Mtibwa Sugar watibua madadiliko ya Yanga SCFT
  • FT: Mtibwa Sugar 1-1 Yanga SC NBC Premier League, 2025/26
  • Pacome Zouzoua amefunga goal dakika ya 23 kipindi cha kwanza
  • Ismail Mhesa amefunga goal dakika za jioni akitokea benchi, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma
  • Mtibwa Sugar watibua mabadiliko Yanga SC, Machi 21, 2026

Mtibwa Sugar watibua mabadiliko Yanga SC NBC Premier League. Wananchi walibainisha wataonyesha utofauti mwisho wamegawana alama moja kwa kufungana 1-1. Huu unakuwa mchezo wa 3 kwa Yanga SC mfululizo bila kupata ushindi ndani ya ligi.

SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi

image

Mtibwa Sugar watibua mabadiliko Yanga SC, Mhesa afunga dakika za jioni

Mtibwa Sugar watibua madadiliko ya Yanga SC
Mhesa Ismael mfungajiwa goli la Mtibwa Sugar kwa pigo la kona. Source: Mtibwa Sugar.

Ni Mtibwa Sugar watibua mabadiliko Yanga SC NBC Premier League. Goli la uongozi lililofungwa na Pacome Zouzoua dakika ya 23 lilidumu hadi dakika ya 89. Ismail Mhesa ambaye alianzia benchi alifunga goli la usawa dakika ya 90+2.

Kabla ya mchezo, Ali Kamwe, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Yanga SC alibainisha kutakuwa na mabadiliko. Licha ya kupata goli vinara walikwama kulinda ushindi huo. Mchezo wa mzunguko wa kwanza ilikuwa Yanga SC 2-0 Mtibwa Sugar, Uwanja wa KMC Complex, Dar.

SOMA HII: Yanga SC wanaanza mabadiliko leo NBC Premier League vs Mtibwa Sugar/ H2H, prediction

Aviator

Takwimu za Mtibwa Sugar 1-1 Yanga SC, NBC Premier League

Mtibwa Sugar Yanga SC
6Mashuti14
3Lenga lango8
37%Umiliki63%
3Mashuti yasiyolenga lango6
0Kadi nyekundu0
1Kadi ya njano0
2Kona7
1Magoli1

Yanga SC yaangusha pointi 6

Maxi Nzengeli
Maxi Nzengeli kiungo wa Yanga SC vs Mtibwa Sugar. Source: Yanga SC.

Mchezo wa leo unakuwa wa tatu mfululizo kwa mabingwa watetezi kukwama kuvuna pointi tatu. Ilikuwa Azam FC 0-0 Yanga SC, TRA United 0-0 Yanga SC na Mtibwa Sugar 1-1 Yanga SC. Pointi 6 wameangusha kwenye mechi za ugenini chini ya Kocha Mkuu, Pedro Goncalves.

Msimamo  wa Mtibwa Sugar vs Yanga SC

POSMPWDLPTS
1. Yanga SC16115038
7.Mtibwa Sugar FC1757522

Kikosi cha Mtibwa Sugar vs Yanga SC

Langoni ni Costantine Malimi

Wengine ni Oscar Masai, Haroun Lyawata, Datius Peter, Omari Selemani, Kassim Shaibu, George Chota, Magata Charles, Andrea Simchimba, Said Mkopi na Evance Fabian.

Wachezaji wa akiba ni Juma Nyangi, Nassoro Kiziwa, Ismail Mhesa, Erick Kyaruzi, Laurent Alfred, Said Kazi, Juma Louzio, Toba Kutisha, Omary Yahya na Riphat Mrisho.

Kikosi cha Yanga SC vs Mtibwa Sugar

Langoni

Djigui Diarra

Mabeki

Frank Assink

Bakari Nondo

Mohamed Hussen

Israel Mwenda

Viungo

Maxi Nzengeli

Mudathir Yahya

Pacome Zouzoua

Duke Abuya

Allen Okello

Mshambuliaji

Emmanuel Mwanengo

Wachezaji wa akiba

Kocha Yanga
Pedro Goncalves, Kocha Mkuu wa Yanga SC. Source: Yanga SC.

Aziz Andabwile, Buba Jammeh, Yao Kouassi, Kibwana Shomary, Lassine Kouma, Mohamed Damaro, Abutwalib Mshery, Sheikhan Ibrahim, Abdulnassir Abdallah na Abubakar Nozar.

SOMA HII: Yanga SC 2-0 Mtibwa Sugar NBC Premier League KMC Complex | Highlights, magoli, Zimbwe Jr mchezaji bora

Aviator

Hitimisho

Mtibwa Sugar watibua mabadiliko Yanga SC kwa kuwazuia kuondoka na alama tatu muhimu. Pointi moja inawaondoa wakulima wa miwa kutoka nafasi ya 9 hadi nafasi 7. Vinara wanafikisha pointi 38 baada ya mechi 16.

Share this: