- Tanzania Premier League 2025/26 Depu ameanza kazi
- Yanga SC 6-0 Mashujaa FC NBC Premier League, Januari 19,2026
- Mudathir Yahya achaguliwa kuwa mchezaji bora, Allen Okelo kwenye majukumu mapya
Yanga SC 6-0 Mashujaa FC NBC Premier League matokeo rasmi ya mchezo wa mzunguko wa kwanza. Wababe hawa wawili walikuwa wakitafuta pointi Uwanja wa KMC Complex. Magoli ya Yanga SC yamefungwa na Mohamed Damalo dakika ya 8, Duke Abuya dakika ya 28, Pacome Zouzoua dakika ya 35, Prince Dube dakika ya 79, Mudathir Yahya dakika ya 80 na Depu dakika ya 89.
SOMA HII: Yanga SC haijapoteza mechi 2025/26 NBC Premier League / Kariakoo Dabi inanukia, matokeo, rekodi
Je hujashinda? Cheza ‘Kindege’ cha SportPesa uvune mamilioni sasa hivi
Sasa ni zamu yako, unaweza kushinda hadi mamilioni muda huu. Cheza mchezo wa ‘aviator’ maarufu kama Kindege. Kushiriki mchezo huu bonyeza picha hii chini.

Yanga SC 6-0 Mashujaa FC NBC Premier League yaandika rekodi

Ushindi wa Yanga SC 6-0 Mashujaa FC NBC Premier League umeandika rekodi mpya ndani ya 2026. Unakuwa ni ushindi mkubwa kwa mabingwa hao watetezi wa taji la NBC Premier League. Mshambuliaji mpya Depu akicheza mchezo wa kwanza amefungua ukurasa wa magoli.
Mbali na Yanga SC kuvuna pointi tatu, wanaandika rekodi kuishusha kileleni JKT Tanzania iliyofunga 2025 ikiwa namba moja. Kufikisha pointi 19 kunawapa nafasi kupanda mpaka namba moja. Wajeda JKT Tanzania wanachukua nafasi ya pili wakiwa na pointi 17, tofauti ya pointi moja.
Huu hapa msimamo
| Timu | P | W | D | L | P | GF |
| 1.Yanga SC | 7 | 6 | 1 | 0 | 19 | 18 |
| 5. Mashujaa FC | 10 | 3 | 4 | 3 | 13 | 5 |
Mudathir mchezaji bora

Kiungo wa Yanga SC, Mudathir Yahya amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo. Baada ya dakika 90 alikabidhiwa tuzo yake kutoka kwa wadhamini wa ligi. Hiyo yote imetokana na kutimiza majukumu yake kwa umakini.
Kwenye ushindi wa magoli 6-0 waliyopata watoto wa Jangwani, Mudathir alifunga goli moja. Kamati imepitisha jina la nyota huyo ambaye alikuwa kwenye kiwango bora. Inakuwa ni tuzo ya kwanza kwa Mudathir 2026.
SOMA HII: Ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC) 2025/26, kimataifa ni Al Ahly vs Yanga SC

Kikosi cha Yanga SC kilichoanza vs Mashujaa FC
Langoni
Aboutwalib Mshery
Mabeki
Bakari Nondo
Dickson Job
Kibwana Shomary
Chadrack Boka
Viungo
Maxi Nzengeli
Pacome
Allan Okelo
Mohamed Camara
Duke Abuya
Mshambuliaji
Prince Dube
Wachezaji wa akiba
Balla Conte
Zimbwe Jr
Yao
Hussen Masalanga
Emmanuel Mwanengo
Abdulnassir Mohamed
Frank Assinki
Laulindo
George Mzungu
Kikosi cha Mashujaa FC vs Yanga SC
Erick Johola
Mpoki Mwakinyuke
Samweli Onditi
Abdulnassir Assa
Salum Kihimbwa
Hassan Alli
Mundhir Vuai
Jafari Kibaya
Yusuf Dunia
Mohamed Salum
Samson Madeleke
Wachezaji wa akiba
Daniel Lyanga
Mapinduzi Balama
Mgandila Shaban
Frank Magingi
Lameck Kanyonga
Abdul Bakari
Mudathir Said
Razakc Hussen
Seleman Bwenzi
SOMA HII: Yanga SC haina utani kuwapa mikataba mastaa hawa wa kazi 2025/26

Hitimisho
Yanga SC 6-0 Mashujaa FC rekodi imeandikwa Uwanja wa KMC Complex. Mashujaa FC wamekwama kuangusha Mbuyu kama ambavyo walibainisha awali. Wachezaji wapya wa Yanga SC tayari wameingia kwenye mfumo kutokana na kupata nafasi kwenye mchezo wa leo.

