- Ligi Kuu ya England inaendelea tena wikiendi hii kwa msisimko mkubwa.
- Hii ni kufuatia mechi kali ya Chelsea vs Liverpool kwenye Uwanja wa Stamford Bridge.
- Timu hizi zimekutana mara 199 katika historia, Chelsea wameshinda michezo 66. Michezo 46 imeisha kwa sare huku Liverpool wakiibuka wababe katika michezo 87.
Ligi Kuu ya England inaendelea tena wikiendi hii kwa msisimko mkubwa, Chelsea vs Liverpool ndio mchezo unaotupiwa jicho kwa ukubwa. Mchezo huu wa kukata na shoka unatarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge. Liverpool watakuwa na kazi kubwa ya kupambana kusalia kileleni, huku Chelsea wao wakijitahidi kuimarika zaidi kutoka kwenye matokeo mchanganyiko.
SOMA HII PIA: The Showdown at Stamford Bridge: Chelsea vs. Liverpool – A Thrilling Carabao Cup Final
Ushindi mzito wa ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni muda huu
Ni zamu yako kushinda na SportPesa, unaweza kushinda mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kupitia Kampuni bora ya michezo ya kubashiri ya SportPesa bonyeza picha hii chini.

H2H Chelsea vs Liverpool

Timu hizi zimekutana mara 199 katika historia, Chelsea wamefanikiwa kushinda michezo 66. Michezo 46 imeisha kwa matokeo ya sare huku Liverpool wakiibuka wababe katika michezo 87.
SOMA HII ZAIDI: Liverpool vs Chelsea clash in the potential title decider 31th January 2024

Mechi 5 zilizopita za Chelsea
30 Sep Chelsea 1-0 Benfica
27 Sep Chelsea 1-3 Brighton
23 Sep Lincoln 1-2 Chelsea
20 Sep Manchester United 2-1 Chelsea
17 sep Bayern Munich3-1Chelsea
Mechi 5 zilizopita za Liverpool
30 Sep Galatasaray 1-0 Liverpool
27 Sep Crystal Palace 2-1 Liverpool
23 Sep Liverpool 2-1 Southampton
20 Sep Liverpool 2-1 Everton
17 Sep Liverpool 3-2 Atletico Madrid
Kikosi cha Chelsea kinachotarajiwa kucheza dhidi ya Liverpool

Kipa:
Sanchez
Mabeki:
James, Acheampong, Badiashile, Cucurella
Viungo:
Fernandez, Caicedo, Estevao.
Washambuliaji
Buonanotte, Neto, Pedro.
Kikosi cha Liverpool kinachotarajia kuanza dhidi ya Chelsea

Kipa:
Mamardashvili
Mabeki:
Frimpong, Konate, Van Dijk, Kerkez
Viungo:
Mac Allister, Gravenberch Salah, Szoboszlai
Washambuliaji:
Gakpo, Isak.
Habari za timu
Trevoh Chalobah kwa upande wa Chelsea anatarajiwa kukosekana, kutokana na kadi nyekundu aliyopokea dhidi ya Brighton. Wachezaji wengine kama Mykhaylo Mudryk, Dario Essugo, Tosin Adarabioyo, Cole Palmer, Liam Delap, na Levi Colwill bado hawana nafasi ya kucheza kutokana na majeraha au adhabu.
Mwanzoni mwa msimu huu Chelsea ilionekana kuwa timu ya kuchungwa, lakini hadi sasa bado ubora wao hauridhishwi kikamilifu. Kocha wa timu hiyo, Enzo Maresca, ameingia katika changamoto kubwa, Hii ni baada ya timu yake kushinda michezo miwili tu, sare mbili, na kupoteza michezo miwili kati ya sita walizocheza hadi sasa.
Changamoto kubwa kwa Chelsea ni ushindi wa mara moja tu katika michezo yao mitatu ya hivi karibuni ya ligi. Hii imesababisha timu hiyo kushuka hadi nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi, ikiwa nyuma kwa pointi saba kutoka kileleni. Kiwango cha majeruhi pamoja na wachezaji walioachwa nje kutokana na adhabu, au matatizo ya nidhamu kumeathiri sana utendaji wa timu hii.
Chelsea wamepokea kadi nyingi zaidi kuliko timu nyingine yoyote msimu huu kadi 118 kwa jumla, kati ya hizo kadi 114 ni za njano na nne ni nyekundu. Hali hii imesababisha timu hii kucheza michezo mingi wakipungukiwa wachezaji muhimu. Hali hii ilionekana kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Benfica, ambapo walikosa wachezaji wawili kwa sababu ya kadi nyekundu, ingawa walifanikiwa kushinda 1-0.
Kwa Liverpool, Alisson Becker yupo nje, lakini Federico Chiesa anaweza kurudi uwanjani baada ya kupata nafuu kutoka majeraha madogo. Giovanni Leoni bado anarejea polepole kutokana na jeraha kubwa la ACL.
Kwa upande mwingine, mabingwa watetezi Liverpool, wanakumbwa na msimu mgumu zaidi. Hali yao imeanza kuonyesha dalili za kushuka kiasi. Hii ikiwa ni baada ya kupoteza michezo miwili mfululizo, jambo ambalo halijawahi kutokea mara nyingi chini ya kocha Arne Slot.
Mchezo wa hivi karibuni uliowapoteza dhidi ya Crystal Palace umevunjika moyo kwa mashabiki wa Liverpool, baada ya Eddie Nketiah kuwalazimisha kupoteza pointi kwenye dakika za mwisho. Pia, katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Liverpool walipoteza kwa Benfica kwa bao 1-0 kupitia penalti, jambo ambalo limeongeza presha kwa timu hiyo.
Liverpool wanakabiliwa pia na changamoto za majeruhi, ikiwa ni pamoja na mlinda mlango wao Alisson Becker, ambaye hatacheza dhidi ya Chelsea kutokana na jeraha la goti. Hali hii inamfanya kocha Slot kutumia mchezaji mwingine.
Utabiri wa mchezo

Ingawa Chelsea hawajashinda michezo mingi hivi karibuni, wanajulikana kwa uwezo wao wa kufunga magoli. Wamefunga katika michezo yao minane iliyopita katika mashindano yote. Jambo ambalo linawaweka katika nafasi nzuri dhidi ya Liverpool, ambayo inaonekana kuwa na ulinzi dhaifu.
Liverpool hawana rekodi nzuri Stamford Bridge, wakiwa hawajashinda katika michezo yao minne ya mwisho ya ligi ugenini dhidi ya Chelsea. Msimu uliopita walipoteza 3-1 uwanjani hapo, ingawa walikuwa tayari wamekuwa mabingwa. Kwa kuzingatia matokeo haya, huenda mchezo huu ukawa kwenye nafasi kubwa ya kuisha kwa matokeo ya sare.
SOMA HII PIA: Chelsea VS Liverpool- Nani kuibuka kidedea?

Hitimisho
Mchezo huu wa Chelsea vs Liverpool unatazamiwa kusubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka. Ingawa kila timu ina changamoto zake, ushindani mkali na mabadiliko ya msimu huu huenda yakatoa matokeo ya kushangaza. Timu zote zinahitaji kuonyesha umoja na kuonyesha uwezo wa hali ya juu ili kupata ushindi au angalau kupata pointi muhimu.

