- Azam FC yafikisha unbeaten mechi 18 msimu wa 2025/26
- Mbeya City FC 0-0 Azam FC NBC Premier League, Tanzania Kwaraa, Manyara
- Matokeo na msimamo wa hivi punde tumekosogezea hapa
Mbeya City FC 0-0 Azam FC NBC Premier League, Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara. Matajiri wa Dar wameangusha pointi mbili. Ilikuwa ni vita kujinasua kutoka hatari ya kushuka daraja na vita yakupanda nafasi ya pili.
SOMA HII: Mzizima Dabi yaiachia maumivu Simba SC 2025/26 | Highlights, msimamo, h2h, ratiba mechi zijazo
Vuna mamilioni sasa hivi ukipaisha Kindege cha SportPesa
Ni sasa hivi unavuna mamilioni ukipaisha Kindege cha SportPesa. Ni rahisi sana hasa ukizingatia Marubani wapo makini. Cheza Aviator upate mgao wako.

Mbeya City FC 0-0 Azam FC NBC Premier League

Dakika 90 zimekamilika ubao umesoma Mbeya City FC 0-0 Azam FC. Matajiri wanaendelea kudunda na rekodi yakutofungwa. Huu ni mchezo wa 18 haijapoteza.
Ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi 34. Ushindi ni mechi 8 na imepata sare 10. Mbeya City baada ya mechi 18 ushindi ni mechi 4, sare 5 ikipoteza mechi 9.
SOMA HII: Azam FC 0-0 Yanga SC Dar Derby/ Highlights, standings, statics

Takwimu mchezo Mbeya City FC 0-0 Azam FC
| Mbeya City FC | Azam FC | |
| 3 | Mashuti | 9 |
| 1 | Lenga lango | 0 |
| 42% | Umiliki | 58% |
| 2 | Mashuti yasiyolenga lango | 9 |
| 0 | Kadi nyekundu | 0 |
| 3 | Kadi ya njano | 1 |
| 1 | Kona | 7 |
| 0 | Magoli | 0 |
Wachezaji walioonyeshwa kadi

Hijjah Lidah dakika ya 54, Riphat Msuya dakika ya 75, Hashimu Mussa dakika ya 81 kwa Mbeya City FC. Pascal Msindo dakika ya 45+3 wa Azam FC. Hakuna kadi nyekundu iliyotolewa.
Msimamo wa NBC Premier League 2025/26
Msimamo wa NBC Premier League uliobereshwa hivi punde. Mbeya City FC nafasi ya 12 pointi 17. Azam FC nafasi ya 3 pointi 34.
| POS | MP | W | D | L | PTS |
| Yanga SC | 18 | 13 | 5 | 0 | 44 |
| Simba SC | 17 | 10 | 6 | 1 | 36 |
| 3. Azam FC | 18 | 8 | 10 | 0 | 34 |
| 4. JKT Tanzania | 18 | 7 | 8 | 3 | 29 |
| 5.Singida Black Stars | 18 | 8 | 4 | 6 | 28 |
| 6.Pamba Jiji FC | 18 | 6 | 8 | 4 | 26 |
| 7.TRA United | 18 | 6 | 6 | 6 | 24 |
| 8. Dodoma Jiji FC | 18 | 6 | 6 | 6 | 24 |
| 9.Mtibwa Sugar | 18 | 5 | 8 | 5 | 23 |
| 10.Namungo FC | 18 | 5 | 7 | 6 | 22 |
| 11.Mashujaa FC | 18 | 4 | 8 | 6 | 20 |
| 12.Mbeya City | 18 | 4 | 5 | 9 | 17 |
| 13.Coastal Union | 18 | 3 | 7 | 8 | 16 |
| 14.Fountain Gate | 17 | 4 | 4 | 9 | 16 |
| 15.Tanzania Prisons | 18 | 3 | 4 | 11 | 13 |
| 16. KMC FC | 18 | 2 | 2 | 14 | 8 |
SOMA HII: Azam FC 2025: Mwongozo Kamili Kuhusu Kikosi, Benchi la Ufundi, na Urithi wa Klabu
Hitimisho
Mbeya City FC 0-0 Azam FC matokeo rasmi NBC Premier League 2025/26. Matajiri wanagawana pointi moja ugenini. Inakuwa ni timu ya pili ambayo haijapoteza mchezo kwenye ligi kama Yanga SC.

