- Timu mbili majirani Uganda na Tanzania zitavaana kesho Jumamosi.
- Uganda vs Tanzania ni mchezo ambao utapigwa kwenye Uwanja wa Stade El Barid mjini Rabat.
- Unatarajia kuwa mchezo mgumu kwani, kipigo kwa timu yoyote kati ya hizi, inamaanisha ataaga mashindano rasmi.
- Makala hii inaangazia baadhi ya dondoo muhimu za mchezo huo.
Baada ya kukubali vipigo katika mechi za ufunguzi za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025), timu mbili majirani Uganda na Tanzania zitavaana kesho Jumamosi. Uganda vs Tanzania mchezo huu utapigwa kwenye Uwanja wa Stade El Barid mjini Rabat. Kipigo kwa timu yoyote kati ya hizi, inamaanisha atakayepoteza anaaga mashindano rasmi. Makala hii inaangazia baadhi ya dondoo muhimu za mchezo huo.
SOMA HII PIA: AFCON 2025 Matchday 1: stats, Mechi 12, Magoli 29
Bado hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.]

H2H, Uganda vs Tanzania

Rekodi inaonyesha timu hizi mbili katika siku za karibuni, Uganda na Tanzania zimekutana mara 19 katika mashindano mbalimbali. Uganda wamekuwa na rekodi nzuri zaidi wakishinda mechi 11. Tanzania imeshinda mechi 4 tu, huku michezo minne iliyosalia ikiisha kwa matokeo ya sare.
Mechi 5 zilizopita za Tanzania
Kuwait 4-3 Tanzania
Iran 2-0 Tanzania
Tanzania 0-1 Zambia
Tanzania 0-1 Niger
Congo 1-1 Tanzania
Mechi 5 zilizopita za Uganda
Morocco 4-0 Uganda
Uganda 2-1 Chad
Algeria 2-1 Uganda
Botswana 0-1 Uganda
Uganda 2-0 Somalia
SOMA HII ZAIDI: AFCON 2025 Mahrez, Jackson, Achouri watikisa: Hawa hapa wafungaji bora wa Raundi ya 1
Vikosi vinavyotarajiwa kuanza

Uganda
Kipa: Magoola
Walinzi: Sibbick, Torach, Obita, Kayondo
Viungo: Ssemugabi, Semakula, Aucho, Mato
Washambuliaji: Lorenzen, Mukwala
Tanzania
Kipa: Foba
Walinzi: Kapombe, Mwamnyeto, Hamad, Hussein
Viungo: Mirishi, Msanga, Msuva, M’Mbobwa, Allarkhia
Mshambuliaji: Samatta
SOMA HII PIA: AFCON 2025 Match round 1: Hawa hapa washindi wa tuzo za mchezaji bora wa kila mechi
Habari za timu

Uganda walianza vibaya kwa kupoteza kwa mabao 3-1 mbele ya Tunisia, katika mchezo wa kwanza wa mashindano hayo. Vijana wa Paul Put watakuwa na hamu ya kuibuka na ushindi mbele ya Tanzania. Uganda wana kazi kubwa kufanikisha hilo kwani kupoteza kwao dhidi ya Tunisia, kunafanya wanakuwa wamepoteza mechi 3 kati ya 4 zilizopita za mashindano yote.
Katika hatua nyingine Uganda wamepoteza mechi sita kati ya tisa za mwisho za AFCON. The Cranes wataingia kwenye pambano hili, wakitafuta kuepuka vipigo vitatu mfululizo kwa mara ya kwanza tangu Novemba 2023. Ikumbukwe kupoteza kunaashiria kukosa nafasi yao ya kusonga mbele, ikizingatiwa kwamba Nigeria inawangoja katika mchezo wao wa mwisho.
Kwa Tanzania hali ni mbaya zaidi kwani katika siku za hivi karibuni, hawajapata ushindi wowote ndani ya michezo 8 mfululizo. Wamepoteza michezo 6 na kutoa sare mechi 2 na mechi za michuano yote (D2, L6), huku mechi zao tano mfululizo zilizopita wakipata vipigo.
Kupoteza kwao mele ya Nigeria siku ya Jumanne kumefanya waandikishe mechi 10 bila ushindi kwenye mashindano ya AFCON wamefungwa mara 7 na kutoa sare 3.
Taarifa za majeraha

Kuhusu majeraha, Uganda hawajaripoti mchezaji yoyote kabla ya mechi yao ya Jumamosi. Kwa Tanzania, Yakoub Suleiman na Feisal Salum, ambao wote walikosa mechi ya kwanza, huenda wakarejea kikosini.
Mlinzi Novatus Miroshi, anayechezea Goztepe ya Ligi Kuu ya Uturuki, alianza kwenye kiungo na alikuwa na kiwango bora.
Hitimisho
Uganda vs Tanzania ni vita ya majirani itakayopigwa Jumamosi hii nchini Morocco. Unatarajia kuwa mchezo mgumu hasa kwa kuwa atakayeruhusu kupoteza ataaga mashindano. Hivyo kila timu itapambana kutopoteza mchezo. Kwa kuangalia fomu yao katika siku za karibuni utabiri wa mchezo huu huenda ukaisha kwa matokeo ya sare.

