- Djigui Diarra amekuwa shujaa kwa kuokoa hatari mbili katika dakika 45 za mwanzo
- Yanga SC 0-0 Simba SC NBC Premier League, New Amaan Complex ikiwa ni mapumziko
- Dickson Job ameshindwa kuendelea na mchezo nafasi yake imechukuliwa na Bakari Nondo
- Loemba amekosa nafasi ya wazi katika dakika 15 za mwanzo, Pacome out Kariakoo Dabi
Yanga SC 0-0 Simba SC NBC Premier League matokeo ya dakika 45 za mwanzo. Mlinda mlango wa Yanga SC, Djigui Diarra ameokoa hatari mbili za hatari langoni. Mnyama anakwenda mapumziko akiwa ameshindwa kuzibadili nafasi alizopata kuwa magoli.
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC taarifa mpya kutoka Zanzibar, hali ya vikosi, Goncalves na Steve Barker

Yanga SC 0-0 Simba SC NBC Premier League, Pacome out

Yanga SC 0-0 Simba SC NBC Premier League ni dakika 45 za moto kwa timu zote mbili Uwanja wa New Amaan Complex. Kiungo wa Yanga SC, Pacome Zouzoua out kwenye mpango kazi kutokana na kutokuwa fiti. Kwenye kikosi cha kwanza wala akiba hayupo.
Beki Dickson Job wa Yanga SC amefanyiwa mabadiliko ya lazima baada ya kuchezewa faulo na Loemba dakika ya 37. Nafasi yake imechukuliwa na Bakari Nondo.
Kikosi cha Yanga SC kilichoanza vs Simba SC
Langoni
Djigui Diarra
Mabeki
Israel Mwenda
Mohamed Hussen
Dickson Job
Ibrahim Bacca
Viungo
Damaro
Maxi Nzengeli
Duke Abuya
Mudathir Yahya
Washambuliaji

Depu
Prince Dube
Wachezaji wa akiba ni Mshery, Yao, Nondo, Abubakar, Aziz, Mwanengo, Abdulnasir, Shekhan, Okello na Buba.
SOMA HII: Yanga SC vs Simba SC NBC Premier League: Nassoro Mwinchui mwamuzi wa kati, utabiri

Kikosi cha Simba SC vs Yanga SC
Langoni
Kassali
Mabeki
Shomari Kapombe
Nickson Kibabage
Toure
De Reuck
Viungo
Yusuph Kagoma
Gueye
Kante
Clatous Chama
Inno
Loemba
Mshambuliaji
Oura
Wachezaji wa akiba ni Hussen Abel, Duchu, Mligo, Naby, Vedastus, Morice, Semfuko, Mwalimu, Neo na Ellie Mpanzu.
Hitimisho
Yanga SC 0-0 Simba SC NBC Premier League ni dakika 45 za mwanzo kwenye mchezo. Matokeo kamili yatafahamika baada ya dakika 90. Nani atachukua pointi tatu jumla ama watagawana alama?

