DepuDepu vs Dodoma Jiji
  • Kibwana Shomari beki wa Yanga SC akimbizwa hospital kwa matibabu zaidi
  • Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC NBC Premier League 2025/26
  • Dupe afunga kwa penati, apewa tuzo ya mchezaji bora

Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC ni matokeo rasmi Tanzania Premier League. Walima zabibu walianza kufunga goli kupitia kwa William Edger dakika ya 42. Mshambuliaji wa Yanga SC, Depu alifunga goli la kuweka usawa dakika ya 45 na kuongeza goli la pili dakika ya 61. Prince Dube alizamisha jahazi la Dodoma Jiji kwa goli la tatu dakika ya 67, Uwanja wa KMC Complex.

SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi

Cheza na ushinde sasa na ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni muda huu

Hujashinda na kindege cha SportPesa? Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege.

image

Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC Depu mchezaji bora

Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC
Depu nyota wa Yanga SC akikabidhiwa tuzo ya mchezaji bora. Source: Yanga SC.

Wakishinda Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC, Januari 27,2026 Depu amechaguliwa kuwa mchezaji bora. Kamati imepitisha jina la mchezaji huyo ambaye amekabidhiwa tuzo yake na wadhamini. Huu ni mchezo wa pili kwa Depu akifunga magoli mawili na kufikisha matatu katika ligi ya NBC Premier League.

Beki wa Yanga SC Kibwana Shomari alikimbizwa hospitali kwa huduma zaidi. Mchezaji huyo alianguka uwanjani kwenye mchezo dhidi ya Dodoma Jiji FC. Taarifa kuhusu maendeleo yake itatolewa mara baada ya vipimo.

Yanga SC vs Dodoma Jiji FC matokeo yao

27/01/2026Yanga SC31Dodoma Jiji FC
22/06/2025Yanga SC50Dodoma Jiji FC
25/12/2024Dodoma Jiji FC04Yanga SC
22/05/2024Dodoma Jiji FC04Yanga SC
  05/02/2024Yanga SC10Dodoma Jiji FC
13/05/2023Yanga SC42Dodoma Jiji FC
22/11/2022Dodoma Jiji FC02Yanga SC

Msimamo wa Yanga SC vs Dodoma Jiji FC

 MPWDLPTS
1. Yanga SC871022
12. Dodoma Jiji FC1124510

Kikosi cha Yanga SC vs Dodoma Jiji FC

Langoni

Djigui Diarra.

Mabeki

Kibwana Shomari

 Zimbwe Jr

 Bacca

 Assinki

Viungo

Conte Balla

 Maxi Nzengeli

 Mudathir Yahya

 Pacome

 Washambuliaji

 Depu

Prince Dube.

Wachezaji wa akiba

 Masalanga, Abubakar, Nondo, Boka, Sheikhan, Damaro, Duke Abuya, Kouma, Mzungu na Okello.

SOMA HII: Yanga SC vs Dodoma Jiji FC (5-0) |Simba SC yawaka moto kwa matokeo ya Ligi Kuu NBC Bara

image

Kikosi cha Dodoma Jiji FC vs Yanga SC

Pacome vs Dodoma Jiji (-)
Pacome vs Dodoma Jiji NBC Premier League. Source: Yanga SC.

Ally Salim.

 Nelson Munganga

Salmin Hoza

Andy Bikoko

 Dickson Mhilu

 Andayson Solomon

 Mwana Kibuta

 Kelfin Salim

 Abdi Banda

 William Edger

 Idd Kipagwile.

Wachezaji wa akiba

Augustino Nsata, Karib Seif, Yassin Ngaza, George Makang’a, Gasper Damiani, Faraji Kayanda, Wazir Junior, Daniel Mrope, Layson Layson, Daud Milandu.

Hitimisho

Yanga SC 3-1 Dodoma Jiji FC inawarejesha kwenye uongozi wa ligi mabingwa watetezi huku wakulima wakiporomoka nafasi mbili. Kutoka nafasi ya 10 sasa nafasi ya 12, JKT Tanzania nafasi ya pili.

Share this: