----------------------------------------------n----------------------------------------------n
EURO
Jamal Musiala

STAA wa kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani na klabu ya Bayern Munchen, Jamal Musiala ndiyo habari ya mjini katika mashindano ya Euro 2024 yanayoendelea nchini Ujerumani.

Musiala amekuwa na wastani mzuri katika mashindano hayo baada ya kufanikiwa kuisaidia Ujerumani kukusanya pointi 6 katika michezo yao miwili ya kwanza.

Ujerumani ya Musiala walianza kwa kishindo kwenye mashindano ya EURO2024 hayo kwa ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya timu ya Taifa ya Scotland kabla ya kuwachapa 2-0 Hungary kwenye mchezo wao wa pili uliopigwa huko jijini Stuttgart.

UJERUMANI YA MUSIALA YAANDIKA REKODI EURO 2024

EURO
Kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani

Ushindi huo dhidi ya Hungary ambao Musiala aliendelea kuamika kwenye kikosi cha kwanza uliifanya Ujerumani kuandika rekodi ya kuwa timu ya kwanza kufanikiwa kutinga hatua ya mtoano ya mashindano hayo kwa mwaka huu.

Ujerumani walifanikiwa kuandika rekodi hiyo mbele ya timu ngumu ya Hungary huku wakishuhudiwa na umati wa mashabiki wengi wa timu hiyo ya Taifa ambao walijitokeza uwanjani kutoa sapoti.

Ni, Musiala na Ilkay Gundogan ambao walipeleka kilio kwenye kambi ya wapinzani wao.

Katika mchezo huo, Hungary walitengeneza nafasi nyingi za kufunga mapema lakini waliadhibiwa wakati Jamal Musiala alipofunga bao la kwanza la mchezo huo, VAR iliangalia kuona ikiwa kulikuwa na uvunjwaji wa sheria.

UBORA WA UJERUMANI UKO HAPA

  1. NAMNA YAO YA KUCHEZA MIPIRA ILIYOKUFA

Wengi wameona kipande cha video ambacho kimefanya vizuri kikionysha Ujerumani ikiwashangaza wadau wa michezo baada ya kupatikana bao la ufunguzi  sekunde saba tu, katika mechi yao ya kirafiki mwezi Machi, mwaka huu.

Mpira mmoja ulichezwa nyuma, watu wengi wakakimbilia mbele juu ya mstari wa nyuma wa Ufaransa na kuwasukuma nyuma. Pasi iliyokatwa kutoka kwa, Toni Kroos kwenye nafasi ya mlinzi wa kushoto na Florian Wirtz, ambaye kisha alipiga shuti kali.

  1. KROOS’ NI MTU NA NUSU

Nyota aliyetangaza kustaafu soka baada ya mashindano ya Euro, Toni Kroos ameendelea kuwashangaza wengi kwa uwezo mkubwa ambao anauonyesha akiwa ana timu hiyo.

Nyota huyo anatarajiwa kutundika ‘Daluga’ mara baada ya mashindano kuisha, huku akitumia muda huu kuaga mashabiki zake.

  1. MFUMO

Chini ya kocha, Julian Nagelsman timu ya Taifa ya Ujerumani kwenye mashindano haya ndani ya makaratasi wamekuwa wakitumia mfumo wa 4-2-3-1, lakini mara nyingi wakiwa hawana mpira hubadilika na kuwa  4-5-1. Hii inaonyesha ni kazi kubwa inafanyika uwanja wa mazoezi.

  1. VITA YA MUSIALA NA JUDE BELINGHAM?
EURO-2024-MUSIALA-AITEKA-SHOO
Jude Bellingham

Musiala na Jude Bellinham ni miongoni mwa mastaa ambao kwa sasa wanazua mijadala mizito juu ya nani bora zaidi kati yao na huku wakiendelea kuwagawa mashabiki wao duniani kote, nyota hao makinda wamekuwa wakitabiriwa kuwa huenda tukashuhudia wakivutana shati kuwania tuzo ya mchezaji bora wa ya EURO 2024.

Mfano, Musiala tayari amechaguliwa kuwa mchezaji bora walipocheza dhidi ya Scotland, huku Jude naye akitwaa tuzo kama hiyo na tayari ameweka kambani bao moja mpaka sasa. lakini tayari kwa mwaka huu pekee amechangi zaidi ya mabao 30 kwenye timu ya Taifa na klabu ya Real Madrid.

Musiala ndani ya mwaka huu pekee amehusika kwenye mabao 24, kwenye timu yake ya Taifa na klabu.

  1. KUREJEA KWA KIWANGO CHA GOLIKIPA, MANUEL NEUER

Kutokana na changamoto ya umri na majeraha, katika siku za hivi karibuni, kuna wakati baadhi ya mashabiki wa Ujerumani walikuwa wanaamini ni muda muafaka sasa kwa kipa na nahodha wao, Manuel Neuer kuachia ngazi.

Nyota huyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 38 mpaka sasa anaonekana kuwajibu wapinzani ambao wameonekana kuhoji kuhusu uwezo wake hususani kutokana na michomo ya hatari aliyoiokoa katika mchezo wao wa makundi EURO 2024 dhidi ya Hungary.

Kampuni ya michezo ya SportPesa inakupa nafasi ya kubashiri na kushinda kutokana na odds kubwa na malipo ya haraka ambazo unazipata kwetu tu, changamkia ofa hii katika kipindi cha mashindano haya ya EURO 2024 ambayo yanaendelea nchini ujerumani. Unaweza kuweka ubashiri wako kwa kutembelea tovuti ya SportPesa, au bonyeza link hii hapa

Share this:

By Joel Thomas

Joel Thomas is a Tanzanian sports writer with a BSc (Education) from Mwenge Catholic University. He spent 4 years at Global Publishers and is in his second year with SportPesa, covering football and betting education for local fans. Anapenda soka na anaandika kwa uwajibikaji.