- Fashion Sakala nyota wa timu ya taifa ya Zambia alifunga goli pekee la ushindi kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
- Tanzania 0-1Zambia FIFA World Cup Qualifier 2026 matokeo yasiyofurahisha kwa Watanzania, kichezo Zambia.
- Vijue vikosi vya timu zote mbili kwenye mchezo huo wa Kundi E Oktoba 8 2025.
Tanzania 0-1 Zambia FIFA World Cup Qualifier 2026 yamezima ndoto za Watanzania kushuhudia wapambanaji wakifuzu hatua hiyo kubwa. Timu hizi zipo kundi E linaongozwa na timu ya taifa ya Morocco. Ni dakika 90 zilizokuwa na purukushani kubwa na matumizi ya nguvu nyingi. Hilo lilisababisha kuwa na jumla ya faulo 28 na kadi 5 za njano zikitolewa Oktoba 8 2025.
SOMA HII: CHAN 2024: Tanzania kuikabili Madagascar leo Agosti 9 2025/ Matokeo, vikosi, utabiri

Vuna mamilioni sasa hivi ukipaisha Kindege cha SportPesa
Ni sasa hivi unavuna mamilioni ukipaisha Kindege cha SportPesa. Ni rahisi sana hasa ukizingatia Marubani wapo makini. Cheza Aviator upate mgao wako.
Tanzania 0-1 Zambia goli lilifungwa kipindi cha pili

Mchezo wa kundi E ulichezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Tanzania 0-1 Zambia FIFA World Cup Qualifier 2026 goli la ushindi likifungwa kipindi cha pili. Mfungaji ni Fashion Sakala dakika ya 75 akitumia pasi ya Lubambo Musonda.
Goli la Zambia linaamnisha nini kwa Taifa Stars?

Goli hilo liliwawapa Zambia nafasi ya kuongoza lilidumu mpaka mwisho wa mchezo. Katika dakika 45 za mwanzo hakuna timu ambayo ilipata goli. Hivyo Tanzania imeangusha pointi tatu muhimu ikiwa nyumbani.
Kupoteza kwa Tanzania kunazima matumaini ya kupata tiketi kufuzu Kombe la Dunia 2026. Kwenye mchezo huo Zambia ilikuwa na umiliki asilimia 54 ilipiga jumla ya mashuti 11 huku 4 yakilenga lango. Tanzania ni mashuti 7 ilipiga ni mashuti 2 yalilenga lango huku wakicheza faulo 15 na Zambia faulo 13.
Zambia ina mchezo mmoja mkononi dhidi ya Niger ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa katika hatua ha makundi. Zambia ina pointi 9 inakutana na Niger yenye pointi 12. Ikiwa itapata ushindi itafikisha pointi 12.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Levy Mwanawasa Oktoba 12 2025. Morocco tayari wamekata tiketi ya kufuzu baada ya kuongoza kundi. Matokeo ya mchezo wa Zambia na Niger yataamua nani atakuwa nafasi ya pili.
Wajue wachezaji walioonyeshwa kadi za njano

Kwenye mchezo huo jumla ya kadi tano za njano zilitolewa na mwamuzi wa kati Ibrahim Traoreh. Tanzania ni wachezaji watatu wakionyeshwa kadi. Wawili walionyeshwa wa timu ya taifa ya Zambia.
Bakari Mwamnyeto dakika ya 56, Yahya Omary dakika ya 30 na kiungo Feisal Salum dakika ya 33 walionyeshwa kadi za njano kwa upande wa Tanzania. Lawarence Mulega dakika ya 89 na Benson Sakala dakika ya 78 walionyeshwa kadi kwa upande wa timu ya Zambia. Sababu kubwa ni kucheza faulo kwa wapinzani.
SOMA HII: Mauritania 0-1 Tanzania CHAN 2024 Kapombe shujaa/ Magoli, takwimu/ Robo fainali yanukia

Kikosi cha Tanzania vs Zambia
Yakoub Suleiman
Ibrahim Bacca
Bakari Mwamnyeto
Pascal Msindo
Israel Mwenda
Khalid Habibu
Yahya Omary
Feisal Salum
Charles M’Mombwa
Abdul Sopu
Paul Peter
Wachezaji wa akiba
Yusuph Kagoma
Lameck Lawi
Hussen Masalanga
Miano Danilo
Zuber Masudi
Kikosi cha Zambia vs Tanzania kilichoanza
Lawrence Mulenga
Kabaso Chongo
Benson Sakala
Kennedy Musonda
Gift Mphande
Kelvin Kapumbu
Obino Chisala
Fashion Sakala
Kelvin Kampamba
Kings Kangwa
Daka Patson
Wachezaji wa akiba
Frankie Musonda
Mathew Banda
Joseph Sabobo
Gift Siame
Charles Kalumba
Patrick Chooma
Clatous Chama
Dominic Chanda.
Msimamo Kundi E
| Timu | Mechi | Pointi |
| 1.Morocco | 7 | 21 |
| 2.Niger | 7 | 12 |
| 3.Tanzania | 8 | 10 |
| 4.Zambia | 7 | 9 |
| 5.Congo | 7 | 1 |
| 6.Eritrea | 0 | 0 |
Hitimisho
Tanzania 0-1 Zambia FIFA World Cup Qualifier 2026 ulikuwa ni mchezo uliobeba matumaini kwa Watanzania kufuzu hatua inayofuata. Kutokana na kupoteza pointi tatu milango imefungwa kutoka kundi E. Mchezo wa mwisho kwa Zambia na Niger utampata atakayekuwa nafasi ya pili ya msimamo wa kundi.


