus Septemba 27 2025, Ligi ya Mabingwa Afrika.
Blue Eagles 0-3 Silver Strikers Oktoba 2 2025, Malawi Cup.
Bullets 2-1 Silver Strikers Oktoba 5 2025, Malawi Cup.
Oktoba 18, 2025, Silver Strikers 1-0 Yanga SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika)
SOMA HII: Matokeo ya Yanga SC 2025/26 | Wafungaji, magoli, ratiba ya mechi zijazo

H2H
Silver Strikers FC 1-0 Yanga SC CAF Champions League, Oktoba 18, 2025 Uwanja wa Bingu, Malawi.
Yanga SC vs Silver Strikers FC, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Oktoba 25, 2025.
Mchezo wa kwanza Yanga SC kupoteza
Huu unakuwa ni mchezo wa kwanza Yanga SC kupoteza msimu wa 2025/26. Chini ya Kocha Mkuu, Romain Folz katika mechi sita zilizopita haikupoteza. Joto ya kupoteza Romain anaipata leo ugenini katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Hitimisho
Yanga SC 0-1 Silver Strikers CAF Champions League matokeo ya raundi ya kwanza. Mchezo wa pili utaamua mshindi wa jumla atakayekata tiketi hatua ya makundi. Je nani atatinga hatua inayofuata?

