- Kituo kinachofuata ni Kariakoo Dabi Machi Mosi 2026, Yanga SC vs Simba SC
- Yanga SC yaichapa 5-0 JKT Tanzania NBC Premier League
- Depu, Prince Dube waliamsha Uwanja wa KMC Complex, Dar
Yanga SC yaichapa 5-0 JKT Tanzania ni matokeo rasmi mchezo wa NBC Premier League. Ushindi huo unawashusha wazee wa kipigo cha kizalendo nafasi ya kwanza mpaka ya pili. Usukani wa ligi upo mikononi mwa Yanga SC ikifikisha jumla ya pointi 28.
SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi
Je hujashinda? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa hivi
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Yanga SC yaichapa 5-0 JKT Tanzania wafungaji hawa hapa

Wakati ubao wa Uwanja wa KMC Complex ukisoma Yanga SC 5-0 JKT Tanzania beki alifungua ukurasa wa magoli. Ni Mohamed Hussen Zimbwe Jr alipachika goli dakika ya 8 kwa pasi ya Prince Dube, alifunga goli la pili Depu dakika ya 61 kwa pasi ya Israel Mwenda.
Kiungo Mudathir Yahya alipachika goli la tatu dakika ya 64 na Prince Dube alipachika goli la nne dakika ya 84 kwa pasi ya Buba Jammeh na msumari wa mwisho ukifungwa na Shekhan Khamis dakika ya 90 pasi ya Mwenda.
SOMA HII: Yanga SC 2-0 JKT Tanzania; Yanga yatinga Fainali Shirikisho CRDB yawasubiri Simba/Singida BS

Yanga SC vs JKT Tanzania msimamo wa NBC
| MP | W | D | L | PTS | |
| 1. Yanga SC | 10 | 9 | 1 | 0 | 28 |
| 2.JKT Tanzania | 17 | 7 | 7 | 3 | 28 |
Kituo kinachofuata ni Yanga SC vs Simba SC

Baada ya ushindi wa leo kituo kinachofuata ni Kariakoo Dabi, Machi Mosi 2026, Uwanja wa New Amaan Complex. Ni Yanga SC vs Simba SC ratiba inaonyesha hivyo. Huu ni mchezo mkubwa Afrika unasubiriwa kwa shauku kubwa.
Hitimisho
Yanga SC yaichapa 5-0 JKT Tanzania ni mwendelezo wa ushindi kwenye mechi za ushindani. Mshambuliaji Depu amezidi kuwa mtambo wa magoli.Prince Dube amechaguliwa kuwa mchezaji bora mara baada ya dakika 90 kukamilika.

