- Buba Jammeh aongoza jahazi kuwazamisha wapinzani wao Uwanja wa KMC Complex.
- Yanga SC 2-0 Cosmopolitan FC CRDB Federation Cup 64 bora
- Azam FC vs Endumenti kupigwa saa 3:00 usiku
- Kamata matokeo na ratiba 2025/26 hapa
Yanga SC 2-0 Cosmopolitan FC CRDB Federation Cup 64 bora ni matokeo rasmi Uwanja wa KMC Complex. Februari 18, 2026 Wananchi waliwafungashia virago wapinzani wao moja kwa moja. Magoli yote yalifungwa na Buba Jammeh dakika ya 13 na 23.
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC joto linazidi kupanda/ Ratiba, msimamo
Bado hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Yanga SC 2-0 Cosmopolitan FC Buba aongoza jahazi

Wakati ubao ukisoma Yanga SC 2-0 Cosmopolitan FC Buba Jammeh aliongoza jahazi kuwazamisha wapinzani. Ni ukurasa wake mpya wa magoli amefungua akiwa na uzi wa kijani na njano. Alisubiri dakika 13 kuandika rekodi hiyo msimu wa 2025/26.
Matokeo ya mechi za CRDB Federation Cup Februari 18,2026
| JKT Tanzania | 7 | 0 | Pan African |
| Kagera Sugar | 3 | 0 | Mighty Elephan |
| Geita Gold | 1 | 0 | Kajuna FC |
| B19 FC | 7 | 0 | Dhujao FC |
| Barberian FC | 1 | 1 | Kijiwe Nongwa FC (Pen: 2-4) |
| Songea United | 2 | 1 | Vijana SC |
| Bigman FC | 0 | 1 | Nyika FC |
| Hausang FC | 2 | 1 | West Sengers |
| Stand United | 4 | 0 | Mabao FC |
| African Sports | 4 | 1 | Kilimo FC |
| Mtibwa Sugar | 5 | 0 | IAA SC |
| Pamba Jiji | 0 | 1 | Alliance FC (Pen: 4-2) |
| Mashujaa FC | 1 | 0 | Nkim FC |
| Mbuni FC | 5 | 1 | 1 Green FC |
Polisi Tanzania vs THB FC (Polisi wamepewa ushindi baada ya THB kutofika uwanjani)
SOMA HII: Allan Okello mambo fresh Yanga SC/ Orodha ya wapya waliotambulishwa

Matokeo ya mechi nyingine hatua ya 64 bora Februari 17

| Simba SC | 3 | 0 | 0 Greenland FC |
| KMC FC | 3 | 3 (P 2-3) | Bandari FC |
| Coastal Union | 3 | 1 | Nyumbu FC |
| Fountain Gate | 1 | 0 | Mapinduzi FC |
| Dodoma Jiji FC | 3 | 1 | Kilimanjaro Wonders |
| Transit Camp | 4 | 0 | Chama la Wana |
Mbeya City vs Biashara United Mara
Mchezo huu haujachezwa kutokana na Biashara United kutokufika uwanjani. Mbeya City walifika na kufuata taratibu zote. Baada ya dakika 30 mwamuzi akamaliza mchezo na hivyo Mbeya City kupewa ushindi kutokana na kanuni.
Ratiba ya Februari 19,2026 CRDB Federation Cup
| 19/02/2026 | Azam FC | vs | Endumenti/ Azam Complex |
Hitimisho
Yanga SC 2-0 Cosmopolitan FC ni karata ya ushindi kutetea taji hilo. Baada ya mchezo huo Wananchi watakuwa na kibarua mchezo wa ligi. Ni Namungo FC vs Yanga SC kituo kinachofuata Februari 22, Uwanja wa Majaliwa.

