- Pacome Zouzoua hatma yake kujulikana leo kutokana na kuumia kwenye mchezo wa CAF Champions League
- Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya kutoka Zanzibar ikitajwa kuwa dabi ngumu
- Steve Barker Kocha Mkuu wa Simba SC kwenye mtihani mzito dhidi ya Pedro Goncalves wa Yanga SC
- Taarifa kuhusu vikosi na presha kwa mnyama Simba SC tumekosegezea hapa
Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya kutoka Zanzibar zinaeleza wageni wapo kwenye presha. Ni leo Machi Mosi 2026, Uwanja wa New Amaan Complex unaobeba mashabiki 15,000. Pedro Goncalves Kocha Mkuu wa Jangwani amebainisha Pacome Zouzoua hatma yake itafahamika leo. Steve Barker, Kocha Mkuu wa Simba SC amesema wataingia kwa tahadhari.
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC: Pacome ashtua, msimamo, Ratiba, Moto utawaka Kariakoo Dabi ya ‘Damaro Day’
Cheza na ushinde sasa na ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni muda huu
Bado hujashinda na kindege cha SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kupitia Kampuni bora ya michezo ya kubashiri ya SportPesa bonyeza picha hii chini.

Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya kutoka Zanzibar, mnyama presha

Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya kutoka Zanzibar zinabainisha wageni wana presha. Ni mnyama Simba SC kutokana na kufungwa katika mechi sita mfululizo za NBC Premier League. Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC aliweka wazi suala hilo.
“Tunakabiliwa na presha kubwa ya mchezo na sisi Simba SC tuna msongo wa mawazo. Kutokana na matokeo mabaya ambayo tulikuwa nayo katika mechi zetu zilizopita.
“Licha ya hayo tupo tayari hii ni mechi mpya ni mechi ambayo tumejipanga kwenda kupata matokeo mazuri.Haitakuwa rahisi hata kidogo lakini tupo tayari,”.
SOMA HII: Yanga SC 1-0 Simba SC: Highlights, magoli yote, h2h – Ngao ya jamii 2025

Matokeo ya mechi zilizopita

Namungo FC 0-1 Yanga SC
Yanga SC 5-0 JKT Tanzania
Tanzania Prisons 0-2 Simba SC
Dodoma Jiji FC 0-0 Simba SC
Ali Kamwe afichua siri ya kambi
Ali Kamwe, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Yanga SC amefichua siri kwa kubainisha kuwa wamefuta matokeo yote yaliyopita.
“Tulipata ushindi kwenye mechi zilizopita hilo lipo wazi.Huu ni mchezo mpya na wachezaji wanajua kwamba wana deni kuelekea mchezo mpya kutafuta ushindi mbele ya timu bora,”.
Rekodi za mechi 10
Msimu wa 2025/26 baada ya mechi 10, Yanga SC haijapoteza. Inakutana na Simba SC iliyocheza mechi 10 ikipoteza mchezo mmoja dhidi ya Azam FC. Ingawa wenyeji wanapewa nafasi kupata ushindi dakika 90 zitakuwa na majibu kamili.
Msimamo Yanga SC vs Simba SC
| MP | W | D | L | PTS | |
| Yanga SC | 10 | 9 | 1 | 0 | 28 |
| 3. Simba SC | 10 | 7 | 2 | 1 | 23 |
Yanga SC vs Simba SC kikosi cha wenyeji
Langoni
Djigui Diarra
Mabeki
Israel Mwenda
Mohamed Hussen
Dickson Job
Ibrahim Bacca
Viungo
Damaro
Maxi Nzengeli
Duke Abuya
Pacome
Okello
Mshambuliaji
Depu
Kocha Mkuu ni Pedro Goncalves, raia wa Ureno
Kikosi cha Simba SC kinachotarajiwa kuanza

Langoni
Kassali
Mabeki
Shomari Kapombe
Kibabage
Rushine
Toure
Viungo
Yusuph Kagoma
Gueye
Loemba
Clatous Chama
Oura
Mshambuliaji
Seleman Mwalimu
Kocha Mkuu ni Steve Barker, raia wa Afrika Kusini
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC joto linazidi kupanda/ Ratiba, msimamo
Hitimisho
Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya zinaeleza kuwa kila timu imechukua tahadhari kubwa kabla ya mchezo. Mwamuzi wa kati wa mchezo ni Nassoro Mwinchui kutoka Tanga atasimamia sheria 17 za mchezo. Dakika 90 zitaamua nani atavuna pointi tatu ama watagawana pointi mojamoja.

