Mo DoumbiaMo Doumbia
  • Mchezo wa mwisho wababe hawa kucheza Uwanja wa Sokoine ubao ulisoma Mbeya City 3-3 Yanga SC.
  • Yanga SC vs Mbeya City burudani ya soka inakwenda kushuhudiwa katika dakika 90 ndani ya NBC.
  • Romain Folz Kocha Mkuu wa Yanga SC na Malale Hamsini Kocha Mkuu wa Mbeya City wapigiana hesabu kali.

Yanga SC vs Mbeya City mchezo mkali wa ligi ya NBC utakaopigwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Matokeo ya  2022/23 wakati Mbeya City inashuka daraja yalikuwa yakushangaza. Ubao ulisoma Mbeya City 3-3 Yanga SC wakigawana pointi mojamoja. Huu unakuwa mchezo wa kwanza baada ya Mbeya City kurejea kwenye ligi ya NBC.  

SOMA HII: SportPesa yaipa Yanga SC Bilioni 21.7 kupitia Ofa kubwa ya kihistoria

Paisha Kindege cha SportPesa uvune mamilioni

Muda wa kupaisha Kindege cha SportPesa uvune mamilioni. Rahisi sana na hakuna longolongo kwenye hili. Cheza Aviator sasa upate mgao wako.

image

  Yanga SC vs Mbeya City H2H

Yanga SC vs Mbeya City
Zimbwe Jr beki wa Yanga SC kwenye maandalizi ya mechi za ligi. Source: Yanga SC.

Yanga SC vs Mbeya City zipo rekodi zao mechi tano zilizopita ndani ya NBC. Ikumbukwe kwamba msimu wa 2022/23 Mbeya City ilishuka daraja. Imerejea ndani ya ligi kwa mara nyingine 2025/26.

13/02/2021Mbeya City 1-1 Yanga SC
05/02/2022Yanga SC 0-0 Mbeya City
25/06/2022Mbeya City 1-1 Yanga SC
26/11/2022Yanga SC 2-0 Mbeya City
6/6/2023Mbeya City 3-3 Yanga SC  

Mbeya City wakiwa nyumbani wagumu

Mechi 5 sare 4. Katika hizo 3 Mbeya City walikuwa nyumbani na moja ugenini. Yanga SC wamekuwa imara kupata matokeo mbele ya Mbeya City wakiwa nyumbani.

Mechi tano za Mbeya City za hivi karibuni

Beno Kakolanya
Beno Kakolanya, kipa namba moja wa Mbeya City 2025/26. Source: Mbeya City.

Fountain Gate 0-1 Mbeya City, ligi.

Azam FC 2-0 Mbeya City, ligi.

Mbeya City 1-1 Namungo FC, mchezo wa kirafiki.

Mtibwa Sugar 1-0 Mbeya City, mchezo wa kirafiki.

Mbeya City 0-2 Azam FC, mchezo wa kirafiki.

Safu ya ushambuliaji ya Mbeya City inaonekana haijawa imara. Katika mechi 5 ni magoli 2 ilifunga. Safu ya ulinzi imeruhusu magoli 6.

SOMA HII: Young Africans SC vs Wiliete SC CAFCL 27 Sept 2025: live score, Takwimu, vikosi, H2H, Utabiri

image

Mechi tano za Yanga SC hivi karibuni

Yanga 1-0 Bandari ya Kenya, (mechi ya kirafiki).

Yanga SC 1-0 Simba SC, (Ngao ya Jamii).
Wiliete 0-3 Yanga SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika).
Yanga SC 3-0 Pamba Jiji, (Ligi ya NBC).
Yanga 2-0 Wiliete SC, (Ligi ya Mabingwa Afrika).

Yanga SC imekuwa imara kwenye eneo la ushambuliaji. Katika mechi tano imefunga jumla ya magoli 10. Safu ya ulinzi haijaruhusu goli ndani ya uwanja.

Kikosi cha Yanga SC kinachotarajiwa dhidi ya Mbeya City

Pacome Master
Pacome kiungo mshambuliaji wa Yanga SC. Source: Yanga SC.

Mlinda mlango

Djigui Diarra

Mabeki

Kibwana Shomari

 Ladack Boka

Bakari Nondo

Ibrahim Bacca

Viungo

 Aziz Andambilwe

 Maxi Nzengeli

 Duke Abuya

Mudathir Yahya

 Pacome Zouzoua

Mshambuliaji

Andy Boyel

SOMA HII: Yanga SC inawadai Simba SC 2024/25

image

Kikosi cha Mbeya City kinachotarajiwa kuanza dhidi ya Yanga SC

Mlinda mlango

Beno Kakolanya

Walinzi

Ibrahim Ame

David Mwasa

Kelvin Kingu

Viungo

Yahya Mbegu

Habib Kyombo

 Omary Chibada

 Radilly Buha

Matheo Anthony

Washambuliaji

Vitalisy Mayanga

Riphat Msuya

Malale Hamsini Kocha wa Mbeya City kuhusu mchezo

“Utakuwa ni mchezo mgumu kwa kuwa tunakutana na mabingwa watetezi uwanjani. Tunamshukuru Mungu tupo salama baada ya kutoka Dar kwenye mchezo dhidi ya Azam FC. Maadalizi kiujumla yapo vizuri na tunaamini tutapata matokeo kwenye mchezo wetu.

Romain Folz Kocha Mkuu wa Yanga SC kuhusu mchezo

“Tunazidi kuimarika taratibu kutokana na mechi ambazo tunacheza. Ninaona kuna maoni ambayo yanatolewa hilo ni jambo zuri wachezaji wanazidi kuwa imara. Mchezo wetu ujao ni muhimu ambacho tunahitaji ni kupata matokeo mazuri,”.

Hitimisho

Yanga SC vs Mbeya City saa 10:00 jioni wanaume watakuwa uwanjani. Utakuwa ni mchezo wa tatu kwa wenyeji Mbeya City ukiwa wapili kwa Yanga SC. Kutokana na Yanga SC kuwa katika mwendelezo wa ushindi anapewa nafasi kubwa kupata matokeo katika mchezo huo.

image




Share this: