- Kwa mara ya kwanza Wananchi chini ya Kocha Mkuu, Romain Folz wameangusha pointi ugenini.
- Yanga SC 0-0 Mbeya City NBC Premier League dakika 90 za ushindani kwa wababe wawili uwanjani.
- Kibarua cha Folz kigumu kutokana na mwendo wa timu hiyo katika mechi za ushindani.
Yanga SC 0-0 Mbeya City matokeo haya yanaongeza ugumu kibarua cha Kocha Mkuu wa Jangwani Romain Folz kusalia hapo. Tetesi zinaeleza kuwa kuna uwezekano mkubwa kocha huyo ataondoka hivi karibuni. Licha ya kutopoteza mchezo hata mmoja kati ya sita ambayo alikaa benchi baada ya kutambulishwa Yanga SC inaelezzwa mwenendo wake bado haujaeleka kwa mabingwa hao watetezi.
SOMA HII: Yanga SC vs Mbeya City Septemba 30 | H2H, vikosi, takwimu muhimu
Shinda mamilioni sasa hivi ukipaisha Kindege cha SportPesa

Ni muda wa kushinda milioni sasa hivi ikiwa utapaisha Kindege cha SportPesa. Unachotakiwa kufanya ni rahisi sana paa hewani. Cheza Aviator upate mgao wako.
Yanga SC 0-0 Mbeya City ziliongezwa dakika 9

Katika mchezo wa leo Yanga SC 0-0 Mbeya City ziliongezwa jumla ya dakika 9. Katika kipindi cha kwa kwanza ziliongezwa 3 na kipindi cha pili ziliongezwa 6. Licha ya dakika hizo kuongezwa bado milango ilikuwa migumu kwa timu zote.
Romain Folz kibarua chake kigumu
Taarifa zinaelezwa kuwa mabosi wa Yanga SC hawafurahishwi na mwendo wa timu. Katika mechi sita ambazo Folz alikuwa benchi inatajwa kuwa hakukuwa na utulivu kwa wachezaji. Licha ya kwamba kocha ni mgeni kuna fukuto ndani.
Folz wakati wa maandalizi ya mchezo dhidi ya Mbeya City alibainisha kuwa anaheshimu maoni. Kocha huyo aliongeza kuwa anahitaji muda zaidi kuwa na kikosi bora. Mchezo dhidi ya Mbeya City ulikuwa unatajwa kuwa ni wa mwisho kwake. Mchezo wake uliopita ilikuwa dhidi ya Wiliete SC.

“Nadhani tuna kikosi bora sana na kwa sasa tunapambana kufika kwenye ubora wa juu. Ni sawa watu kutoa maoni lakini sisi kama klabu ni lazima tuwe kitu kimoja nyakati hizi tunaposuka kitu kizuri kwa ajili ya timu yetu. Nadhani ndani ya kipindi kifupi kijacho tutakuwa sehemu nzuri sana,” alisema Folz.
SOMA HII: Romain Folz kocha mpya Yanga SC mwenye CV kubwa | Wachezaji wenye uhakika 2025/26

Mechi 6 za Yanga SC vs Mbeya City za ligi
| 13/02/2021 | Mbeya City 1-1 Yanga SC |
| 05/02/2022 | Yanga SC 0-0 Mbeya City |
| 25/06/2022 | Mbeya City 1-1 Yanga SC |
| 26/11/2022 | Yanga SC 2-0 Mbeya City |
| 6/6/2023 | Mbeya City 3-3 Yanga SC |
| 30/09/2025 | Mbeya City 0-0 Yanga SC |
Sare 5 ushindi mechi 1
Mbeya City wamekuwa na rekodi nzuri katika uwanja wa nyumbani. Kwenye mechi 6 ambazo walikutana na Yanga SC walipata sare 5. Mchezo mmoja walipoteza wakiwa ugenini.Katika sare tano, nne Mbeya City walikuwa nyumbani.
Kikosi cha Yanga SC kilichoanza dhidi ya Mbeya City
Mlinda mlango
Djigui Diarra
Mabeki
Dickson Job
Chadrack Boka
Israel Mwenda
Ibrahim Bacca
Viungo
Aziz Andambilwe
Maxi Nzengeli
Duke Abuya
Mohamed Doumbia
Pacome Zouzoua
Mshambuliaji
Andy Boyel
Wachezaji wa akiba

Balla Conte
Lassine Kouma
Abutwalib Mshery
Ecua Elastin
Mohamed Hussen
Edmund John
Prince Dube
Offen Chikola
Abdulanassir Abdallah
Abubakar Othman
SOMA HII: Usajili wa Yanga SC orodha ya wapya 11 msimu wa 2025/26 | Rekodi, magoli na timu walizotoka

Kikosi cha Mbeya City kilichoanza dhidi ya Yanga SC
Mlinda mlango
Beno Kakolanya
Walinzi
Ibrahim Ame
Yahya Mbegu
Mwani Thobias
Gabriel Mwaipola
Viungo
Omary Chibada
Baraka Filemon
Adilly Buha
Matheo Anthony
Washambuliaji
Vitalisy Mayanga
Eliud Ambokile
Wachezaji wa akiba
Peter Mwalyanzi
Pillar Kelvin
David Mwasa
Stewart Theodory
Daniel Lukandamila
Mukrim Juma
Jonathan Mwaibindi
Riphat Khamis
Malack Joseph
Hashimu Mussa
Hitimisho
Yanga SC 0-0 Mbeya City hii ni sare ya kwanza kwa mabingwa watetezi. Wapinzani hawa katika mechi zao zote wanazokutana huonyeshana ubabe kwelikweli. Katika mchezo wa leo kulikuwa na matumzi makubwa ya nguvu na spidi ndani ya dakika 90 na mwamuzi wa kati alikuwa ni Omary Mdoe.


