Aziz AAziz A
  • Matokeo ya Yanga SC ni kicheko kwa mashabiki kutokana na mwendo ambao wanakwenda nao kwenye mechi za ushindani.
  • Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League, Waangola wabebeshwa zigo la magoli 5-0 kimataifa
  • Romain Folz mbinu zimejibu huku tetesi zikieleza kuwa kocha huyo atafungashiwa virago vyake hivi karibu

Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League ni ushindi wa pili mfululizo kwenye mashindano makubwa Afrika. Wananchi wanasonga mbele hatua ya pili Ligi ya Mabingwa Afrika,(CAF). Baada ya kufuzu watakutana na Silver Strikers ya Malawi katika hatua inayofuata anga la kimataifa.

Paisha Kindege cha SportPesa upate mamilioni sasa hivi

image

Ni muda wakupaisha Kindege cha SportPesa sasa hivi upate mamilioni. Inawezekana kwako rubani bila shida hata kidogo. Cheza sasa Aviator upate mgao wako haraka.

Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League magoli

Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League
Pacome Zouzoua alifungua akaunti ya magoli anga la kimataifa Uwanja wa Mkapa. Source: Yanga SC.

Septemba 27 2025 Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League nyota wawili walifunga. Goli la kwanza lilifungwa na Pacome Zozuzoa dakika ya 70 akitumia pasi ya Andy Boyel. Goli la pili lilifungwa na Aziz Andambwile dakika ya 85 kwa pasi ya Offen Chikola.

Soma hii: Young Africans SC vs Wiliete SC CAFCL 27 Sept 2025: live score, Takwimu, vikosi, H2H, Utabiri

 Magoli 2-0 waliyopata Yanga SC mbele ya Waangola Uwanja wa Mkapa Septemba 27 2025 yanawapeleka hatua inayofuata. Katika hatua ijayo watakutana na Silver Strikers ya Malawi. Wababe hawa wawili watakutana katika kuwania kufuzu hatua ya makundi.

Namna Yanga SC ilivyotinga hatua ya pili CAF

Matokeo yaliyopita
Matokeo ya Yanga SC mchezo wa ugenini kimataifa. Source: Yanga SC.

Yanga SC ya Tanzania imefuzu hatua ya pili kwa ushindi wa jumla ya mabao 5-0. Mchezo wa ugenini ilipata ushindi wa mabao 3-0 na nyumbani ikawa ni mabao 2-0. Ndani ya dakika 180 kimataifa hawajaruhusu kufungwa Yanga SC.

Soma hii: Wiliete SC 0-3 Yanga SC Caf Champions League 2025

Katika mechi zote mbili Yanga SC ilikuwa na mbinu tofautitofauti. Kwenye mchezo wa ugenini walipata goli la ufunguzi kipindi cha kwanza. Mchezo wa pili Uwanja wa Mkapa walipata goli la ufunguzi kipindi cha pili.

Aziz Andambwile huyu alifungua ukurasa wa mabao ugenini. Alipopata nafasi ya kuanza Uwanja wa Mkapa alifunga pia. Katika mchezo wa pili ni Pacome alifungua ukurasa wa magoli.

Silver Striker itakayokutana na Yanga SC imefuzu hatua hiyo kwa kuwafungashia virago Elgeco Plus ya Madagascar. Ni faida ya bao la ugenini imewapa tiketi kutinga hatua ya pili. Mchezo wa kwanza ilikuwa Elgeco Plus 1-1 Silver Striker na mchezo wa pili nchini Malawi ilikuwa 0-0 Septemba 27 2025.

Mchezo ujao kimataifa Yanga SC

Katika hatua ya pili Ligi ya Mabingwa Afrika mchezo wa kwanza unatarajiwa kuchezwa kati ya Oktoba 17-19 nchini Malawi. Mchezo wa marudio unatarajiwa kuchezwa kati ya Oktoba 24-29 Uwanja wa Mkapa. Mshindi kwenye mchezo atatinga hatua ya makundi.

Mbinu za Romain Folz zimejibu

Mbali na kutofungwa kimataifa katika mechi tano mfululizo ambazo wamecheza Yanga SC hawajaruhusu bao la kufungwa. Mbinu za Kocha Mkuu Romain Folz zimejibu licha ya tetesi kueleza kuwa huenda akaondoka ndani ya timu hiyo. Sababu inatajwa timu hiyo kutocheza katika kiwango kinachovutia.

Wiliete SC vs Yanga SC
Romain Folz Kocha Mkuu wa Yanga SC 2025/26. Source: Yanga SC.

Soma hii: Yanga SC 3-0 Pamba Jiji FC

Mechi tano za Yanga SC chini ya Kocha Romain Folz

MchezoAina ya mashindano
Yanga 1-0 Bandari ya KenyaMechi ya kirafiki, Yanga Day
Yanga SC 1-0 Simba SC

Ngao ya Jamii
Wiliete 0-3 Yanga SCLigi ya Mabingwa Afrika
Yanga SC 3-0 Pamba JijiLigi ya NBC
Yanga 2-0 Wiliete SCLigi ya Mabingwa Afrika


Hitimisho

Yanga SC 2-0 Wiliete SC CAF Champion League dakika 90 zilizokuwa na ushindani mkubwa. Wiliete walifanya jaribio moja la hatari kupitia kwa Junior liligonga mwamba. Wazawa wamekuwa katika ubora kimataifa wakiongozwa na Aziz ambaye kafunga jumla ya magoli mawili.

image










Share this: