- Yanga SC vs Polisi Tanzania ni mchezo unaofuata kwenye ratiba Uwanja wa KMC Complex, saa 1:15 usiku.
- Simba SC 2-0 B19 FC CRDB Federation Cup, Loemba na Clatous Chama wafunga magoli ya ushindi.
- Azam FC kujiuliza kwa Mbeya Kwanza Uwanja wa Azam Complex.
Simba SC 2-0 B19 FC CRDB Federation Cup ni matokeo rasmi hatua ya 32 bora, Uwanja wa Mej Gen. Isahmuyo. Magoli ya Inno Loemba dakika ya 22 na Clatous Chama dakika ya 77 yamewatuliza wapinzani wao. Ni hatua ya 16 bora wanatinga wakiwa nyumbani. Yanga SC vs Polisi Tanzania, Azam FC vs Mbeya Kwanza ni mechi zinazofuata kwenye ratiba.
SOMA HII: Usajili wa Chama Simba SC washtua! Mayele, Kagere, Okwi wafunguka Mazito
Je, bado hujashinda pesa? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa
Ni zamu yako sasa, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Simba SC 2-0 B19 FC CRDB Federation Cup, Loemba afungua pazia

Simba SC 2-0 B19 FC CRDB Federation Cup ubao umesoma namna hiyo baada ya dakika 90. Inno Loemba alifungua pazia kwa pigo la kichwa kilichomshinda mlinda mlango. Hiyo ni baada ya wenyeji kufanya shambulizi la kushtukiza.
Kiungo Clatous Chama alifunga goli la pili lililoihakikishia Simba SC kutinga hatua ya 16 bora. Mchezo unaofuata CRDB Federation Cup itakuwa vs Dodoma Jiji FC. Ikumbukwe kwamba mchezo wa ligi wababe hawa waligawana pointi mojamoja.
Kikosi cha Simba SC kilichoanza
Mlinda mlango
Hussen Abel
Mabeki
Duchu
Anthony Mligo
Vedastus
Toure
Viungo
Naby
Bashiri
Kante
Inno
Morice Abraham
Gueye
Wachezaji wa akiba

Kassali, Kapombe, Kibabage, Mbegu, Kagoma, Oura, Semfuko, Baraka, Chama na Mpanzu
Seleman Mwalimu aukosa mchezo wa kwanza
Mshambuliaji wa Simba SC, Seleman Mwalimu ameukosa mchezo wa kwanza kati ya mitatu aliyofungiwa. Nyota huyo anatumikia adhabu ya kutocheza mechi tatu ni baada ya maamuzi ya Kamati ya Saa 72. Kosa la mchezaji huyo ni kumpiga kiwiko mchezaji wa Dodoma Jiji FC, Andy Bikoko.
Mchezo ujao wa Singida Black Stars vs Simba SC, Mwalimu ataukosa pia na ule wa tatu itakuwa ni TRA United vs Simba SC.
SOMA HII: Ratiba ya Simba SC 2025/26 Machi dakika 450 za kazi/ Msimamo, matokeo

Matokeo 32 bora Machi 7 2026
Namungo FC 4-1 Kagera Sugar,
Pamba Jiji 2-1 Transit Camp,
Geita Gold 4-1 Nyika
Mashujaa FC 0-0 Ken Gold (Pen: 5-3)
Matokeo ya Machi 6,2026
TRA United FC 4-0 Kijiwe Nongwa
Dodoma Jiji 2-0 African Sports
JKT Tanzania 2-0 Hausung FC
Ratiba ya 32 bora

Yanga SC vs Polisi Tanzania, Machi 8,2026, Uwanja wa KMC Complex, saa 1:15 usiku
Azam FC vs Mbeya Kwanza, Machi 8,2026, Uwanja wa Azam Complex saa 3:15 usiku
SOMA HII: Simba SC kufanya usajili mkubwa | Maeneo yatakayoboreshwa | Mo atoa tamko zito | Ahmed atamba
Hitimisho
Simba SC 2-0 B19 FC CRDB Federation Cup yanaipa timu hiyo tiketi kusonga hatua ya 16 bora. Mabingwa watetezi Yanga SC vs Polisi Tanzania ni mchezo unaofuata kwenye ratiba. Je mafahari hawa wawili watakutana fainali? Matokeo yataamua kila hatua.

