Kocha Mkuu mpya Simba SC Steve BarkerKocha Mkuu mpya Simba SC Steve Barker
  • Uongozi wa Simba SC rasmi umemtangaza raia wa Afrika Kusini, Steve Barker kuwa kocha wao mkuu mpya.
  • Kocha mpya Simba SC Steve Barker anakuwa Mwalimu wa tatu kuiongoza Simba SC msimu huu.
  • Kocha huyu anakuja kuchukua mikoba ya Dimitar Pantev aliyefungashiwa virago.
  • Je, unajua CV ya kocha Barker? Soma Makala hii ujue kila kitu.

Uongozi wa Simba SC rasmi umemtangaza raia wa Afrika Kusini, Steve Barker kuwa kocha wao mkuu mpya. Kocha huyo anatarajiwa kuanza rasmi majukumu ya kukinoa kikosi hiko, akichukua mikoba ya Dimitar Pantev aliyefungashiwa virago. Makala hii inaangazia wasifu (CV), ya kocha huyo mpya.

SOMA HII PIA: Kocha mpya Simba SC jina mezani/ Kocha Yanga SC CV zake zatua Msimbazi, utambulisho wapangwa

Hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa

Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

image

Wasifu binafsi wa kocha mpya Simba SC Steve Barker

Steve Barker
Steve Barker

Kuzaliwa: 23/12/1967 (57)

Mahali alipozaliwa: Lesotho Maseru

Uraia: South Africa

Mfumo anaopenda kutumia

Stellenbosch
Stellenbosch

Kocha huyu anapendelea soka la kushambulia na hutumia zaidi mfumo wa 4:3:3. Kwa kawaida amekuwa na wastani wa miaka 4.2 katika timu ambazo amewahi kufundisha. Barker ni mzoefu wa soka la nchi za Kusini mwa Afrika, ambapo alitumia muda mwingi nchini Afrika Kusini. Kocha huyu amejiunga Simba SC akitokea kikosi cha Stellenbosch aliyoifikisha nusu fainali ya kombe la Shirikisho msimu uliopita.

SOMA HII ZAIDI: Unamfahamu, Dimitar Pantev kocha mpya Simba SC? Hizi hapa rekodi zake, mifumo na mafanikio

Takwimu zake msimu huu

Kwa mujibu wa mtandao maarufu wa kutunza takwimu za michezo wa Transfermarkt, msimu huu Barker ameiongoza Stellenbosch katika michezo 24. Ameshinda mechi 8, sare mechi 6 na kupoteza mechi 10. Katika michezo hiyo amekusanya pointi 30, hii inamfanya awe na wastani wa pointi 1.25 kwa mchezo.

Total:        24     8       6       10     30     1.25

Rekodi ya timu alizowahi kupita

Steve Barker - Mechi --- kama kocha mkuu Stellenbosch
Steve Barker – Mechi 300 kama kocha mkuu Stellenbosch

Stellenbosch kuanzia mwaka 2017 ameifundisha michezo zaidi ya 300

Alexandra Black Aces 2016-2017

AmaZulu FC 2014-2016

University of Pretoria FC U. Pretoria 2008-2014.

SOMA HII PIA: Dimitar Pantev kocha mpya Simba SC anapenda kushambulia | Mkataba wake, orodha ya wachezaji wapya

Hitimisho

Mafanikio ya Steve Barker
Mafanikio ya Steve Barker

Uteuzi wa kocha mpya Simba SC Steve Barker umekamilika, swali kubwa sasa ni ikiwa ataweza kufikia matarajio ya Wanasimba.  Hii ni baada ya kuwa na mwenendo usioridhisha tangu walipoachana na kocha Fadlu Davis. Barker anakuwa kocha wa tatu kuifundisha Simba SC msimu huu, mara baada ya Fadlu Davis na Dimitar Pantev.

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.