PascalMsindo StarsPascalMsindo Stars
  • Iran 2-0 Tanzania, haya ndio matokeo rasmi kwenye mchezo wa kirafiki kwenye Uwanja wa Rashid.
  • Wenyeji Iran walipata ushindi kupitia magoli ya Amirhossen Hosseinzadeh na Mohammad Mohebi.
  • Haya ndio matukio, magoli na matokeo rasmi ya Iran vs Tanzania

Iran 2-0 Tanzania ndio matokeo rasmi kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa Oktoba 14,2025 pale Dubai. Iran walipata goli la kwanza kupitia tuta la penalti dakika ya 17 na kuongeza la pili dakika ya 26. Mchezo uliopita Tanzania, ilipoteza kwa kufungwa goli 1-0 dhidi ya Zambia, mchezo uliochezwa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Unasubiri nini? Vuna mamilioni sasa hivi

Kuna jambo umekwama kwa sasa kuhusu mkwanja? Usiogope, rubani ni jasiri na kazi yake ni kupaisha kindege cha SportPesa. Cheza sasa hivi Aviator uvune mamilioni bofya hapa chini.

image

SOMA HII: CHAN 2024: Central African 0-0 Tanzania | Matokeo, vikosi, takwimu |Feisal Salum na tuzo

Iran 2-0 Tanzania, wajue wachezaji waliofunga magoli

Iran 2-0 Tanzania
Nyota wa Tanzania akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Iran. Source: TFF.

Amirhossen Hosseinzadeh alifungua pazia la kufunga dakika ya 17, huku Mohammad Mohebi akitikisa wavu dakika ya 26. Kufikia kipindi cha pili Iran waliongeza goli tatu lilikataliwa na mwamuzi wa mechi. Magoli hayo yalidumu mpaka mwisho wa mchezo huku Tanzania ikipoteza kwa 2-0 dhidi ya Iran.

Haya ndio maoni ya Kocha Mkuu wa Tanzania Hemed Morocco

Simba SC vs Nsingizini Hotspurs
Hemed Suleiman Kocha Mkuu wa Taifa Stars. Source: Simba SC.

Morocco amesema:”Tulikuwa na mchezo mgumu, tulipata nafasi tukashindwa kutumia. Makosa ya mtu mmojammoja yalitokea na hapo wapinzani wakapata nafasi wakatumia.

“Tulikuwa tumeanza vizuri dakika 20, 25 kulikuwa na presha kubwa kutoka kwa wapinzani wetu Iran. Kwa aina ya wachezaji ambao tupo nao makosa ambayo yanatokea ni sehemu ya mchezo. Katika dakika za mwanzo tulikuwa tunafanya kazi kubwa. Mwisho wapinzani wetu walikuja kulazimisha kutafuta magoli.

“Ninajivunia kwa ajili ya wachezaji kwa namna ambavyo wanacheza. Kuna mwendelezo ambao upo kwa ajili ya wakati ujao. Ilikuwa ni mechi ngumu hivyo tukipata mechi nyingine kama hizi tutakuwa bora zaidi.

“Kipindi cha pili tulikuja na mbinu ya kutafuta usawa. Haikuwa hivyo bado tulikwama kufunga. Unaona kuna mwendelezo ambao upo kwa kuwa vijana wanazidi kuwa imara.

Magoli yote yalifungwa kipindi cha kwanza na nyota wa Iran, dakika ya 17 kwa mkwaju wa penalti na dakika ya 26.

SOMA HII: CHAN 2024: Tanzania 2-1 Madagascar Mzize afunga magoli mawili/ Robo fainali imejibu, rekodi, magoli

image

Kikosi cha Iran vs Tanzania

 Kocha Mkuu, Amir Ghalenoei

Mlinda mlango
P. Niazmand

Mabeki

D Esmaeulifar
S. Khalilzadeh
M.A. Hazbavi
M. Mohammadi

Viungo

S.Ghoddos
S. Ezatolahi
K.Taheri

Washambuliaji

A.Hisseinzade
M.Hashemnejad
M. Mohebi.

Wachezaji wa akiba

 Mohammadjavad Hosseinnehed

Alireza Jahanbakhs

Ali Nemati

 Mohammad Ghorbani

 Allahyar Sayyadmanesh

 Ali Alipour

 Mohammadreza Akhbari

Alireza Beiranvand

 Omid Noorafkan

Mehdi Zare

 Mohammad Khodabandelou

Ramin Rezaeian.

Kikosi cha Tanzania, Taifa Stars vs Iran

Tanzania vs Iran
Abdul Suleiman nyota wa Tanzania kwenye mchezo dhidi ya Iran. Source: TFF>

 Kocha Mkuu Hemed Suleiman

Mlinda mlango
Yakoub Suleiman
Mabeki
Ibrahim Bacca
Pascal Msindo
Bakari Nondo
Israel Mwenda

Viungo
T. Allarakhia
Miroshi
Y. Omary
Feisal Salum

Washambuliaji
P.Peter
C. M’Mombwa

Wachezaji wa akiba

Lusajo Mwaikenda
Morice Abraham
Abdul Suleiman
Zuber Foba
Offen Chikola
Miano Danilo
Lameck Lawi
Hussen Masaranga
Khalid Habibu

SOMA HII: CHAN 2024: Tanzania 0-1 Morocco ni kilio kwa wenyeji | Matukio muhimu, vikosi, takwimu

image

Hitimisho

Iran 2-0 Tanzania ndio matokeo kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa pale Dubai. Kwa Taifa Stars kilikuwa ni zaidi ya kipimo kwa kuwa wachezaji wamepata nafasi kujitangaza. Kukosa ushindi kutawapa nafasi kujipanga kwa mechi zijazo kuwa imara zaidi. Baada ya mchezo huu, Iran wanajipanga kwenda kwa mashindano mengine ya timu nne yatakayofanyika Dubai mnamo Novemba 2025.

Share this: